NA
GENOFEVA MATEMU NA SALOME MAJALIWA
JUMLA ya wagonjwa
22 wenye matatizo ya moyo yatokanayo na mfumo wa umeme wa
moyo usiofanya kazi sawasawa wamefanyiwa upasuaji mdogo na kuwekewa
vifaa maalum vitakavyousaidia moyo kufanya kazi vizuri.
Madaktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo kutoka
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao wa Shirika la Madaktari Afrika
la nchini Marekani wakiandaa vifaa
vitakavyotumika katika upasuaji mdogo wa kumuwekea mgonjwa kifaa maalum cha
kuusaidia moyo kufanya kazi vizuri (Implantable cardioverter defibrillator - ICD)
katika kambi ya matibabu kwa wagonjwa wenye matatizo ya mfumo
wa umeme wa moyo. (PICHA NA GENOFEVA
MATEMU – JKCI)
Madaktari
Bingwa wa Magonjwa ya Moyo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na
wenzao wa Shirika la Madaktari Afrika la nchini Marekani wakiangalia jinsi mfumo wa umeme wa moyo wa
mgonjwa unavyofanya kazi kabla ya kumwekea kifaa maalum cha kuusaidia moyo
kufanya kazi vizuri (Implantable cardioverter defibrillator - ICD) katika
kambi ya matibabu kwa wagonjwa
wenye matatizo ya mfumo wa umeme wa moyo.
Daktari
Bingwa wa Magonjwa ya Moyo kutoka Shirika la Madaktari Afrika la nchini
Marekani Prof. Matthew Sackett akiwaelekeza Madaktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI) jinsi ya kumuwekea mgonjwa kifaa cha kuusaidia moyo kufanya
kazi vizuri (Implantable cardioverter defibrillator - ICD)
katika
kambi maalum ya siku saba ya matibabu kwa wagonjwa wenye matatizo ya mfumo
wa umeme wa moyo.
Madaktari
Bingwa wa Magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao kutoka Shirika
la Madaktari Afrika la nchini Marekani wakimuwekea mgonjwa kifaa cha kuusaidia
moyo kufanya kazi vizuri (Implantable cardioverter defibrillator - ICD))
katika kambi maalum ya matibabu kwa
wagonjwa wenye matatizo ya mfumo wa umeme wa moyo.
Matibabu hayo
yamefanyika katika kambi maalum ya siku saba iliyofanyika katika
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa mgonjwa kufanyiwa upasuaji wa
bila kufungua kifua (Catheterization) kwa kutumia mtambo wa Cathlab.
Akiongea na
waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Kurugenzi ya
Magonjwa ya moyo ambaye pia ni Daktari Bingwa wa Moyo Peter Kisenge alisema
kambi hiyo inafanywa na madaktari wa Taasisi ya Moyo kwa kushirikiana na wenzao
wa nchini Marekani kutoka Shirika la Madaktari Afrika.
Dkt. Kisenge
alisema kambi hiyo ni maalumu kwa ajili ya kuwasaidia wagonjwa wenye matatizo
ya mfumo wa umeme wa moyo ambao mapigo yao yako chini kwa asilimia
hamsini kwa dakika kwa kuwawekea kifaa maalum akinachosaidia mapigo
ya moyo kuongezeka (Pacemaker).
“Kazi ya kifaa
hiki maalum cha mfumo wa umeme wa moyo ni kuwasaidia wagonjwa
wasipoteze maisha ghafla, kwani mara nyingi wagonjwa wenye matatizo ya
mapigo ya moyo ambayo yako chini hufa vifo vya ghafla”, alisema
Dkt. Kisenge.
Kuhusu matibabu
waliyopatiwa wagonjwa katika kambi hiyo Dkt. Kisenge alisema zoezi
limeenda vizuri na kwa ufanisi mkubwa kwa wagonjwa kuwekewa vifaa vya
pacemaker na ICD (Implantable cardioverter defibrillator - ICD) kwa wagonjwa ambao mapigo yao ya moyo
yako chini ya asilimia 30.
Kwa upande wake
Prof. Matthew Sackett kutoka Madaktari Afrika alisema kambi hiyo ilienda
sambamba na utoaji wa elimu kwa madaktari na wataalam wengine wa
afya ambao baada ya mafunzo hayo wataweza kuwawekea wagonjwa kifaa cha
ICD ambapo kabla ya hapo hawakuwa wanaweza kufanya hivyo.
“Wiki hii imekuwa ni wiki ya mafanikio kwetu, tumetibu wagonjwa na nimetoa elimu ya namna ya kumuwekea mgonjwa kifaa cha ICD kwa madaktari na wataalam wengine wa afya, kila nitakapopata nafasi nitakuja kutoa huduma kwa wagonjwa na elimu kwa wafanyakazi”, alisema Prof. Sacckett.



No comments :
Post a Comment