Saturday, August 18, 2018

Fahamu mkutano mkuu wa wadau na miaka 20 ya mfuko wa ZSSF

zssf
zssf

HakiPensheni
zssf

Mkurugenzi Mwendeshaji wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) Sabra Issa Machano akizungumza na vyombo habari siku ya uzinduzi rasmi wa sherehe za kutimiza miaka 20 kwa Mfuko wa ZSSF tangu kuanzishwa kwake mwaka 1998 pamoja na juu ya mkutano mkuu wa wadau utakaofanyika Agosti 20, 2018.

Na Christian Gaya,  majira Ijumaa, 17 Agosti 2018
Njia mojawapo ya wadau wa mifuko ya hifadhi ya jamii ni kufuatilia na kujua utendaji wa mifuko hii inayosimamiwa na bodi za wadhamini kwa njia ya mikutano mikuu inayofanyika kila mwaka. Ambapo wadau kama vile wanachama ambao ndio wachangiaji na waaajiri...
ambao mara nyingi ndio waliodhaminiwa au wakala wa kuhakikisha ya kuwa wanashirikiana na mifuko hii kama vile kusimamia ukataji na kupeleka michango kwenye mifuko ya hifadhi na kuhakikisha ya kuwa wanatunza kumbukumbu za wafanyakazi wao,

Kwa mfano, mfuko wa hifadhi ya jamii ya Zanzibar (ZSSF) umeshaanza kusherehekea miaka 20 tangia kuanzishwa kwake mwaka 1998 na kilele chake kitakuwa ni kumalizia kufanya mkutano mkuu wake wa NNE wa wanachama wa mfuko na wadau mbalimbali wa sekta ya hifadhi ya jamii utakaofanyika tarehe 20 Agosti 2018 kwa ajili ya  kutathmini juu ya mafanikio na changamoto za mfuko ambapo mgeni rasmi atakuwa Makamu wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd.

Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa Zanzibar ulianzishwa chini ya kifungu cha sheria Namba 2 ya mwaka 1998 na baadaye ilirekebishwa chini ya kifungu cha Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar, Sheria Namba 9 ya mwaka 2002 na Sheria Namba 2 ya mwaka 2005. Kabla ya kifungu cha Sheria na uanzishwaji wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar, kulikuwa hakuna rasmi mpango wa kinga ya hifadhi ya jamii katika nchi ya Zanzibar

Hiki ni kipengele mojawapo muhimu cha kuzingatia utaratibu na kanuni za utawala bora hivyo tunaamini ya kuwa mfuko wa ZSSF utaendelea kujenga imani zaidi wakati wa mkutano mkuu kwa wanachama na wadau kwa kuwahakikishia ya kuwa mfuko unaendeshwa na kuongozwa na utawala bora na kwa ufanisi wa hali ya juu zaidi kwa kuendesha mkutano kwa njia ya ukweli na uwazi

Kuna haja ya uongozi wa mifuko ya hifadhi ya jamii kuwa wazi kama kigezo muhimu cha utawala bora kuthibitisha pale uamuzi unapofanywa kwa kuzingatia masilahi ya mfuko kwanza na siyo masilahi binafsi ya viongozi.

Tunaamini ya kuwa mfuko huu wa ZSSF unazingatia kanuni za uongozi bora na ndiyo  maana kwa kufanya hivyo kumekuwa na uwezekano mkubwa kwa mfuko kuwa na utendaji mzuri unaofikia malengo na kukidhi matarajio ya wanachama wake na familia zao. 

ZSSF hivyo tumieni  nafasi hii ya mkutano mkuu wa wadau kwa kuhamasisha  kuanza kupanua wigo zaidi wa hifadhi ya jamii kwa kutoa elimu ya hifadhi ya jamii kwa wanachama, wadau na kwa umma wa Tanzania kwa ujumla kwa njia ya kujenga ushirikiano kati ya wadau ili kuhamasisha wananchi kujiunga na mifuko ya huu wa ZSSF wa hifadhi ya jamii nchini.

Watanzania wengine tumieni fursa hii ya wiki ya mkutano mkuu kwa wanachama na wadau nchini kujifunza na kujielemisha juu ya uhai, utendaji, afya na ustawi wa mfuko wa ZSSF juu ya taarifa zinazohusiana na hesabu, taarifa za ukaguzi wa mahesabu, na taarifa za bodi ya wadhamini wa mifuko na kujua nafasi na uwezo wa mfuko kifedha kwa njia ya magazeti, redio, luninga, blog na njia zingine za mitandao kwani pensheni ni haki yako

ZSSF kwa kutimiza Miaka 20 imekuwa ya mafanikio makubwa ambapo Mfuko umeweza kutimiza majukumu yake ya kulipa mafao bila kulazimika kukopa au kuuza rasilimali zake; kufanya shughuli zake kwa asilimia 70 kwa kutumia teknohama  iliyobuniwa na wafanyakazi wa ndani, pamoja na hayo ZSSF imekuwa ikishiriki kwenye miradi mbalimbali ya uwekezaji yenye manufaa kwa Taifa kiuchumi na kwa kimaendeleo ya kijamii, kwa kupunguza umasikini kama siyo kuondoa umasikini kwa wanachama na wastaafu wake.

Christian Gaya ni mwanzilishi wa Kituo cha HakiPensheni Tanzania, mshauri na mtaalamu wa masuala ya pensheni. Kwa maelezo zaidi: gayagmc@yahoo.com unaweza kutembelea  www.hakipensheni monitor online na hakipensheni blog Simu +255 655 13 13 41 info@hakipensheni.co.tz



No comments :

Post a Comment