Friday, August 31, 2018

PATA VICHWA VYA HABARI TOKA MAGAZETI YA LEO 01 SEPTEMBA 2018




TAASISI YA MOYO YAANZISHA KITENGO CHA HUDUMA KWA MTEJA (CUSTOMER CARE)


Mkurugenzi Mtendaji Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akizungumza na waajiriwa wa kampuni ya Professional Cleaner watakaokuwa wanatoa huduma kwa mteja (customer care) kwa wadau wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa mafunzo mafupi ya utoaji wa huduma bora kwa mteja leo katika ukumbi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa Taasisi hiyo Agnes Kuhenga
Mkurugenzi wa Fedha na Utawala Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Agnes Kuhenga (kushoto) akitoa maelekezo ya namna ya kutoa huduma bora kwa waajiriwa wa kampuni ya Professional Cleaner watakaokuwa wanatoa huduma kwa mteja (customer care) kwa wadau wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa mafunzo mafupi ya utoaji wa huduma bora kwa mteja leo katika ukumbi wa Taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam.

  Mkurugenzi Idara ya Uuguzi Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Robert Mallya (kulia) akitoa mada ya namna ya kupokea wagonjwa kwa waajiriwa wa kampuni ya Professional Cleaner watakaokuwa wanatoa huduma kwa mteja (customer care) kwa wadau wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa mafunzo mafupi ya utoaji wa huduma bora kwa mteja leo katika ukumbi wa Taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam.


Mfanyakazi wa kampuni ya Professional Cleaner ambaye ni mmoja kati ya watoa huduma kwa mteja (customer care) wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Khadija Abeid akielezea namna ambavyo atakua akitoa huduma bora kwa wateja wakati wa mafunzo mafupi ya utoaji wa huduma bora kwa mteja leo katika ukumbi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Jijini Dar es Salaam.(Picha na: Genofeva Matemu)

SHIRIKA LA POSTA TANZANIA LAELEZA MATARAJIO NA MALENGO YAKE KWA MWAKA 2018/2019


Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania (TPC), Kanali Mstaafu, Dk. Haruni Kondo, akizungumza na waandishi wa habari, wakati alipokuwa akielezea masuala mbalimbali yanayohusu matarajio na malengo ya shirika hilo, kwa mwaka 2018/2019. Kushoto ni Postamasta Mkuu wa shirika, Hassan Mwang’ombe.  
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Elia Madulesi, akizungumza wakati akiwakaribisha waandishi wa habari katika mkutano ambao Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika, Kanali Mstaafu, Dk. Haruni Kondo, alielezea mambo mbalimbali yanayohusu matarajio na malengo ya shirika hilo, kwa mwaka 2018/2019, jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Postamasta Mkuu, Hassan Mwang'ombe na kushoto ni Kaimu Meneja Mkuu Rasilimali za Shirika Macrice Mbodo.
Baadhi ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari, wakichukua taarifa iliyokuwa ikitolewa na  Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania, Kanali Mstaafu, Dk. Haruni Kondo. 
Baadhi ya wapiga picha na waandishi wa habari, wakichukua taarifa kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta, Kanali Mstaafu, Dk. Haruni Kondo.
Baadhi ya wapiga waandishi wa habari, wakisikiliza taarifa  iliyokuwa ikitolewa na Mwenyekiti wa Bodi, Kanali Mstaafu, Dk. Haruni Kondo. 
Mwenyekiti wa Bodi, Kanali Mstaafu, Dk. Haruni Kondo (katikati), akizungumza na waandishi katika mkutano huo.  
Postamasta Mkuu, Hassan Mwang'ombe, akizungumza katika mkutano huo, wakati alipoelezea kuhusu duka la Shirika la kwenye mtandao kwamba sasa tayari linafanya kazi na kuwataka wananchi kulitumia kwa kuweka bidhaa zao ili kuweza kuuza ndani na nje ya nchi. Kulia Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika, Kanali Mstaafu, Dk. Haruni Kondo.
Maofisa wa Kitengo cha Mawasiliano cha Shirika la Posta Tanzania (TPC),wakiwa katika mkutano huo, wakimsikiliza Postamasta Mkuu wa shirika hilo, Hassan Mwang'ombe, alipokuwa akizungumza katika mkutano huo, jijini Dar es Salaam leo. 
Postamasta Mkuu, Hassan Mwang'ombe,akizungumza wakati alipokuwa akijibu maswali yaliyokuwa yakiulizwa na waandishi wa habari katika mkutano huo,jijini Dar es Salaam leo.   
Mwenyekiti wa Bodi, Kanali Mstaafu, Dk. Haruni Kondo akijibu maswali yaliyokuwa yakiulizwa na waandishi wa habari katika mkutano huo.   

MUHIMBILI WATOA KIWANJA CHA UJENZI WA KITUO CHA POLISI MLOGANZILA


 Kaimu Kamishna wa Fedha na Lojistiki, DCP Leonard Paul na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi shirikishi Muhimbili Prof. Andrea Pembe wakibadilishana nyaraka baada ya kusaini makubaliano ambapo Chuo hicho kimelipatia Jeshi la Polisi eneo la ekari mbili katika Kampasi ya Mloganzila kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Polisi.Makubalino hayo yalisainiwa Makao Makuu ya Polisi Dar es Salaam.
 Kaimu Kamishna wa Fedha na Lojistiki, DCP Leonard Paul na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi shirikishi Muhimbili Prof. Andrea Pembe wakisaini makubaliano ambapo Chuo hicho kimelipatia Jeshi la Polisi eneo la ekari mbili katika Kampasi ya Mloganzila kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Polisi.Makubalino hayo yalisainiwa Makao Makuu ya Polisi Dar es Salaam

Kaimu Kamishna wa Fedha na Lojistiki, DCP Leonard Paul na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi shirikishi Mhimbili Prof. Andrea Pembe wakizungumza baada ya kusaini makubaliano ambapo Chuo hicho kimelipatia Jeshi la Polisi eneo la ekari mbili katika Kampasi ya Mloganzila kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Polisi.Makubalino hayo yalisainiwa Makao Makuu ya Polisi Dar es Salaam.(Picha na Jeshi la Polisi)


 Kaimu Kamishna wa Fedha na Lojistiki, DCP Leonard Paul na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi shirikishi Mhimbili Prof. Andrea Pembe wakionyesha nyaraka baada ya kusaini makubaliano ambapo Chuo hicho kimelipatia Jeshi la Polisi eneo la ekari mbili katika Kampasi ya Mloganzila kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Polisi.Makubalino hayo yalisainiwa Makao Makuu ya Polisi Dar es Salaam.

Maofisa kutoka Makao Makuu ya Polisi na viongozi wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi shirikishi Mhimbili  wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kusaini makubaliano ambapo Chuo hicho kimelipatia Jeshi la Polisi eneo la ekari mbili katika Kampasi ya Mloganzila kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Polisi.Makubalino hayo yalisainiwa Makao Makuu ya Polisi Dar es Salaam.(PICHA NA JESHI LA POLISI)

NAIBU WAZIRI MAVUNDE AIPONGEZA SEKTA BINAFSI KWA MCHANGO MKUBWA KATIKA UKUAJI WA SEKTA YA VIWANDA NA FURSA YA AJIRA

  NA MWANDIHI MAALUM

NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi,Vijana na Ajira Mh Anthony Mavunde ameishukuru sekta binafsi kwa mchango mkubwa inaoutoa katika sekta ya Uchumi wa Viwanda na fursa za Ajira inazozitengeneza kupitia uwekezaji.

Naibu Waziri Mavunde ameyasema hayo katika uzinduzi wa muonekano mpya wa kinywaji kikali cha K-VANT katika Hotel ya Serena Jijini Dar es salaam ambapo pia amechukua fursa hiyo kuipongeza kampuni ya MEGA BEVERAGES kwa kutoa fursa za AJIRA kwa wananchi zaidi ya 1000 na pia kwa uwekezaji wa kiwanda cha kuzalisha vinywaji na kuitaka kampuni hiyo kuzingatia ubora ili kuifanya bidhaa yao kuwa shindani na kuvuka mipaka ya Tanzania.

Akimkaribisha Mgeni Rasmi,Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni MEGA BEVERAGES Bw. Francis Kimaro ameishukuru Serikali kwa mazingira wezeshi yaliyofanikisha uwekezaji huo wa kiwanda na kuahidi kuzalisha bidhaa zenye ubora.






MAKAMU WA RAIS AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA MAWAZIRI JIJINI DODOMA LEO TAREHE 31 AGOSTI 2018.


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiongoza kikao cha Baraza la Mawaziri , kushoto ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein, kikao hicho kimefanyika kwenye ukumbi wa TAMISEMI, Mkapa House leo jijini Dodoma.
 Kikao kikiendelea
 Kikao kikiendelea
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Kangi Lugola (kushoto) akizungumza na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega kabla ya kuanza kwa kikao cha Baraza la Mwaziri katika ukumbi wa TAMISEMI jijini Dodoma.

  Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Subira Mgalu (kulia) akizungumza na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji muda mfupi kabla ya kuanza kikao cha Baraza la Mawaziri katika ukumbi wa TAMISEMI jijini Dodoma. (PICHA NA OFISI YA MAKAMU WA RAIS)

16 WANAODAIWA KUKWAPUA FEDHA ZA USHIRIKA WILAYANI HAI ,WAWEKWA NDANI KWA AMRI YA DC SABAYA


Mkuu wa wilaya ya Hai,Lengai Ole Sabaya akizungumza wakati wa mkutano wa utoaji wa taarifa ya uchunguzi wa kamati iliyoundwa na mkuu huyo kuchunguza ubadhilifu wa fedha za Ushirika wa watumia maji katika kijiji cha Mijongweni.
Mkuu wa wilaya ya Hai,Lengai Ole Sabaya akiwahoji baadhi ya wajumbe wa serikali ya kijiji cha Mijongweni kuhusiana na ubadhilifu uliofanyika katika Ushirika huo.
Mkuu wa wilaya ya Hai,Lengai Ole Sabaya ,akizungumza juu ya maamuzi yaliyochukuliwa mara baada ya kamati aliyoiunda kuwasilisha taarifa yake.
Baadhi ya wananchi wakisikiliza kwa makini juu ya maamuzi yaliyochukuliwa na Mkuu huyo wa wilaya .
Baadhi ya wananchi wakionesha mabango yenye ujumbe mbalimbali wakati wa mkutano huo.
Katibu tawala wa wilaya ya Hai,Upendo Wera akizungumza katika mkutano huo.
Mmoja wa wakazi wa kijiji cha Mijongweni ,Omary Mohamed akizungumza kwa niaba ya wananchi wengine katika mkutano huo.
Mkuu wa wilaya ya Hai,Lengai Ole Sabaya akitizama baadhi ya mashine zilizotolewa kwa Ushirika huo ambazo zinatajwa kutumika huku mapato yake hayajulikani yalipo.
Moja ya Mashine hizo ikiwa tayari imeharibika baada ya kuondolewa Roller inayotumika kwa ajili ya kutembelea.
Mashine mpya ya Ushirika huo ambayo haijaanza kutumika bado.
Baadhi ya watuhumiwa wa ubadhilifu wa fedha za Mradi wa Ushirika huo wakiwa kwenye gari la Polisi mara baada ya kukamatwa wakiwa eneo la mkutano.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii,Kanda ya Kaskazini.


-WADAIWA KUFANYA UBADHILIFU WA ZAIDI YA MIL 200.
-WENGINE WAUZA VIPURI VYA MASHINE.
WATU 16 wakiwemo viongozi wa Bodi ya Ushirika wa Umoja wa watumia maji katika kijiji cha Mijongweni (UWAMI) wanashikiliwa na Jeshi la  Polisi kwa amri ya mkuu wa wilaya ya Hai,Lengai Ole Sabaya  wakituhumiwa kuhusika na ubadhilifu wa fedha za mradi zaidi ya