Saturday, August 18, 2018

KOFI ANNAN AFARIKI DUNIA



Mashirika ya Habari

KATIBU Mkuu wa zamani wa  Umoja wa Mataifa (UN) na mshindi wa tuzo ya amani ya Nobel, Kofi Annan (pichani)amefariki dunia leo Agosti 18, 2018 akiwa na umri wa miaka (80), wakfu wake umethibitisha.

Annan ambaye amezaliwa nchini Ghana mwaka 1938 amehudumu kama Katibu Mkuu wa 7 wa Umoja wa Mataifa (UN) kutoka mwaka 1997 hadi mwaka 2006 na alikuwa ni mmoja wa zao la watumishi wa UN kufikia nafasi hiyo.

Alikuwa mmoja wa wanakundi la Wazee wa Dunia (Kundi la Viongozi  wa Dunia), lililojikita katika masuala ya kutetea haki za binadamu tangu lilipoanzishwa mnamo mwaka 2007, na mwaka 2013 Annan alikuwa Mwenyekiti wa kwanza wa kundi hilo.

Wakfu wa marehemu Kofi Anna, umethibitisha kutokea kwa kifo chake kwa masikitiko makubwa kupitia ukurasa wake wa tweter.

“Ann amefariki kwa amani Jumamosi asubuhi baada ya kuugua kwa muda mfupi, pembeni yake akiwepo mkewe Nane na watoto wao watatu wakati wa siku zake za mwisho,” umesema Wakfu wake


No comments :

Post a Comment