Waziri wa Madini Mhe. Angellah
Kairuki (Mb) akihutubia washiriki wa hafla ya uzinduzi wa Tume ya
Madini leo Jijini Dodoma ambapo alikuwa mgeni rasmi .
Mwenyekiti wa Tume ya Madini Prof.
Idrissa Kikula akihutubia washiriki wa wa hafla ya uzinduzi wa Tume
ya Madini leo Jijini Dodoma ambapo Waziri wa Madini Mhe. Angellah
Kairuki (Mb) alikuwa mgeni rasmi .
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt.
Binilith Mahenge akisisitiza kuhusu fursa zilizopo Mkoani Dodoma wakati
wa wa hafla ya uzinduzi wa Tume ya Madini leo Jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya
Bunge ya Nishati na Madini Mhe. Dustan Kitandula akizungumzia manufaa
ya kuanzishwa kwa Tume ya Madini wakati wa hafla ya uzinduzi wa Tume
hiyo leo Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Madini Prof.
Simon Msanjila akitoa hotuba ya kumkaribisha Waziri wa Madini Mhe.
Anjellah Kairuki Kuzindua Tume ya Madini leo Jijini Dodoma.
Waziri wa Madini Mhe. Angellah
Kairuki (Mb) akifurahia jambo na Mwenyekiti wa Tume ya Madini Prof.
Idrissa Kikula wakati akimkabidhi vitendea kazi mara baada ya Kuzindua
Tume hiyo leo Jijini Dodoma.
Waziri wa Madini Mhe. Angellah
Kairuki (Mb) akimkabidhi vitendea kazi Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume
hiyo Prof. Shukrani Manya mara baada ya Kuzindua Tume hiyo leo Jijini
Dodoma.
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania
Prof. Florens Luoga ( kushoto) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dkt.
Aderladus Kilangi( kulia) Wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Madini
ambaye alikuwa mgeni rasmi wakati wa hafla ya uzinduzi wa Tume ya
madini leo Jijini Dodoma.
Makamishana wa Tume hiyo
wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Madini Mhe. Angellah Kairuki (Mb)
ambaye alikuwa mgeni rasmi wakati wa hafla ya kuzindua Tume hiyo leo
Jijini Dodoma.
Waziri wa Madini Mhe. Angellah
Kairuki (Mb) akimkabidhi Vitendea kazi mmoja wa Makamishna wa Tume hiyo
Dkt. Florence Turuka ambaye pia ni Katibu Mkuu Wizara ya Ulinzi na
Jeshi la Kujenga Taifa wakati wa hafla ya uzinduzi wa Tume ya Madini leo
Jijini Dodoma.
Waziri wa Madini Mhe. Angellah
Kairuki (Mb) akiwa kwenye picha ya pamoja na Makamishna wa Tume ya
Madini mara baada ya Kuzindua Tume hiyo leo Jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Madini Mhe. Dotto
Biteko (kushoto) akiteta jambo na Waziri wa Madini Mhe. Anjellah Kairuki
wakati wa hafla ya kuzindua Tume hiyo iliyofanyika leo Jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na
Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt. Anjelina Mabula akiteta jambo na Naibu
Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Elias Kuandikwa wakati wa
hafla ya uzinduzi wa Tume ya Madini leo Jijini Dodoma.
(Picha zote na Frank Mvungi- MAELEZO , Dodoma
……………….
Frank Mvungi- MAELEZO, Dodoma
Tume ya Madini imetakiwa
kuhakikisha inatekeleza kikamilifu jukumu la usimamizi, Udhibiti,
Ukaguzi, Ufuatiliaji, Ukusanyaji wa taarifa na kuweka kumbukumbu kwa
kusimamia sekta hiyo
kwa uadilifu hali itakayosaidia Taifa kunufaika na
uwepo wa rasilimali madini.
Akizungumza wakati akizindua Tume
hiyo Jijini Dodoma, Waziri wa Madini Mhe. Angellah Kairuki amesema kuwa
kuzinduliwa kwa Tume hiyo kunaashiria kuanza kwa ukurasa mpya katika
sekta ya madini nchini kwa kuwa uamuzi huo ni mapinduzi makubwa hali
itakayosaidia wananchi kunufaika na sekta hiyo.
“Ni imani yangu, na pia ni imani
ya Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli na imani ya Watanzania wote
kuwa mtatubadilishia simulizi za sekta ya madini kutoka kuwa za
kukatisha tamaa na kuwa za matumaini, kuibadili historia ya sekta ya
madini kutoka kuwa ya miguno na manunguniko na kuwa yakujivunia”
Alisisitiza Mhe. Kairuki
Akifafanua Mhe. Kairuki amesema
kuwa, si kwamba Tume hiyo imepewa mamlaka makubwa bali pia imepewa imani
kubwa kwa kuwa mamlaka makubwa yanakuja na wajibu mkubwa mikononi mwa
watendaji wa Tume hiyo.
Aliongeza kuwa Watanzania wana
matarajio makubwa na Tume hiyo na viongozi wake kwa kuwa Serikali na
wananchi wanaamini kuwa sekta hiyo sasa iko katika mikono safi na
salama.
Kutokana na imani hiyo Mhe.
Kairuki amesema kuwa wananchi wanaamini Tume hiyo itatenda haki,
kusimamia ukweli na kuzingatia maslahi ya kizazi hiki na kijacho ili
viweze kunufaika na madini ambayo Mwenyezi Mungu amelijalia Taifa letu.
Aidha, Mhe. Kairuki ameitaka Tume
hiyo kuhakikisha inasimia kikamilifu wachimbaji wadogo kwa kuwatambua
na kurasimisha shughuli zao ili sekta hiyo iwanufaishe kama ilivyo azma
ya Serikali ya Awamu ya Tano.
Kwa upande wa vibali vya mauzo ya
madini nje ya Nchi amesema kuwa ni vyema Tume ikafanya mapitio ya fomu
na vibali ili kuhakikisha kuna maelezo na taarifa za kina za madini
yanayosafirishwa kuhusu yalipotoka (origin),.
Vile vile kwa kushirikiana na
vyombo vya ulinzi na usalama ameitaka Tume iandae mbinu na mikakati ya
kudhibiti utoroshaji wa madini ili kudhibiti biashara haramu ya madini.
Tume ya madini imetakiwa kuangalia
uwezekano wa kuweka utaratibu wa kutoa bei elekezi za madini ya aina
mbalimbali ambapo utaratibu huo utawasaidia wachimbaji wadogo na wa
kati.
Pia Mhe. Kairuki ameitaka Tume
hiyo kuhakikisha kuwa kila anayefanya biashara ya madini ana leseni na
ni leseni hai iliyolipiwa na kuhakikisha kwamba inathibiti watu au
makampuni yanayomiliki leseni walizopewa kwa muda mrefu bila
kuziendeleza kinyume na masharti ya leseni hizo.
Kuwepo kwa utaratibu wa kufanya
ukaguzi wa mara kwa mara kuona maendeleo ya uwekezaji katika migodi
ambayo imepata leseni ni moja ya jukumu ambalo Tume hiyo inatakiwa
kulitekeleza.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa
Tume ya Madini Prof. Idrissa Kikula amesema kuwa wamepokea maelekezo
yote ya Serikali na Tume hiyo iko tayari kufanya kazi kwa maslahi ya
Taifa .
Aliongeza kuwa Tume imejipanga
kuhakikisha kuwa inatatua migogoro iliyopo katika sekta hiyo kwa
kushirikisha vyama vyao vilivyopo katika maeneo yao.
Tume ya Madini imeundwa ikiwa ni
sehemu ya juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano kuhakikisha kuwa
rasilimali za Taifa zinawanufaisha wananchi wote, Kutokana na azma hiyo
Tume imepewa jukumu la kusimamia sekta ya madini na Wizara ya Madini
kubaki na Masuala ya kisera.
No comments :
Post a Comment