Saturday, February 4, 2017

ASKARI WA K.A.R WA UINGEREZA AWEKA SHADA LA MAUA KWENYE MNARA WA MASHUJAA


s300_David_Nickol
Na Mahmoud Ahmad Arusha
AFISA mstaafu wa jeshi la kikoloni,King Africa Rifles,(K.A.R) Capten mstaaf, David Nickol (96) kutoka nchini Uingereza,ameweka shada la maua kwenye mnara wa kumbu kumbu ya mashujaa wa vita vya Kagera, jijini Arusha,kwenye hafla fupi iliyoshuhudiwa na Katibu tawala wa mkoa wa Arusha, Richard Kwitega, na maafisa wa ngazi za juu wa jeshi la Ulinzi la wananchi wa Tanzania.
Akizungumza mara baada ya kuweka shada hilo la maua kwenye mnara huo uliopo kwenye bustani ya mkuu wa mkoa wa Arusha ,Nickol,maarufu mwanickol, amesema amekuwa akija nchini kutoka kwao Uingereza, kila mwaka kuja kuweka shada la maua kwenye mnara huo ikiwa ni kumbukumbu na heshima kwa askari wa Tanzania waliokufa wakiwa vitani.
Nickol ,amesema  alikuwa ni mkuu wa wilaya za Arusha, na Singida,  mara tu Tanganyika ilipopata Uhuru wake mwaka 1961kabla ya kustaafu na kurejea kwao  na hivyo ana mapenzi makubwa na Tanzania.
Amesema wakati akiwa askari alishiriki vita ya pili ya dunia,ambapo alipigana kwenye nchi mbalimbali  ikiwemo nchini Burma, Ethiopia ,Madagascan a Somalia ambapo walipata mafanikio makubwa nchini Somalia walipoweza kuwashinda Wataiano,baada ya kupigana kwa muda wa miezi sita  na kukamata mateka wengi.
Nickol,amesema ni jambo la heshima kubwa kwake kuja nchini na kuweka maua kwenye mnara wa askari waliokufa wakiwa vitani na anaishukuru serikali ya Tanzania.
Amesema hakuna nchini nyingine barani afrika anayoiheshimu kama Tanzania kwa kuwa ni nchi yenye Ukarimu,Ustaarabu  na upendo  ameahidi kuja nchini kila mwaka ili kudhuru mnara huo wa mashujaa  na hiyo inatokana na kuthamini na kutambua umuhimu wa askari wa jeshi .
Nae  Balozi wa Uingereza nchini, Richard Beatty Obe, amesema serikali yake itamwezesha  Capten huyo msitaafu kila mwaka kuja nchini Tanzania kudhuru mnara huo wa kumbu kumbu ya mashujaa kuwekashada la  maua .
Kwa upande wake Katibu tawala wa mkoa wa Arusha, Richard Kwitega, amesema hiyo ni heshima pekee kwa Tanzania, kutembelewa na afisa huyo mstaafu wa cheo cha Kapten kutoka Uingereza  na kutembelea mnara wa kumbu kumbu ya askari wa vita ya Kagera.
Amesema  kuwa afisa huyo raia wa Uingereza ana moyo wa kipekee na ni mfano wa kuigwa kutokana na upendo wake alionao kwa Tanzania ,kufunga safari kutoka kwao kuja nchini kwetu na hiyo ni heshima kubwa kwa nchi yetu.

No comments :

Post a Comment