Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania Mhe. Kassim M. Majaliwa akiwa katika mzungumzo na Kamishna
Mkuu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) Bw Filippo
Grandi. Mazungumzo hayo yamefanyika kando na mkutano wa TICAD7
Yokohoma,Japan.
Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi
akifuatilia mazungumzo kati ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mhe. Kassim M. Majaliwa na Kamishna Mkuu wa Shirika la
Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) Bw Filippo Grandi(hayupo pichani)
Yokohama, Japan.
Mazungumzo kati ya Waziri Mkuu wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim M. Majaliwa na Kamishna Mkuu
wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) Bw Filippo Grandi
kuhusu wakimbizi waliopo Tanzania yakiendelea. Yokohama, Japan.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania Mhe. Kassim M. Majaliwa akiagana na Kamishna Mkuu wa
Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) Bw Filippo Grandi mara
baada ya kumalizika kwa mazungumzo baina yao kuhusu wakimbizi waliopo
Tanzania. Mazungumzo hayo yamefanyika Yokohama, Japan.
Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi
akisalimiana na Kamishna Mkuu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani
(UNHCR) Bw Filippo Grandimara baada ya kumaliza kufanya mazungumzo na
Waziri Mkuu mhe. Kassim M. Majaliwa. Yokohama, Japan.
Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akiteta
jambo na Kamishna Mkuu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR)
Bw Filippo Grandi mara baada ya kumalizika mazungumzo ya Waziri Mkuu
mhe. Kassim M. Majaliwa. Yokohama, Japan.
……………….
Tanzania imetoa rai kwa Jumuiya ya
Kimataifa na Japan kuendelea kutafuta suluhu ya kudumu kwenye
changamoto mbalimbalii ambazo bado zinajitokeza kwenye baadhi ya nchi za
Afrika ikiwemo ugaidi wa kimataifa, uhalifu, mabadiliko ya tabianchi,
ukame, njaa na