Monday, July 4, 2022

MWALIMU CHUO CHA VETA KARAGWE ALEZEA WALIVYOTUMIA MCHAICHAI, TANGAWIZI, AMDALASINI KUTENGENEZA WINE

01:Mwalimu wa Ujasiriamali katika Chuo cha VETA-
Karagwe mkoani Kagera Hamiss Jumanne akiwa
ameshika Wine ya Kombucha ambayo imebuniwa
na chuo hicho baada ya kuchanganya Tangawizi,
Mchaichai na Amdalasini .Wine hiyo imekuwa ni ya
kibuni na ladha yake iko tofauti na ladha za wine
nyingine.


 Na Said Mwishehe, Michuzi TV

MWALIMU wa Ujasiriamali katika Chuo cha VETA-

Karagwe mkoani Kagera Hamiss Jumanne amesema

kwamba chuo chao kimekuja na ubunifu wa

kutengeza Wine(Mvinyo) unatokana na tangawizi,

Mchaichai na Amdalasini ambayo ni tofauti kabisa

na aina nyingine za Wine zinazotengenezwa ndani

na nje ya Tanzania.

Akizungumza na Michuzi TV katika Banda la VETA

lililopo kwenye Maonesho ya 46 ya kimataifa ya

Biashara yanayoendelea viwanja vya Sabasaba

mkoani Dar es Salaam Mwalimu Jumanne amesema

katika maonesho hayo yenye ujumbe unaosema

Tanzania ni mahali sahihi kwa uwekezaji na masuala

ya biashara wao VETA –Karagwe wameamua kuja

na ubunifu wa kipee wa kutengeza Wine hiyo.

“Sisi VETA Karagwe tumekuja na kitu cha ubunifu

kabisa na cha kipekee utengenezaji wa Wine kwa

kutumia Mchaichai ,Amdalasini, Rozela pamoja na

Tangazi ,huu ni utofauti mkubwa sana na ubunifu

wa kipee ambao pia tumekuwa tukiwafundisha

wanafunzi wetu kuona thamani ya vituo vingine.

“Wamezoea Mchaichai na Amdalasini unatumika

kwenye chai tu lakini leo kwa ubunifu wetu uko

kwenye Wine , ukiweka Wine kwa namna hii

wanafunzi wakienda mtaani wataamua kujitegea

wenyewe kwasababu watakuwa wamepata maarifa

haya lakini itaongeza thamani na uchumi kwa

wananchi.

“Ule Mchaichai na tangawizi vitalimwa kwa wingi

sana ili waweze kuleta viwandani na viwandani

vingine vinaweza kukua, kumbuka wanafunzi hawa

ndio watakuwa wakurugenzi wa baadae.Kwa hiyo

Wine hii ni tofauti na Wine nyingine kwani tuna

fahamu zipo Wine zinazotengenezwa na Zabibu na

Rozela lakini VETA Karagwe tumekua na Wine

inayotokana na tangawizi, mchaichai na

amdalasini.”

Amesisitiza hivyo Wine hiyo ni ya upekee kabisa

unayoipata wilayani Karagwe Kagera na

inafahamika kwa jina la Kombucha na

mchanganyiko wake pamoja na mambo mengine

umekuwa unasaidia kusafisha na kuimarisha

mishipa, hivyo hata kwenye suala la tendo la ndio

linakuwa liko vizuri lakini hairuhusiwi kwa walio na

umri chini ya miaka 18.

Amefafanua kwa anayetaka Wine hiyo kwa sasa

wako Sabasaba na wanaohitaji wanakaribishwa

banda la VETA.“Lakini unaweza kupiga simu 0759

817029 ina maana ukiwasiliana na sisii basi

tunakuletea popote ulipo kwani Serikali yetu

imerahisisha masuala ya usafiri.

“Sisi kutoka Karagwe basi ikitoka kule asubuhi saa

nane usiku inakuwa imefika Dar es Salaam na Wine

itakuwa imekufikia.Watu wanavutiwa sana kwani

kila ambaye ananunua anarudi tena kutokana na ule

uasili uliomo kwenye Wine yetu.”

No comments :

Post a Comment