Sunday, January 31, 2021

TBL Plc yatoa mifuko 150 ya saruji kufanikisha ujenzi wa madarasa Mwanza

Meneja Mawasiliano wa TBL Amanda Walter akiongea wakati wa hafla hiyo.

Kaimu Mkurugenzi wa manispaa ya Ilemela, Benson Mihayo(wa pili kulia) akipokea mifuko 150 ya Saruji kutoka kwa Meneja wa kiwanda cha bia TBL tawi la Mwanza Mhandisi Godwin Fabian, zilizotolewa na kampuni kwa ajili ya kufanikisha ujenzi wa madarasa katika kata ya

Pasiasi, wengine pichani kushoto ni Meneja Rasilimali watu wa TBL Dora Nyambalya, Meneja Mawasiliano wa TBL Amanda Walter na Afisa mtendaji wa Kata ya Pasiansi Aloyce Mkono(kulia)

………………

Kampuni ya Tanzania Breweries Limited (TBL Plc)  imeendeleza jitihada zake za kuunga mkono jitihada za Serikali za kusaidia shughuli za kijamii ambapo mwishoni mwa wiki imetoa msaada wa mifuko 150 ya saruji kwa ajili ya kufanikisha ujenzi wa madarasa katika  kata ya Pasiasi iliyopo mkoani Mwanza.

Akiongea katika hafla ya kukabidhi msaada huo iliyofanyika jijini Mwanza, Meneja Mawasiliano wa TBL Plc, Amanda Walter  alisema kuwa kampuni itaendelea kuunga mkono jitihada za Serikali kwa lengo la kuboresha huduma za kijamii hususani katika sekta ya elimu, Afya, mazingira sambamba na kutoa  elimu kwa jamii kuhusiana na masuala ya usalama barabarani na matumizi ya vinywaji vyenye kilevi kistaarabu.

Kaimu Mkurugenzi wa manispaa ya Ilemela, Benson Mihayo alishukuru kwa msaada huo ambao alisema umetolewa kwa wakati mwafaka ambapo zoezi la ukamilishaji wa majengo ya madarasa katika kata  hiyo unaendelea

 

No comments :

Post a Comment