Thursday, October 1, 2020

ACP MARWA ASHIRIKI HAFLA YA KUWAVISHA VYEO MAAFISA 10 NA ASKARI 5 WA KIKOSI DHIDI YA UJANGIRI KUSINI SONGEA

Kamanda wa Polisi mkoa wa Ruvuma Simon Maigwa Marwa akikagua gwaride rasmi  katika hafla fupi ya kuwavisha vyeo maafisa 10 na askari 5 wa kikosi dhidi ya ujangili na wa pori la akiba la Liparamba wilayani Mbinga hafla iliyofanyika katika ofisi ya kikosi cha kuzui ujangili kanda ya Kusini Songea,kushoto mkuu wa gwaride hilo mhifadhi mwandamizi Joseph Ruben.

Meneja wa pori la akiba Liparamba wilayani Mbinga Nollasco Ngowe kushoto, akimvisha cheo kipya mhifadhi mwandamizi wa mamlaka ya Uhifadhi Wanyamapori Tanzania(TAWA)Joseph Ruben jana, ambapo maafisa 10 na askari 5 kikosi cha dhidi ya ujangili na pori la akiba Liparamba walivishwa vyeo mbalimbali hafla iliyofanyika katika ofisi za kikosi cha kuzuia ujangili kanda ya kusini Songea.

Picha na Mpiga Picha Maalum

 

No comments :

Post a Comment