Thursday, September 3, 2020

TOTAL YAWEZESHA WATAZANIA KUMILIKI VITUO VYA NISHATI YAMAFUTA


Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mafuta ya Total Tanzania Jean Francoius akiangalia mfumo wa Oil katika gari iliyopita kupata huduma wakati uzinduzi ampapo mwenye gari amepata kuwekewa mafuta bure na kuwekewa Oil.
Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kampuni Marsha Msuya-Kilewo akizungumza namna wanavyoingia Ubia na watanzania katika umiliki wa vituo vya nishati ya mafuta wakati uzinduzi wa kituo cha mafuta cha Total Mchigani Goba jijini Dar es Salaam.
Mmiliki wa Kituo cha Mafuta Total Mchigani Goba Mhandisi Frank Malle akizungumza kuhusiana namna alivyowezeshwa na Kampuni ya Mafuta Total kumiliki kituo hicho ,jijini Dar es Salaam.
Mliliki wa Kituo cha mafuta cha Total Mchigani Goba Mhandisi Frank Malle akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Total Jean Francois wakikata utepe kuashilia uzinduzi wa kituo hicho jijini Dar es Salaam.
Wafanyakazi wa Kampuni ya Total wakiwa katika picha ya pamoja na Mmiliki wa Kituo cha Mafuta na baadhi ya wgeni waalikwa katika uzinduzi huo,jijini Dar es Salaam.

Na Chalila Kibuda, Michuzi TV

Kampuni ya Mafuta ya Tatal imesema kuwa iko katika mikakati ya kuwawezesha Watanzania umiliki wa vituo vya mafuta katika maeneo ambayo yanaweza kufanya biashara hiyo kwa kuwawezesha kufanya biashara .

Mkakati wa kuwawezesha watanzania kumiliki vituo vya mafuta unahitaji watanzania 100 lakini hadi sasa ni watanzania Nane wamewezeshwa kuwa na vituo vya mafuta kwa kigezo kuwa na ardhi pamoja na mwenye ardhi kuwekeza katika ujenzi.

Akizungumza wakati wakati wa uzinduzi kituo cha mafuta  cha Mchigani Goba jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mafuta ya Total  Tanzania Jean Francoius amesema kuwa Mmilki wa Kituo cha mafuta hicho Mhandisi Frank Malle amepata katika mfumo wa DODO ambao kampuni imekuja nao katika kuhakikisha watanzania wanakuwa sehemu ya kumiliki vituo vya mafuta.

DODO ni mfumo wa kibiashara ni mfumo wa kibiashara ambao kampuni ya Total kutumia katika kuongeza mtandao vituo vya nishati ya mafuta nchini unaowezesha wafanyabiashara kuingia katika mfumo wa ubia na kuweza kumilki ,kuendesha pamoja na kusimamia vituo vya huduma ya mafuta vyenye chapa ya Total.

Amesema kuwa wameweka kituo hicho ikiwa ni kuhakikisha wananchi wa Goba wanapata mafuta yenye kiwango bora na vilainishi  bila kusahau basi za kubeba abiria zinazotumia barabara ya Goba katika safari za Mbezi Mwisho ,Tegeta  pamoja na Kimara.

Francocius amesema kuwa Kampuni ya Total wanauzoefu wa biashara ya nishati ya  mafuta nchini   zaidi ya miaka 50   ikiwa na mtandao nchi nzima  na kuwa na vituo vya Total pekee unaoweza kupata mafuta yenye excellium yenye uwezo wa kusafisha injini pamoja na oli kutoka kwa wataalam wabobevu waliotayari kutoa huduma.

Nae Mmiliki wa Kituo cha Mafuta Frank Malle amesema kuwa katika maisha yake hajawahi kufikiria kufanya biashara ya mafuta lakini Total imemwezesha kuwa miongoni mwa watazania wanaomiliki vituo vya mafuta.

Amesema wazo hilo lilikuja kutokana na ardhi aliyeinunua kwa ajili ya makazi zilitokea kampuni nne za mafuta zikitaka eneo kisha kwenda Total na kuweza kuingia kupata utalaam na kuwezeshwa umiliki huo.

Malle amesema anawashukuru Total kwa uwezeshaji wa kuwa na kituo cha mafuta na kuahidi kuendelea kufanya biashara hiyo kwa kuongeza vituo vingine.

Nae Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kampuni Marsha Msuya-Kilewo amesema kuwa wanaendelea na mkakati wa kuweza kufika vituo 100 vya mafuta kwa watazania kumiliki ambapo hadi sasa ni vituo Nane tu.

No comments :

Post a Comment