Thursday, September 3, 2020

CHUO CHA MAENDELEO YA MIPANGO VIJIJINI :TUNAHITAJI KUWA WATAALAM WENGI KATIKA MIPANGO


 Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Mipango Vijijini Profesa Hozen Mayaya akizungumza na waandishi habari kuhusiana na ushiriki wa maonesho ya vuo vikuu yanayofanyika katika  viwanja vya mnazi Mmoja.
Msajili wa Wanafunzi Profesa Mirabless Malila akitoa maelezo namna wanavyotoa elimu bora kwa wanafunzi kwa kuwa wahadhili wabobevu katika Nyanja ya mipango.

Na Chalila Kibuda,Michuzi TV
CHUO cha Maendeleo ya Mipango Vijijini Dodoma kimesema maendeleo yeyote ili yaweze kutokea kunahitaji kuwepo kwa mipango hivyo I chuo pekee  kilichojikita katika kutoa elimu katika eneo hilo

Akizungumza na waandishi wa habari katika Maonesho ya  Vyuo Vikuu  jijini Dar es Salaam Mkuu wa Chuo hicho Profesa  Hozen Mayaya amesema kuwa katika maonesho ni kuleta wanafunzi pamoja  kusoma elimu  iliyojikita kusukuma maendeleo ya nchi  katika uandaji wa mipango.

Amesema wamekuwa na kozi za muda mrefu na kozi za muda mfupi ambapo wanafunzi wakihitimu wanaweza kuendelea na shahada katika kuongeza uwigo kuwa mwanataaluma bora katika mipango na hadi shahada ya uzamivu.

Mayaya amesema kuwa katika eneo lingine walilojikita ni pamoja na kutoa ushauri ambapo katika ushauri huo kwa kushirikiana na  UNDP wanajenga kiwanda cha kutengeneza Barafu kanda ya Ziwa katika kuchochea mandeleo ya uvuvi wa samaki kwa kuhakikisha samaki hawaozi.

Hata hivyo  amesema kuwa katika kutoa elimu pia wanafanya utafiti  mbalimbali wa kuweza kuwasaidia watanzania kuondokana na umasikini katika maeneio mbalimbali ikiwemo sekta ya kilimo na maeneo waliyofanya katika wilaya  Mbulu kumekuwa na matokeo chanya ya kilimo cha vitunguu Swaum.

Profesa Mayaya amesema kuwa katika utoaji wa elimu nchini wanampongeza Rais Dkt. John  Pombe Magufuli kwa kuifikisha nchi katika Uchumi wa kati kwa muda ambao haukutarajia kufika kama nchi.

Aidha amewataka wazazi na wanafunzi kusoma Chuo hicho ili kuweza kuja kuisaidia nchi katika upangaji wa maedeleo na hatimaye  nchi kwenda kwenda uchumi wa juu zaidi kwa kushirikiana na viongozi wa wa nchi.

Mkuu wa Chuo Profesa Mayaya amesema katika maonesho yajayo watakuja na matokeo ya taifiti kama serikali ilivyoagiza ili kuonyesha uhalisia wa vitu wanavyofanya katka chuo hicho.

No comments :

Post a Comment