Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya
Ujenzi) Arch. Elius A. Mwakalinga (wa pili kulia) akipewa maelezo kuhusu
vitendea kazi vipya vya karakana mara baada ya kuvizindua na Kaimu
Mkurugenzi wa Idara ya Matengenezo na Huduma za Ufundi Mhandisi
Sylvester Simfukwe, kushoto ni Mtendaji Mkuu TEMESA Mhandisi Japhet Y.
Maselle na Mwenyekiti wa Bodi ya ya Ushauri ya Wakala wa Ufundi na Umeme
(TEMESA) Prof. Eng. Idrissa B. Mshoro. Hafla hiyo imefanyika katika
karakana ya Mt. Depot Keko jijini Dar es Salaam.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi)
Arch. Elius A. Mwakalinga katikati akikata utepe pamoja na viongozi
waandamizi wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) kuzindua rasmi
vitendea kazi vipya vya karakana katika hafla iliyofanyika karakana ya
Mt. Depot Keko jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y.
Maselle akisoma taarifa kuhusu utendaji wa karakana katika hafla ya
uzinduzi na usambazwaji wa vitendea kazi vya karakana iliyofanyika
karakana ya Mt. Depot Keko jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi) Arch. Elius A. Mwakalinga
aliyenyoosha mkono akisistiza jambo wakati akikagua vitendea kazi vya
karakana katika hafla ya uzinduzi na usambazwaji wa vitendea kazi hivyo
iliyofanyika karakana ya Mt. Depot Keko jijini Dar es Salaam. Kushoto ni
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y.
Maselle
Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya
Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Prof. Eng. Idrissa B. Mshoro
akisisitiza jambo wakati akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi na
usambazwaji wa vitendea kazi vya karakana iliyofanyika karakana ya Mt.
Depot Keko jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Mameneja wa vituo na
mikoa mbalimbali wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) wakimsikiliza
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya
Ujenzi) Arch. Elius A. Mwakalinga (hayupo pichani) alipokua akizungumza
wakati wa hafla ya uzinduzi na usambazwaji wa vitendea kazi vya karakana
iliyofanyika karakana ya Mt. Depot Keko jijini Dar es Salaam.
**********************************
Serikali kupitia Wakala wa Ufundi
na Umeme (TEMESA) imetenga kiasi cha shilingi bilioni 9,538,970,000/=
katika bajeti ya mwaka wa fedha 2020/2021 kwa ajili ya miradi ya
maendeleo ya karakana kutoka Mfuko Mkuu wa Serikali (GOT) ili kuboresha
na kuimarisha
miundombinu na vitendea kazi kwenye karakana kwa aijili ya
kukidhi matarajio ya wateja.
Hayo yamebainishwa leo na
Mtendaji Mkuu wa Wakala huo Mhandisi Japhet Y. Maselle wakati wa hafla
fupi ya uzinduzi na usambazaji wa vitendea kazi vipya vya karakana
ambavyo vinatarajiwa kusambazwa katika mikoa 14 nchini.
Awali, akizungumza katika
hafla hiyo ambayo imefanyika katika karakana ya MT. Depot iliyopo Keko
jijini Dar es Salaam, mgeni rasmi, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi) Arch. Elius A. Mwakalinga
ameupongeza uongozi na menejimenti ya Wakala kwa kuweza kufanikisha
ununuzi wa vitendea kazi hivyo na kuongeza kuwa vitendea kazi hivyo
vitaongeza chachu ya utendaji kazi wa karakana za Wakala wa kiasi
kikubwa.
“Kupata vitendea kazi ni moja,
lakini lakini kuvitumia sasa vile vitendea kazi ili kuleta matokeo
chanya kwa wahitaji wa huduma inayotokana na vitendea kazi hivi ndio
jambo la msingi” alisema Katibu Mkuu ambapo aliagiza vifaa hivyo
visambazwe haraka sana kwa mameneja husika ili vikaanze kazi mara moja.
Aliongeza kuwa Wizara imepanga kutengeneza karakana mpya mkoani Dodoma
ambayo itakuwa karakana ya mfano kwenye utoaji wa huduma bora na za
kisasa zaidi.
“Tukishaitengeneza ile na
tukaridhika sasa kwingine kote kutafwatia, na kwa mwaka huu wa fedha
tumeshatenga bilioni 3 kwa ajili ya kazi hizo”.
Awali akisoma taarifa kuhusu
ununuzi wa vitendea kazi hivyo katika hafla hiyo, Mtendaji Mkuu wa
Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle alisema
vitendea kazi hivyo vimegharimu serikali kiasi cha Tsh 430,823,810.23 na
vitagawiwa katika mikoa/vituo 14 ambavyo ni
Dar es salaam (Vingunguti),
Mtwara, Mara, Simiyu, Kagera, Tabora, Iringa, Rukwa, Manyara, Arusha,
Kilimanjaro, Tanga, Songwe na Same.
“Katika mwaka wa fedha
2019/2020 tulipokea kiasi cha Tsh 2,533,080,000/= kutoka Serikalini
kupitia Wizara kwa ajili ya miradi ya maendeleo kwenye karakana”.
Alisema Mhandisi Maselle ambapo aliishukuru Serikali kwani kwa kupitia
agizo la Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Kassim
Majaliwa (Mb) la kuzitaka taasisi zote zinazodaiwa na TEMESA ziwe
zimelipa madeni yao kufikia Julai 30, 2020, kiasi cha Tshs.
771,496,076.39 zimelipwa kati ya Tshs 25,882,593,038/= zilizokuwa
zinadaiwa.
Naye Mwenyekiti wa Bodi ya ya
Ushauri ya Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Prof. Eng. Idrissa B.
Mshoro, akizungumza katika hafla hiyo alisema anaishukuru Wizara ya
Ujenzi kwa kuendelea kuhakisha Wakala unaendelea kutoa huduma bora kwa
taasisi za Serikali na binafsi hasa katika kugharamia utekelezaji wa
miradi mbalimbali ya maendeleo ya TEMESA.
No comments :
Post a Comment