Monday, September 7, 2020

BALOZI IBUGE AKUTANA NA BALOZI WA CHINA, ITALIA NCHINI



Balozi wa China nchini Mhe. Wang Ke akimueleza jambo Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi, Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge wakati walipokutana kwa majadiliano leo jijini Dar es Salaam
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi, Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akiongea na Balozi wa China nchini Mhe. Wang Ke
Balozi wa Italia nchini, Mhe. Roberto Mengoni akiongea na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi, Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge
Balozi wa Italia nchini, Mhe. Roberto Mengoni akimsikiliza Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi, Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge.
************************************
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa China nchini Mhe. Wang Ke pamoja na Balozi wa Italia nchini Mhe. Roberto Mengoni katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu, Balozi Ibuge amesema kuwa pamoja na mambo mengine, waliweza kujadili umuhimu wa kuongeza ushirikiano hussusan katika sekta ya biashara na uwekezaji pamoja na utalii.  
“Tumezungumzia kuhusiana na miradi mbalimbali ambayo tumekuwa tukishirikiana na China katika kukuza maendeleo endelevu,” amesepa Balozi Ibuge
Balozi Ibuge ameongeza kuwa Tanzania na China zitaendelea kuimarisha mashirikiano katika sekta za kilimo na utalii kwa sababu ni sekta ambazo zikiimarishwa vizuri zaidi zitakuza uchumi haraka zaidi.
Nae Balozi wa China, Mhe. Wang Ke amesema kuwa Serikali ya China imejidhatiti kuimarisha uhusiano wake na Tanzania hasa baada ya janga la COVID 19 ili kuhakikisha kuwa nchi hizi mbili zinakuwa na uchumi imara.
Katika tukio jingine, Katibu Mkuu Balozi Ibuge amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Italia nchini, Mhe. Roberto Mengoni ambapo wamejadiliana mambo mengi yanaohusiana na kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na China.
“Italia na Tanzania ni marafiki wa muda mrefu katika mazungumzo yetu tumejadili namna ya kuimarisha mashirikano na namna ya kuendeleza na kuboresha sekta za biashara na uwekezaji, elimu na utalii,” amesema Balozi Ibuge.
Kwa upande wake Balozi Mengoni amesema kuwa wamejadili mambo mbalimbali ya kuimarisha uhusiano na kukubaliana kuendelea kufanya kazi kwa pamoja ili kukuza uchumi wa mataifa yetu.
Viongozi hao wamejadiliana na kubaliana kuendelea kuimarisha ushirikiano wa kihistoria baina ya mataifa hayo mawili ambao umejikita katika sekta za elimu,   utalii pamoja na biashara na uwekezaji.

No comments :

Post a Comment