Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani(kushoto) Katibu
Mkuu Wizara ya Nishati, Mhandisi Zena Said wakiwa kwenye kikao Pamoja
na wataalamu mbalimbali kutoka TANESCO(hawapo pichani) kabla ya kuanza kwa ukaguzi wa ujenzi wa Mradi mkubwa wa kufua Umeme kwa maji wa Julius Nyerere(JNHPP)
Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani(mwenye shati la bluu) Naibu
Waziri wa Ujenzi wa Misri, Jenerali Mahmoud Nassar,(mwenye suti) wakiwa
na wataalamu mbalimbali kutoka nchini Tanzania na Misri wakiangalia
picha mbalimbali za Mradi mkubwa wa kufua Umeme kwa maji wa Julius
Nyerere(JNHPP)
Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani(aliyesimama) akizungumza kwenye kikao baina ya ujumbe kutoka Serikali ya Tanzania na Misri kabla ya kuanza kwa ukaguzi wa ujenzi wa Mradi mkubwa wa kufua Umeme kwa maji wa Julius Nyerere(JNHPP),Septemba 6,2020.(kushoto) Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Mhandisi Zena Said(kulia) Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Tanesco Dkt Alexander Kyaruzi.
Katibu Mkuu Wizara ya Nishati,
Mhandisi Zena Said(kulia) Kaimu Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu
Edward Ishengoma wakiwa katika kikao baina ya ujumbe kutoka Serikali ya
Tanzania na Misri kabla ya kuanza kwa ukaguzi wa ujenzi wa Mradi mkubwa wa kufua Umeme kwa maji wa Julius Nyerere(JNHPP),Septemba 6,2020.
Naibu Waziri wa Ujenzi wa Misri, Jenerali Mahmoud Nassar akizungumza
na Waandishi wa Habari mara baada ya kumaliza kukagua wa ujenzi wa
Mradi mkubwa wa kufua Umeme kwa maji wa Julius Nyerere(JNHPP),Septemba
6,2020.(kulia) Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani.
Ujumbe kutoka katika Serikali ya
Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani na ujumbe
kutoka nchini Misri wakiongozwa na Naibu Waziri wa Ujenzi wa Misri,
Jenerali Mahmoud Nassar wakikagua maeneo mbalimbali ya ujenzi wa Mradi
mkubwa wa kufua Umeme kwa maji wa Julius Nyerere(JNHPP)
…………………………………………………..
Hafsa Omar-Morogoro
Waziri wa
Nishati, Dkt Medard Kalemani, amesema ujenzi wa Mradi mkubwa wa kufua
Umeme kwa maji wa Julius Nyerere(JNHPP) utakamilika kwa wakati na kwa
kiwango cha
kimataifa.
Ameyasema hayo,
Septemba 6,2020, wakati alipofanya ziara ya ukagua wa maendeleo ya
ujenzi wa mradi huo unaotekelezwa kwenye mto Rufiji.
Katika ziara yake
hiyo, aliambatana na Naibu Waziri wa Ujenzi wa Misri,Jenerali Mahmoud
Nassar, Katiku Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Zena Said, Kaimu
Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu Edward Ishengoma, Mwenyekiti wa
Bodi ya Wakurugenzi Tanesco Dkt Alexander Kyaruzi, Mkurugenzi Mtendaji
Tanesco Dkt Tito Mwinuka na wataalamu mbalimbali kutoka nchini Tanzania
na Misri.
Aidha,ameeleza
kuwa tayari Serikali imemlipa mkandarasi wa mradi huo zaidi ya trilioni
1.49, ambayo ni sawa na asilimia 100 ya malipo ambayo mkandarasi huyo
analitakiwa kulipwa kwasasa, ili kuhakikisha anafanya kazi kwa kasi na
kwa kiwango cha kimataifa.
“Tunataka mradi
ukamilike kwa wakati na kwa kiwango cha juu, sio mradi unakamilika
baada ya miezi miwili unanza kuhitaji tena ukarabati kwa gharama
nyengine kwa hili hatutakubali kwahiyo nitoe wito kwa mkandarasi kufanya
kazi kwa weledi na kiwango cha juu”alisema.
Amesema kuwa ,
Serikali imekuwa ikifuatilia kwa ukaribu utekelezaji wa mradi huo, ili
kuhakikisha mradi huo unakamilika ndani ya muda ulipooangwa na kumtaka
mkandarasi kuongeza kasi ya ujenzi katika mradi huo.
Katika juhudu za
kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa wakati, Dkt. Kalemani ametoa
maagizo kwa mkandarasi Pamoja na msimamizi wa mradi huo, maagizo hayo
ni pamoja na kuwataka waatalamu wote waliofanya kazi kwenye mradi huo
kufanya kazi kwa bidii na kumaliza kazi zao kwa wakati.
Pia, amemtaka
mkandarasi wa mradi huo kuhakikisha kuwa ifikapo mwisho wa mwezi huu awe
tayari amemaliza ujenzi wa handaki ujenzi huo ambao ameuelezea kuwa
muhimu ambao unategemewa kwa kiasi kikubwa kuendesha mradi huo.
Vilevile,
amemtaka mkandarasi huyo kuhakikisha anajiri waatalamu wote ambao
wanahitajika katika ujenzi wa mradi huo na ifikapo mwisho wa mwezi huo
wawe tayari wamefika nchini kwaajili ya ujenzi huo.
“ hatuna wasiwasi
na ajira zinazotelewa hapa kwenye mradi hadi sasa umeajiri watanzania
zaidi ya 4500 kati ya watanzania 5500 na kwa wale waliobaki waajiri ili
kazi ziweze kwenda kwa haraka”alimesema Dkt Kalemani.
Pia, ameagiza
uharakishwaji wa ujenzi ya nyumba za wafanyakazi ambazo bado ujenzi
wake haujakamilika na kumtaka mkandarasi huyo kuzikamilisha kwa haraka
ili wafanyakazi wa mradi huo wahamie katika eneo hilo ambapo itasaidia
kufanya kazi zao kwa muda mrefu na mradi huo kukamilika mapema.
Dkt Kalemani,
amesema kuwa mradi huo ndio utakaotatua matatizo yote ya umeme nchini na
kuahidi Serikali itasimamia kikamilifu ujenzi wa mradi huo ambao
utakuwa na faida kubwa na utapunguza changamoto za umeme na utasaidia
sana usambazaji wa umeme kwenye vijiji na vitongoji nchini.
Kwa upande
wake, Naibu Waziri wa Ujenzi wa Misri, Jenerali Mahmoud Nassar, amesema
Rais wa nchi yao anafuatilia kwa karibu utekelezaji wa mradi huo na yupo
tayari kuhakikisha kuwa mradi huo unakamilika kwa wakati.
Aidha, amesema
kuwa mradi huo utakamilika kwa mafanikio makubwa kwasababu ya
ushirikiano mkubwa wanaopata kutoka kwa Watanzani, na kueeleza kuwa
mradi huo utakapokamilika utaleta maendeleo makubwa nchini.
Pia, amesema
changamoto zote zilizojitokeza kwenye mradi huo watazifanyia kazi ili
kuhakikisha mradi huo unakamika wa kwa muda uliopangwa.
Naye,Katibu Mkuu
Wizara ya Nishati, Mhandisi Zena Said amesema maendeleo ya mradi huo ni
mazuri na changamoto zilizojitokeza zitafanyiwa kazi na kuwataka
Watanzania kuendelea kuunga mkono mradi huo wenye faida nyingi katika
katika Taifa letu.
No comments :
Post a Comment