Katibu Mkuu Wizara ya
Maji Mhandisi Anthony Sanga akizungumza wakati akifunga Mkutano Mkuu wa
17 wa Mwaka wa Wahandisi uliokwenda na kaulimbiu isemayo “Katika
mapinduzi ya 4 ya Viwanda vipi uelekeo katika kukabiliana na changamoto
za dunia” uliofanyika jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa bodi ya
usajili wa Wahandisi nchini (ERB) Prof. Ninatubu Lema,akizungumza wakati
akifunga Mkutano Mkuu wa 17 wa Mwaka wa Wahandisi uliokwenda na
kaulimbiu isemayo “Katika mapinduzi ya 4 ya Viwanda vipi uelekeo katika
kukabiliana na changamoto za dunia” uliofanyika jijini Dodoma.
Msajili wa Bodi ya
Usajili wa Wahandisi, Patrick Barozi,akitoa tathimini wakati kufunga
Mkutano Mkuu wa 17 wa Mwaka wa Wahandisi uliokwenda na kaulimbiu isemayo
“Katika mapinduzi ya 4 ya Viwanda vipi uelekeo katika kukabiliana na
changamoto za dunia” uliofanyika jijini Dodoma.
Sehemu ya washiriki
wakifatilia hotuba ya Katibu Mkuu Wizara ya Maji Mhandisi Sanga wakati
akifunga Mkutano Mkuu wa 17 wa Mwaka wa Wahandisi uliokwenda na
kaulimbiu isemayo “Katika mapinduzi ya 4 ya Viwanda vipi uelekeo katika
kukabiliana na changamoto za dunia” uliofanyika jijini Dodoma.
…………………………………………………………………
Na.Alex Sonna,Dodoma
Na.Alex Sonna,Dodoma
Katibu Mkuu Wizara ya
Maji Mhandisi Anthony Sanga ametoa rai kwa taasisi zote nchini
kuhakikisha zinakuwa na Mpango kabambe wa kutenga bajeti ili kuwawezesha
wahitimu wa
vyuo vikuu wa fani ya uhandisi kujishikiza katika taasisi
hizo Mara tu wanapohitimu kabla ya kupata ajira kuliko kuzurura mtaani.
Mhandisi Sanga ameyasema
hayo jana jijini Dodoma wakati akifunga mkutano Mkuu wa 17 wa Mwaka
wa Wahandisi uliokwenda na kaulimbiu isemayo “Katika mapinduzi ya 4 ya
Viwanda vipi uelekeo katika kukabiliana na changamoto za dunia”
“Katika kutoa motisha na
kuwapa moyo vijana kuipenda fani ya uhandisi ni lazima kuangalia mbinu
pindi wanapohitimu wasiwe wa kuzurura njia sahihi ni kuwaandalia
mazingira hivyo ni vyema taasisi kuaandaa bajeti ya kuwawezesha
kujishikiza katika taasisi hizo kabla ya kuajiriwa kuliko kuwaacha
wanazurura mtaani kwani fani ya uhandisi ni nyeti mno kwa maendeleo ya
taifa”amesema.
Aidha,ametumia fursa hiyo kuwakumbusha wahandisi waliokula kiapo cha uaminifu kuhakikisha wanazingatia maadili ya taaluma yao .
Pia Mhandisi Sanga
amewapongeza Wahandisi kote nchini kwa kufanikisha Tanzania kuivusha
katika uchumi wa kati na kubainisha kuwa uwezo waliojengewa Wahandisi
katika mkutano huo utakuwa chachu kwa maendeleo ya Taifa.
Kuhusu
ufuatiliaji,Mhandisi Sanga ameitaka bodi ya Usajili ya Wahandisi
kuhakikisha inafuatilia kwa makini na muafaka maazimio kwa ajili ya
kufanya mrejesho baadae .
Kwa upande wake
Mwenyekiti wa bodi ya usajili wa Wahandisi nchini (ERB) Prof. Ninatubu
Lema amesema karibu washiriki 3500 wameshiriki mkutano huo wa Mwaka
wakiwamo washiriki 500 waliokuwa wakifuatilia kwa njia ya mtandao kutoka
maeneo tofauti ya dunia.
Hata hivyo Prof.Lema
amebainisha baadhi ya mapendekezo yaliyotokana na mkutano huo kuwa ni
pamoja na kuwa na chombo kitakachokuwa kinashauri upande wa
Effort(Kanda),uhitaji wa kubadili mitaala ya Elimu kuanzia chini hadi
juu ili TAIFA linufaike na mapinduzi ya Viwanda .
Prof. Lema ametaja
mapendekezo mengine ni pamoja na Kuifanya Dodoma kuwa jiji la mfano kwa
kupendeza na miundombinu iliyobora (Smart City),kuhamasisha Sera ili
ziende kwenye Usajili na ziweze kutekelezwa
Akitoa neno la shukrani
kwa niaba ya Wahandisi kote nchini,Mhandisi Mohammed Jaye kutoka
Zanzibar ameshukuru kwa Serikali kwa kuendelea kuimarisha mkutano kwa
kila Mwaka.
No comments :
Post a Comment