*********************************
Na Mwandishi wetu, Rufiji
Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt.
Medard Kalemani akiwa katika ziara ya kukagu utekelezaji wa Mradi wa
kufua umeme kwa maji wa Julius Nyerere (JNHPP) Leo Septemba 7, amesema
kuwa
mradi huo unatarajiwa kuwa injini itakayochochea ukuaji wa shughuli
za kimaendeleo na uchumi wa Taifa kwa kasi kubwa.
Aliongeza kuwa, Mradi huo wa
JNHPP, utazalisha umeme wa bei nafuu wa Jumla ya Megawati 2115 ambazo
zitatumika katika shughuli mbalimbali kiuchumi na kimaendeleo na hivyo
kuongeza kasi ya maendeleo na ukuaji wa uchumi wa Taifa.
Utekelezaji wa Mradi huu Mkubwa na
wa kimkakati ulianza Mwezi Juni 2019 na unatarajiwa kukamilika mwezi
Juni 2022. Lengo la Serikali ni kuhakikisha mradi wa Julius Nyerere
unakamilika ndani ya wakati Alisema Dkt. Kalemani.
Aidha, Waziri Kalemani aliendelea
kwa kueleza kuwa, kulingana na mpango kazi uliopo, Serikali ya Tanzania
imeshamlipa Mkandarasi anayetekeleza mradi huo zaidi shilingi trilioni
1.49 ambayo ni sawa na asilimia 22 ya malipo yote ya mradi.
Hata hivyo, katika mwaka wa fedha
2020/21, Serikali tayari imetenga kiasi cha Shilingi za Tanzania
Trilioni 1.44 kwaajili ya kuendeleza shughuli za Mradi wa huo.
Kwa mujibu wa Dkt. Kalemani, mradi
wa JNHPP utakuwa ni kama injini ya uchumi wa Tanzania, kwani kukamilika
kwake kunatarajiwa kushusha bei ya umeme na kukuza uwekezaji hasa sekta
ya viwanda nchini itakayozalisha ajira pamoja na kuongeza vipato vya
wananchi pamoja na pato la Taifa.
Mradi wa Julius Nyerere
unatekelezwa kwa kutumia fedha za ndani ambazo ni kiasi cha shilingi
trilioni 6.558 mpaka kukamilika kwake.
Mradi huu pia, utasaidia kuhifadhi mazingira na kupunguza ukataji wa miti kutokana na kushuka kwa gharama za umeme.
Aliongeza kuwa, mradi wa JNHPP
ndio utakao tatua matatizo ya umeme nchini hivyo kukamilika kwake kuna
tija kubwa sana kwa Taifa na Mwananchi mmoja mmoja kwa ujumla.
Katika ziara hiyo, Waziri Kalemani
aliambatana Naibu Waziri wa Ujenzi Misri Mhandisi Jenerali Mohmoud
Nassar, Katibu Mkuu Nishati Mhandisi Zena Said, Kaimu Kamishna wa Umeme
na Nishati Jadidifu, Edward Ishengoma, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi
TANESCO Dkt. Alexander Kyaruzi, Mkurugenzi Mtendaji TANESCO Dkt. Tito
Mwinuka na Naibu Mkurugenzi Uwekezaji TANESCO Mhandisi Khalid James.
No comments :
Post a Comment