Monday, September 7, 2020

WANAHABARI MAHIRI UANDISHI WA HABARI ZA HALI YA HEWA WATUNUKIWA TUZO


IMG_6130
Baadhi ya wanahabari washindi wa tuzo za habari za Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) wakiwa katika picha na Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dk. Buruhani Nyenzi pamoja na wajumbe wa bodi ya TMA. Kutoka kulia ni Bw. Jerome Risasi (Clouds Media mshindi wa pili), Bi. Theopista Nsanzugwako (Mshindi wa kwanza)  na Bw. Daniel Samson (Mshindi wa tatu) walioshika vyeti.


IMG_6079
 Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dk. Buruhani Nyenzi (kushoto) akimkabidhi cheti mshindi wa kwanza wa tuzo za umahiri wa uandishi wa habari za hali ya hewa, Bi. Theopista Nsanzugwako.


IMG_6073
Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dk. Buruhani Nyenzi (kushoto) akimkabidhi cheti mshindi wa pili wa tuzo za umahiri wa uandishi wa habari za hali ya hewa, Bw. Jerome Risasi kutoka Clouds Media.
 
IMG_6107
Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dk. Buruhani Nyenzi akizungumza kwenye hafla ya tuzo hizo kwa wanahabari iliyoandaliwa na TMA. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Dk. Agnes Kijazi.


 


IMG_6084
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Dk. Agnes Kijazi (kulia) akizungumza kwenye hafla ya tuzo na semina ya wanahabari iliyoandaliwa na TMA.


IMG_6059
Ofisa Uhusiano wa TMA, Bi. Monica Mutoni akielezea mchakato wa tuzo hizo kabla ya washindi kutangazwa.
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tuzo kwa wanahabari bora wa uandishi wa habari za Hali ya Hewa nchini kwa mwaka 2020. Wanahabari watatu wamebahatika kushinda
tuzo hizo zilizotolewa jijini Dar es Salaam.
Akizungumza leo wakati akikabidhi tuzo hizo, Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dk. Buruhani Nyenzi alisema TMA inatambua mchango mkubwa wa wanahabari katika kuhabarisha umma juu ya taarifa za mamlaka hiyo na ndio maana imeanza kutoa motisha kwao.
Mwanahabari alieibuka mshindi wa kwanza ni Bi. Theopista Nsanzugwako kutoka Gazeti la Habari Leo, na Bw. Jerome Risasi kutoka Clouds Media kushika nafasi ya pili, huku nafasi ya tatu ikinyakuliwa na Bw. Daniel Samson mwandishi wa habari kutoka Mtandao wa Nukta.
Aidha Dk. Nyenzi aliwataka wanahabari walioshinda kutumia tuzo hizo kama chachu ya kuongeza umahiri na uandishi wa habari za hali ya hewa, na wale ambao hawakushinda safari hii kuongeza bidii ili kuleta ushindani zaidi katika tuzo zijazo.
Amesema TMA itaendelea kuziboresha tuzo hizo na kuwaomba wanahabari kujitokeza zaidi katika shindano lijalo ambalo muda ukifika litatangazwa tena. Awali akitangaza namna washindi walivyopatikana katika mchuano huo, Ofisa Uhusiano wa TMA, Monica Mutoni alisema timu ya majaji wa tuzo hizo ilitangaza muda wa kupokea kazi za wanahabari kabla ya kuzichakata na kuibuka na washindi.
Utoaji wa tuzo hizo leo ulienda sambamba na warsha ya wanahabari, kuhusu mwelekeo wa msimu wa mvua za vuli kwa kipindi cha mwezi Oktoba hadi Disemba 2020 nchini, iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania, Ubungo Plaza, Dar es Salaam

No comments :

Post a Comment