KATIBU Mkuu Wizara ya
Elimu,Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo akizungumza katika
hafla ya uzinduzi wa mafunzo ya umahiri wa ufundi simu za mkononi pamoja
na mtaala wa mafunzo hayo iliyofanyika leo jijini Dodoma.
Mkuu wa wilaya ya Dodoma Mjini
Josephat Maganga kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Dkt Binilith Mahenge
,akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa mafunzo ya umahiri wa
ufundi simu za mkononi pamoja na mtaala wa mafunzo hayo iliyofanyika leo
jijini Dodoma.
Mkurugenzi Mkuu wa VETA Mhandisi
Pancras Bujulu,akitoa taarifa katika hafla ya uzinduzi wa mafunzo ya
umahiri wa ufundi simu za mkononi pamoja na mtaala wa mafunzo hayo
iliyofanyika leo jijini Dodoma.
Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya TEHAMA
Bw.Samson Mwela akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa mafunzo ya
umahiri wa ufundi simu za mkononi pamoja na mtaala wa mafunzo hayo
iliyofanyika leo jijini Dodoma.
Mkuu wa chuo cha Teknolojia Dar es
Salaam(DIT) Prof. Preksedil Ndomba,akizungumza wakati wa hafla ya
uzinduzi wa mafunzo ya umahiri wa ufundi simu za mkononi pamoja na
mtaala wa mafunzo hayo iliyofanyika leo jijini Dodoma.
Mwenyekiti mafundi simu mkoani
Dodoma Emmanuel Msangi akielezea jinsi baadhi ya a mafundi simu zaidi ya
200 mkoani Dodoma waliopata mafunzo hayo.
Mwenyekiti wa mafundi simu Kanda
ya Ziwa Maguha Manyanda Butonyole akitoa neno wakati wa hafla ya
uzinduzi wa mafunzo ya umahiri wa ufundi simu za mkononi pamoja na
mtaala wa mafunzo hayo iliyofanyika leo jijini Dodoma.
Sehemu ya washiriki wakifatilia
hafla ya uzinduzi wa mafunzo ya umahiri wa ufundi simu za mkononi pamoja
na mtaala wa mafunzo hayo iliyofanyika leo jijini Dodoma.
KATIBU Mkuu Wizara ya
Elimu,Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo akizindua mafunzo ya
umahiri wa ufundi simu za mkononi pamoja na mtaala wa mafunzo hayo
iliyofanyika leo jijini Dodoma.
KATIBU Mkuu Wizara ya
Elimu,Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo,akimkabidhi Kitabu
Mkurugenzi Mkuu wa VETA Mhandisi Pancras Bujulu mara baada ya kuzindua
mafunzo ya umahiri wa ufundi simu za mkononi pamoja na mtaala wa
mafunzo hayo iliyofanyika leo jijini Dodoma.
KATIBU Mkuu Wizara ya
Elimu,Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo,akimkabidhi Muongozo
wa Kitabu Mkuu wa chuo cha Teknolojia Dar es Salaam(DIT) Prof.
Preksedil Ndomba mara baada ya kuzindua mafunzo ya umahiri wa ufundi
simu za mkononi pamoja na mtaala wa mafunzo hayo iliyofanyika leo
jijini Dodoma.
KATIBU Mkuu Wizara ya
Elimu,Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo akiwa katika picha
mbalimbali za pamoja mara baada ya kuzindua mafunzo ya umahiri wa
ufundi simu za mkononi pamoja na mtaala wa mafunzo hayo iliyofanyika leo
jijini Dodoma.
……………………………………………………………………………
Na.Alex Sonna,Dodoma
KATIBU Mkuu Wizara ya
Elimu,Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo amezindua mafunzo ya
umahiri wa ufundi simu za mkononi pamoja na mtaala wa
mafunzo hayo.
Akizungumza katika hafla hiyo Dkt.
amewataka mafundi hao kuzingatia mafunzo yatakayotolewa ili wakafanye
kazi kwa weledi na kujitengenezea ajira na uchumi wao,badala ya
kufikiria kupata leseni na cheti pekee.
Hata hivyo Dkt.Akwilapo amewataka
kufikiria zaidi kujiendeleza baada ya kuhitimu mafunzo hayo ya VETA
ambayo yatatolewa kwa wiki tano kwa ufadhili wa Mamlaka ya Mawasiliano
nchini (TCRA).
“Lakini takwimu za mwaka 2012 zinaonyesha watumiaji wa simu
za mkononi walikuwa milioni 17,takwimu za sasa zinaonyesha watumiaji hao
wamefikia milioni 48 hivyo wigo wa Mawasiliano unaendelea
kupanuka.”amesema Dkt.Akwilapo
Aidha Dkt.Akwilapo ametoa wito kwa
taasisi zingine kushirikiana na VETA katika kuwezesha mafunzo ya
mafundi simu huku akiwaasa wanufaika mafunzo kutoishia kwenye mafunzo
na vyeti bali wawe chachu ya kuboresha huduma .
Naye Mkurugenzi Mkuu wa VETA
Mhandisi Pancras Bujulu amesema kuwa mafunzo hayo yamelenga kuongeza
tija na kuinua zaidi uchumi wa viwanda kupitia tehama.
Kwa upande wake mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa TCRA John
Daffa amesema TCRA imeanzisha mitaala wa mafunzo simu ili kurasimisha
shughuli za utengenezaji simu na kupunguza wimbi la.wizi wa simu za
mkononi.
Mkuu wa chuo cha Teknolojia Dar
es Salaam(DIT) Prof. Preksedil Ndomba amesema kuwa DIT imejipambanua
kuwa taasisi ya Elimu ya juu katika Teknolojia na kuwaasa kusoma kwa
bidii.
Mkuu wa wilaya ya Dodoma Mjini
Josephat Maganga kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Dkt Binilith Mahenge amesema
kuwa mafunzo hayo yatasaidia vijana kujiajiri wenyewe
Mwenyekiti mafundi simu mkoani
Dodoma Emmanuel Msangi amesema kuna mafundi simu zaidi ya 200 mkoani
Dodoma waliopata mafunzo lengo ni kupanua wigo wa ajira kwa vijana huku
Mwenyekiti wa mafundi simu Kanda ya Ziwa Maguha Manyanda Butonyole
akisema kuwa kuanzishwa kwa Chama cha mafundi simu kumebadilisha Maisha
yao .
No comments :
Post a Comment