Mkuu
wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro (wa pili kutoka kushoto)
akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Kusini Pemba Mhe. Hemed Suleiman kabla
ya kuanza kwa kikao kazi na wadau wa vyama vya siasa, viongozi wa dini,
viongozi wa Kamati ya ulinzi na usalama pamoja na wadau wengine wa
uchaguzi kisiwani Pemba. Picha na Jeshi la Polisi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro, akizungumza na baadhi
ya wadau wa vyama vya siasa, viongozi wa dini, viongozi wa Kamati ya
ulinzi na usalama pamoja na wadau wengine wa uchaguzi (hawapo pichani)
leo kisiwani Pemba wakati alipokuwa kwenye ziara ya kikazi ambapo
aliwataka wadau wote wa uchaguzi pamoja na wananchi kuendelea kudumisha
amani na utulivu kwenye kisiwa hicho. Picha na Jeshi la Polisi.
Mkuu
wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro, Kamishna wa Polisi Zanzibar
CP Mohamed Hassan wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa
dini baada ya kumaliza kikao kazi pamoja na wadau wa vyama vya siasa,
viongozi wa dini, viongozi wa Kamati ya ulinzi na usalama pamoja na
wadau wengine wa uchaguzi leo kisiwani Pemba wakati alipokuwa kwenye
ziara ya kikazi ambapo aliwataka wadau wote wa uchaguzi pamoja na
wananchi kuendelea kudumisha amani na utulivu kwenye kisiwa hicho. Picha
na Jeshi la Polisi.
No comments :
Post a Comment