Friday, September 4, 2020

CAMFED YATOA ELIMU YA BIASHARA KWA WASICHANA TOKA WILAYA TANO


Mkuu wa Idara ya Miradi wa CAMFED, Bi. Nasikiwa Duke (kushoto) akitoa mafunzo ya elimu ya biashara na ujasiriamali kwa wasichana kutoka katika Wilaya tano za Tanzania, yaani Wilaya za Morogoro, Chalinze, Handeni Mjini na Vijijini pamoja na Wilaya ya Pangani.
Meneja Mradi wa Maendeleo ya Ujasiriamali wa CAMFED, Sylvester Mselle (mbele) akizungumza leo katika semina ya mafunzo ya elimu ya biashara na ujasiriamali kwa wasichana kutoka katika Wilaya tano za Tanzania, yaani Wilaya za Morogoro, Chalinze, Handeni Mjini na Vijijini pamoja na Wilaya ya Pangani.
Mkuu wa Idara ya Miradi wa CAMFED, Bi. Nasikiwa Duke (kulia) akitoa mafunzo ya elimu ya biashara na ujasiriamali kwa wasichana kutoka katika Wilaya tano za Tanzania, leo jijini Dar es Salaam.
Na Joachim Mushi, Dar
SHIRIKA la CAMFED Tanzania limetoa mafunzo ya elimu ya biashara na ujasiriamali kwa wasichana kutoka katika Wilaya tano za Tanzania, yaani Wilaya za Morogoro, Chalinze, Handeni Mjini na Vijijini pamoja na Wilaya ya Pangani.
Akiendesha mafunzo hayo leo jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Idara ya Miradi wa CAMFED, Bi. Nasikiwa Duke amesema mafunzo hayo yanafanyika kwa siku tano na baada ya hapo kundi hilo la wasichana wanufaika litaenda kuendesha mafunzo kama hayo ngazi ya kata wanazotoka kwa ajili ya kueneza elimu hiyo zaidi.
Aliwataka vijana hao na wengine nchini kujitambua wenyewe binafsi na kuwa na malengo katika maisha yao ikiwa ni pamoja na kutambua kwamba Serikali ipo kwa ajili ya kuwawezesha ili waweze kufikia malengo yao kupitia fursa anuai. 
“…Kimsingi kila kijana akiwa na malengo yake, nahaki ya kufika ofisi za halmashauri na kutembelea idara ya maendeleo ya jamii na idara ya biashara akapata taarifa kamili jinsi ya kuunda vikundi na konufaika na fursa za mikopo zinazotolewa, na kuziangatia masharti ya mikopo hiyo,” alisisitiza Bi. Duke.
Kwa upande wake, Meneja Mradi wa Maendeleo ya Ujasiriamali wa CAMFED, Sylvester Mselle akizungumza katika mafunzo hayo, alieleza kuwa CAMFED imekuwa ikiwawezesha kundi hilo la vijana ili kuondoka katika mnyororo wa umasikini.
Mkuu wa Idara ya Miradi wa CAMFED, Bi. Nasikiwa Duke (mbele) akitoa mafunzo ya elimu ya biashara na ujasiriamali kwa wasichana kutoka katika Wilaya tano za Tanzania, leo jijini Dar es Salaam.
Picha ya pamoja kati ya sehemu ya washiriki na wawezeshaji kwenye semina ya mafunzo ya elimu ya biashara na ujasiriamali kwa wasichana kutoka katika Wilaya tano za Tanzania.
Alibainisha kuwa wanufaika wa mafunzo hayo ya biashara 25, wanakwenda kutoa mafunzo kwa wasichana takribani 300 ambao watakuwa katika ngazi ya kata kwenye Wilaya zilizotajwa, ambao nao watanufaika na mafunzo ya biashara na ujasiriamali. Alisema mradi huo maalum unawalenga kundi la vijana takribani 26,000 wanufaika wa CAMFED nchin zima kupitia programu ya uwezeshaji kielimu.
Aliongeza kuwa program inayofuata ya uwezeshaji wa wasichana wwanufaika wa CAMFED kibiashara utaongezwa na jumla ya Wilaya 19 kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania itanufaika huku lengo likiwa ni kuwawezesha wasichana wadogo kutoka katika hali ya utegemezi na kujitegemea kiuchumi.

No comments :

Post a Comment