Friday, August 14, 2020

ZAIDI YA SH.MILIONI 700 ZABORESHA MIUNDOMBINU CHUO CHA HOMBOLO


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo akizindua moja la jengo la watumishi wa Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo jijini Dodoma.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo akitoa maelezo kwa fundi anayejenga madarasa yaChuo cha Serikali za Mitaa Hombolo jijini Dodoma.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo akiweka jiwe la msingi katika ujenzi wa madarasa katika  Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo jijini Dodoma.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Madarasa yenye ukumbi wa Mikutano katika Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo jijini Dodoma.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo akizungumza na watumishi pamoja na wanafunzi wa chuo cha Hombolo wakati wa uzinduzi wa  madarasa na nyumba za walimu wa chuo hicho kilichopo nje ya jiji  la Dodoma

Mkuu wa Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo., Dk.Mpamila Madale,akitoa taarifa wakati wa uzinduzi wa  madarasa na nyumba za walimu wa chuo hicho kilichopo nje ya jiji  la Dodoma

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo,akikata utepe kuashiria uzinduzi wa  program ya kutoa shahada ya utawala na menejimenti katika Mamlaka za Serikali za Mitaa,Hombolo mara baada ya kuzindua madarasa na nyumba za walimu wa chuo hicho kilichopo nje ya jiji  la Dodoma

Baadhi ya wanafunzi wakifatilia hotuba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo,wakati wa kuzindua program ya kutoa shahada ya utawala na menejimenti katika Mamlaka za Serikali za Mitaa,Hombolo pamoja na  madarasa na nyumba za walimu wa chuo hicho kilichopo nje ya jiji  la Dodoma

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo,akigawa vyeti kwa wana kikundi cha ngoma mara baada ya kuzindua program ya kutoa shahada ya utawala na menejimenti katika Mamlaka za Serikali za Mitaa,Hombolo pamoja na madarasa na nyumba za walimu wa chuo hicho kilichopo nje ya jiji  la Dodoma

Sehemu ya watuishi wakifatilia hotuba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo,wakati wa kuzindua program ya kutoa shahada ya utawala na menejimenti katika Mamlaka za Serikali za Mitaa,Hombolo pamoja na  madarasa na nyumba za walimu wa chuo hicho kilichopo nje ya jiji  la Dodoma

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo,akiwa katika picha za pamoja mara baada ya  kuzindua program ya kutoa shahada ya utawala na

menejimenti katika Mamlaka za Serikali za Mitaa,Hombolo pamoja na  madarasa na nyumba za walimu wa chuo hicho kilichopo nje ya jiji  la Dodoma

………………………………………………………………………………..

Na.Alex Sonna, Dodoma
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo ameupongeza uongozi wa chuo cha Serikali za Mitaa (LGTI) kwa kutumia Zaidi ya Sh.Milioni 747 zilizotokana na mapato ya ndani ya chuo hicho kuboresha miundombinu ya elimu chuoni hapo na kuongeza mvuto na hamasa kwa wasomi wa kada hiyo nchini.
Mhe.Jafo amebainisha hayo mara baada ya kuweka jiwe la msingi katika uboreshaji huo na kuzindua kwa program ya kutoa shahada ya utawala na menejimenti katika Mamlaka za Serikali za Mitaa, uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano, Hombolo Jijini Dodoma.
Aidha Mhe. Jafo amesema kuwa uongozi wa chuo cha Serikali za Mitaa (LGTI) kwa kutumia mapato ya ndani kujenga kuboresha miundombinu ambayo ni kumbi za miadhara, madarasa na nyumba za waalimu.
“ hatua hiyo ni ya kuigwa kwani ni chuo cha kwanza kilichoweza kupiga hatua ya kujenga majengo kwa kutumia mapato ya ndani jambo ambalo ni lamkipekee nchini”, ameeleza Mhe. Jafo.
Ujezi wa jengo la kwanza la miadhara lenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 500 limegharimu Shilingi milioni 246, ukumbi wa pili umegharimu Shilingi 226, madarasa mawili ambayo kila mmoja linauwezo wa kuchukua wanafunzi 250 linagharimu shilingi milioni 274 na nyumba yenye thamani ya milioni 99,majengo haya yote yamejengwa kwa kutumia “Force Account”
Mhe.Jafo ametoa wito kwa vyuo vyote vya Serikali kuiga mfumo wa Chuo cha Serikali za Mitaa ambao wametumia mapato yao ya ndani kuongeza majengo kwa ajili ya kuwasaidia wanafunzi kuwa katika mazingira mazuri ya kujifunza na kufundishia.
Waziri Jafo amepongeza hatua ya uongozi wa chuo hicho kwa kutekeleza agizo la kuanza kutoa shahada ya kwanza na kusisitiza haja ya chuo hicho kuangalia namna ya kuanza na shahada ya ukutubi ili kuwarahisishia wananchi wanaotaka kujiendeleza au kusoma fani hiyo.

Naye, Mkuu wa Chuo hicho Dkt.Mpamila Madale amesema kuwa uwepo wa ongezeko la wanafunzi limechangia kuongeza mapato ya ndani ambayo yamefanya kuboresha miundombinu ili ikidhi mahitaji ya ongezeko hilo.
Ameeleza kuwa chuo kina mkakati wa kujenga jengo la utawala,ujenzi wa jengo katika tawi la miji ili kuondokana na adha ya kulipa pango inayowakumba kwa sasa ambapo wamekuwa wakilipa Shilingi milioni 75 kwa mwaka
Madale ameongeza kuwa kwa sasa wako katika hatua za kuandaa mitaala kwa ajili ya kuanzisha kozi za shahada ya utawala na rasilimali watu, shahada ya ukutubi na Maendeleo ya jamii.
Kwa upande wake Meneja wa Milki, Mhandisi Frank Massawe amesema katika awamu ya kwanza wameweza kujenga jengo moja lenye nyumba mbili za watumishi ambapo mpango wa chuo ni kujenga majengo 10 kwa kutumia mapato ya ndani.

 

No comments :

Post a Comment