Sunday, August 16, 2020

WANANCHI KIGAMBONI WAIPONGEZA SERIKALI, NSSF

Na MWANDISHI WETU
Baadhi ya wananchi wa Kigamboni, wameipongeza Serikali na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) kutokana na kuusimamia vizuri mradi wa ujenzi wa barabara inayounganisha Daraja la Nyerere ambayo ipo kwenye hatua za mwisho kukamilika.

Walitoa pongezi hizo na kuonesha hisia zao mwishoni mwa wiki mbele ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira, na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama wakati wa ziara ya kukagua ujenzi wa barabara hiyo.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi wenzake, Meja Mstaafu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Adiel Raphael Kaaya, alisema mradi huo ni miongoni mwa miradi ambayo inaonekana dhahiri na kama kuna mtu ambaye ni mmbishi aende akashuhudie ujenzi wa barabara hiyo ambayo ni nzuri na yenye ubora wa hali ya juu.

Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, William Erio, aliishukuru Rais Dkt. Magufuli kwa sababu yanayofanyika ni matokeo ya maelekezo yake baada ya mkwamo wa muda mrefu wa kipande hicho cha barabara.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama, akishuhudia mafundi wakiendelea na kazi ya usambazaji wa lami katika barabara inayounganisha Daraja la Nyerere, Kigamboni, mwishoni mwa wiki.

Mafundi wakiendelea na kazi ya kuweka lami katika barabara inayounganisha Daraja la Nyerere, Kigamboni.Mwendesha Bodaboda, Godfrey Kurumwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ujenzi wa barabara inayounganisha Daraja la Nyerere, ambapo aliipongeza Serikali kwa kukamilisha mradi huo wa barabara.

No comments :

Post a Comment