………………………………………………
Na Silvia Mchuruza, BUKOBA,
Kiasi cha shilingi
bilioni 10 zimetengwa na serikali nchini kwa mwaka huu wa fedha wa
2020-21 kwa ajili ya kuziwezesha taasisi za utafiti wa mazao kutekeleza
shughuli zake kwa ufanisi.
Hayo yameelezwa na
katibu mkuu wizara ya kilimo nchini Jerard Kusaya wakati alipotembelea
kituo cha utafiti Maruku na kwamba taasisi hizo zinao mchango mkubwa
katika kuhakikisha sekta ya kilimo nchini inakua kwa kuongeza uzalishaji
hasa katika mazao ya kimkakati yanayokuwa yamepangwa na serikali kwa
kuzalisha mbegu bora.
Amesema kuwa ili tija
iweze kupatikana kupatikana ni lazima taasisi hizo ziwezeshwe na kwamba
mbali na fedha shilingi bilioni 10 iliyotengwa kwa mwaka huu katika
mwaka wa fedha uliopita serikali imetoa kiasi cha shilingi bilioni 3 na
kwamba matunda yamekuwa makubwa nchini yatokanayo na utafiti wa mazao na
elimu inayotolewa na taasisi hizo.
Kwa upande wake mkuu
wa kituo cha utafiti Maruku Dr,John Sariha amesema kuwa licha ya kituo
hicho kukabiliawa na changamoto ya watumishi bado hali ya uzalishaji
itokanayo na matumizi ya mbegu bora zinazozalishwa na kituo hicho mkoani
Kagera unaongezeka kwa kiasi kikubwa.
No comments :
Post a Comment