Na Silivia Mchuruza, Bukoba
KATIBU mkuu Wizara ya
kilimo Gelard Kusaya ameahidi kutatua changamoto mbalimbali zilizoko
ndani ya uwezo wa Serikali zinazowakabili chuo Cha kilimo Maruku- MATI
kilichoko Bukoba Vijijini mkoani Kagera hususani,maslahi ya watumishi na
ukosefu wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia wanachuo na kukujenga
majengo mapya ya kisasa na ya mfano ili kuweka mazingira bora
yatakayowavutia na kusoma kwa amani na furaha.
Aidha ameagiza vyuo
vyote vya kilimo nchini kutengeneza mazingira ya kibiashara ili vyuo
hivyo viweze kujitegemea kwa kujiendesha kuliko kusubiri ruzuku kama
ilivyo sasa wakati wanazo raslimali ikiwemo maeneo yaliyoachwa wazi bila
kuedelezwa ambayo yamekuwa mapori wakati yangetumika kuanzisha shughuli
za uzalishaji na kuingiza kipato.
Akiwa ziarani Bukoba
ametembelea na kukagua miundombinu na mashamba darasa chuoni hapo na
kujionea maeneo ambayo yako wazi ambayo hayatumiki na kisha alipata
taarifa juu ya Maendeleo ya chuo na mipango ya baadaye kutoka kwa mkuu
wa chuo hicho Mathew Luhembe.
Pia ameongea na
wanachuo na watumishi wa kada mbalimbali chuoni hapo na kusikiliza
changamoto zinazowakabili ambapo aliwapa moyo kuwa zitatafutiwa majibu
ya haraka kwani Serikali ya Rais John Magufuli ipo kwa ajili ya kutoa
fedha kumaliza kero za aina hiyo.
Alisema nia ya Serikali ni kuhakikisha wanajenga mazingira mazuri na rafiki kwa wanachuo na watumishi wote hapa nch
Naye Sophia Christian
ni mfanyakazi wa muda katika chuo hicho amemuomba katibu mkuu
kuwatizama kwa jicho la huruma wafanyakazi wa muda wasio na ajira ya
kudumu kwa kuogezewa kiasi cha malipo yao ya mwezi kwani,wanafanya kazi
kubwa ukilinganisha na kiasi cha sasa wanacholipwa shilingi laki
135,000 na kulipwa kwa wakati ili kupinguza changamoto zinazowakabili za
kifamilia.
Jackobo Marco ni Rais
wa Serikali ya wanachuo hao alitoa shukrani kwa Katibu mkuu kwa
kuwapatia gari ambapo limekuwa mkombozi kwao kwani wakati mwingine
inatokea mgonjwa wa dharula hasa usiku lakini walikuwa inakuwa ngumu
kupata usafiri na sasa hiyo imepungua ambapo,wameomba Serikali kuwaletea
hata nesi katika mazingira yao ya chuo ili wawezekupata huduma ya
kwanza wakati taratibu nyingine za kupata huduma za Afya kunakohusika.
Baada ya Katibu mkuu
Kusaya kusikia hayo amewaeleza kuwa kuanzia wiki ijayo ataleta Kompyuta
za kutosha,pikipiki nne ,kuwaletea nesi kwa ajili ya huduma ya kwanza
kuongeza posho ya mwezi kwa wafanyakazi wa muda toka laki 135 hadi laki
200,000,kujenga bwalo la kulia chakula,kuleta ng’ombe wa kulikia na
power teler na trekta itakayotumika kwa ajili ya kilimo na kujifunzia
pamoja na kutatua changamoto ya mafao ya watumishi na kupandishwa vyeo .
Alisema sasa Serikali
inaompango wa kujenga majengo mapya ya kisasa na mfano ya chuo hicho
hivyo akaahidi wiki ijayo kutuma timu ya wataalam waje wapite maeneo ya
chuo na kutoa ushauri waatumizi bora ya ardhi ni eneo gani lijengwe
majengo mapya ila ninachoomba mkuu wa chuo kuwasiliana na watu wa
mipango miji tupate ramani haraka tuanze taratibu kazi hiyo.
“Baada ya hayo sasa
naagiza vyuo vyetu vya kilimo vipatapatavyo 14 hapa nchini na vituo
vidogo vinne kuandaa utarati b u wa kujiendesha kibiashara kwa kutumia
raslimali walizonazo,tunayo maeneo makubwa lakini yamebaki kuwa mapori
tujenga vitega uchumi,tuanzishe mashamba darasa tukivuna mazao tukauza
tunaongeza pato”aliagiza .
Wakati huo huo
ametembelea Taasisi ya utafiti wa zao la kahawa (TaCRI) -Maruku ambapo
ameagiza kuendelea kuzalisha Miche kinzanima na magonjwa mingi zaidi ya
kahawa na kuwagawia wananchi ili waendelee kulidhika na kuongeza tija
kati kuzalisha zao hilo,pia ametembelea Taasisi ya utafiti wa kilimo
-TARI Maruku ambapo amewataka kuendelea kufanya tafiti zake katika mazao
mbalimbali hari itakayopelekea wananchi kulima kwa ubora na tija.
No comments :
Post a Comment