Monday, August 17, 2020

NHIF YANUFAISHA WATANZANIA MILIONI 4


Waandishi wa Habari wanachama wa DCPC wakiwa katika picha ya pamoja na wawakilishi kutoka NHIF baada ya kufunguliwa mkutano mkuu wa klabu hiyo mwishoni mwa wiki.
Meneja Uhusiano wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Taifa (NHIF), Angela Mziray akizungumzia mbele wa Waandishi wa Habari Wanachama wa Klabu ya Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam (DCPC) wakati wa mkutano mkuu na uchaguzi mkuu wa viongozi.
…………………………………………………
NA SULEIMAN MSUYA
ZIADI ya Watanzania milioni 4.4 wananufaika na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), huku mfuko ukisisitiza wananchi kujiunga kwa wingi.
Hayo yamesemwa na Meneja Uhusiano wa NHIF, Anjela Mziray wakati wa mkutano mkuu na uchaguzi wa viongozi wa Klabu ya Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam (DCPC) uliofanyika mwishoni mwa wiki.
Mziray alisema NHIF ni chombo sahihi kwa usalama wa afya ya Watanzania hivyo anawaomba waandishi kujiunga na kuhamasisha wananchi kujiunga kwa kuandika na kuelezea faida za mfuko huo.
Alisema Watanzania milioni 4.4 bado ni idadi ndogo hivyo wao wanaendelea kutoa elimu kwa jamii kuhusu faida za mfuko huo kwenye maisha yao.
“Hadi sasa zaidi ya Watanzania milioni 4.4 wananufaika na mfuko ila mikakati yetu ni idadi hii iongezeke mara dufu hali ambayo itachochea ustahimilivu wa mfuko.
Ila nisisitize kuwa NHIF ni sawa na kusema msaada tutani kwani imekuwa ikiwaokoa watu wengi wakati wanapokutwa na majanga ya kiafya,” alisema Mziray.
Kwa upande wake Meneja Masoko na Huduma wa NHIF, Hipoliti Lelo alisema mfuko huo umefanyiwa mabadiliko mengi ili uweze kukidhihaja za wanufaika wore ambao wanataka kujiunga wakiwemo waandishi wa habari.
“Tuna mifumo miwili ya kunufaika na NHIF, wapo wanaochangia asilimia 6 ambapo mwajiri anachangia asilimia 3 na mwajiriwa 3. Ila lipo kundi linalochangia kuanzia 50,400, 100,000 hadi zaidi ya milioni 1 wote wananufaika na mfuko na nyie waandishi tumewapa kifurushi maalum cha 100,000 ila mmeshindwa kukichangamkia,” alisema.
Lelo aliwaomba waandishi wa habari kutumia kalamu zao kuandika namna  mfuko huo unavyoweza kumsaidia mtu katika wakati mgumu.
Meneja huyo aliwataka waandishi kote nchini kutumia nafasi hiyo ya upendeleo kwa kujiunga na mfuko huo ili waweze kukabiliana na changamoto za matibabu ambazo wanaweza kukutana nazo.
Alisema fursa hiyo ya waandishi inawahusu wenza wao hivyo wanapaswa kuitumia kikamilifu.
Akizungumzia fursa hiyo Mwandishi Mwandamizi, Salehe Mohammed alisema watahakikisha wanaitumia kikamilifu ili waweze kukabiliana na changamoto za matibabu.

No comments :

Post a Comment