Mkutano Maalum wa 41 wa Baraza la
Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki utafanyika tarehe 4 na 5 Juni
2020 kwa njia ya mtandao (Video Conference). Mkutano utafanyika katika
ukumbi wa mikutano wa Wizara uliopo Mji wa Serikali, Mtumba – Dodoma.
Mkutano huo Maalum wa 41 wa Baraza
la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki, utaanza kwa mkutano wa
ngazi ya wataalam tarehe 4 Juni, 2020 na kufuatiwa na mkutano wa ngazi
ya Makatibu Wakuu tarehe 5 Juni 2020 na kisha kufuatiwa na mkutano wa
Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki siku hiyohiyo
(kuanzia
saa 9:00 alasiri hadi saa 11:00 jioni).
Pamoja na mambo mengine, Mkutano huo utajadili masuala ya fedha na utawala ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.
No comments :
Post a Comment