Katibu Mkuu Wizra ya Mifugo na
Uvuvi Prof. Elisante Ole Gabriel akizungumza kwenye mjadala wa Wadau wa
Tasnia ya Maziwa yaliyokuwa mbashara kwa njia ya video-conference
jijini Dodoma
Msajili wa Bodi ya Maziwa
Dkt.Sophia Mlote,akitoa ufafanuzi jambo kwenye mjadala wa Wadau wa
Tasnia ya Maziwa yaliyokuwa mbashara kwa njia ya video-conference jijini
Dodoma.
Mkurugenzi wa Utafiti,Mafunzo na
Ugani kutoka wizara ya mifugo Dkt.Angello Mwillawa akichagia mada
kwenye mjadala wa Wadau wa Tasnia ya Maziwa yaliyokuwa mbashara kwa
njia ya video-conference jijini Dodoma
Sehemu ya wadau wa maziwa
wakiwa kwenye mjadala wa Wadau wa Tasnia ya Maziwa yaliyokuwa mbashara
kwa njia ya video-conference jijini Dodoma
………………………………………………………………
Na.Alex Sonna, Dodoma
Serikali imepanga kuendelea
kuhamasisha uzalishaji wa maziwa kutoka lita bilioni 3.01 za sasa hadi
kufikia bilioni saba ifikapo 2025.
Kauli hiyo imetolewa na KATIBU
Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, (Sekta ya Mifugo), Prof Elisante Ole
Gabriel amesema kabla ya kuanza mjadala wa Wadau wa Tasnia ya Maziwa
yaliyokuwa mbashara kwa njia ya video-conference.
Aidha Profesa Gabriel amesema kuwa uzalishaji kwa sasa umefikia lita 3.01 mwaka jana
kutoka 2.7 mwaka juzi.
Profesa Gabriel amesema mkakati
huo wa serikali utafanikiwa tu kama wazalishaji na wasindikaji
watashiriki katika kuhamasisha umma, kuzalisha lakini unywaji wa maziwa
utakaoenda sambamba na unywaji.
Katika mjadala huo unaolenga
kukusanya maoni nini kifanyike ili uzalishaji maziwa uongeze tija, wadau
kuhamasisha uzalishaji lakini pia kutafuta masoko ya maziwa
yanayozalishwa.
Pia Wadau wameomba serikali
kuongeza uwigo wa kutoa mikopo kwa wazalishaji kwa wazalishaji na
wasindikizaji ili kuongeza usindikaji maziwa bora nchini.
Kwa upande wake Msajili wa Bodi ya
Maziwa, Dk Sofia Mlote amesema kuwa ili kuhakikisha maziwa
yanayoingia sokoni yanakuwa bora, imekuwa ikikamata shehena ya maziwa
yasiyofuata taratibu hasa Ubungo Dar es Salaam.
Dk. Mlote amesisitiza kuwa Bodi
hiyo imekuwa ikifanya juhudi katika kutekeleza maziwa ambayo hayajafuata
tarataribu pamoja na kuwatoza ffaini wanaoingiza maziwa hayo kutoka
Kibaya, Morogoro na mahali pengine.
Naye Asha Lukaso kutoka Rungwe
amesema kuwa ili kuongeza tija katika uzalishaji wa maziwa lazima
kuangalia upya mfumo wa utoaji mikopo kwa wafugaji kwani imekuwa na riba
kubwa.
Huku Bernard Manyamba kutoka
Tandahima Mtwara ametoa wito kwa serikai kuhamasisha wafugaji kufuga
kisasa ili kuwa na ng’ombe bora wa kutoa maziwa bora.
“Sasa ni wakati wa kuhamasisha
wananchi kujenga viwanda vidogo vigodo kwa ajili ya usingikizaji wa
mazira ambao utaenda sambambana ufugaji wa ngombe wa kisasa”, ameongeza
Alfred Mgolole kutoka Tanga.
Kwa upande wake Restistuta Ndelwa
kutoka Njombe amesema kuwa inatakiwa kutolewa elimu ya ufugaji pamoja
na kuwafanya vijana waingie katika tasnia hiyo ambayo ina faida nyingi
zikiwemo za ajira na tija kwa lengo la kuandaa miundombinuya ufugaji
hasa vitendea kazi.
Innocent Mushi kutoka Kiwanda cha
Maziwa cha Tanga Fresh amesema kuna takiwa kuwa na mkakati wa vituo vya
ukusanyaji maziwa ili wenye viwanda wafike hapo na kuchukua hivyo
maziwa yanayozalishwa yatafika kusindikiwa.
Akizungumza Msajili wa Bodi ya
Maziwa, Dk Sofia Mlote amesema kuwa bodi imekuwa ikifanya juhudi katika
kutekeleza maziwa ambayo hayajafuata tarataribu pamoja na kuwatoza
faini wanaoingiza maziwa hayo kutoka Kibaha, Morogoro na mahali
pengine.
Profesa Ole Gabriel amehitimisha
kwa kusema kuwa katika uhamashishaji jamii kunywa maziwa, utatu wa
wadau yaani serikali, wazalishaji na wasindikaji wanatakiwa kushirikiana
katika kuhamasisha jamii.
“Wadau wanatakiwa kuendele
kuhimiza unywaji wa maziwa hata kama kumekuwa na uongezeko kutoka lita
49 kwa mtu hadi lita 53.9 kwa mwaka 2019/20,”amesisitiza Profesa
Gabriel.
No comments :
Post a Comment