Koplo Brown Twaibu akipokea mkono
wa pongezi ya fedha taslimu milioni moja kutoka Bw. David Raymond
Kigwire Mkuu wa mawasiliano wa Benki ya NBC kwa kuhamasisha jamii juu ya
uvaaji wa barakoa kwa dhumuni la wananchi kujikinga na kuwakinga
wengine dhidi ya maambukizi ya virusi vya Korona, katika hafla ndogo
iliyofanyika katika kituo cha polisi cha Salender Bridge.
RPC wa Ilala Zuberi Chembera
akimkabidhi Koplo Brown Twaibu cheti cha pongezi kwa kazi njema
aliyoifanya ya kuelimisha jamii juu ya uvaaji wa barakoa kwa dhumuni la
wananchi kujikinga na kuwakinga wengine dhidi ya maambukizi ya virusi
vya Korona, katika hafla ndogo iliyofanyika katika kituo cha polisi cha
Salender Bridge.
…………………………………………………………………………………………
Benki ya NBC leo imetambua juhudi
mahususi za Jeshi la Polisi Tanzania na maofisa wake
katika kipindi
chote cha mlipuko wa homa kali inayosababishwa na virusi vya Covid-19
maarufu kama corona. Katika matukio mbali mbali ya kipekee, maofisa kwa
Jeshi la Polisi Tanzania wameonyesha hekima ya hali ya juu na dhamira ya
kuwatumikia, kuwalinda na kuhakikisha Watanzania wanatekeleza maelekezo
ya wataalam ya jinsi ya kupambana na ugonjwa wa corona.
Aidha, benki hiyo ikishirikiana na
Jeshi la Polisi Tanzania pia imemtambua na kumpongeza Koplo Brown
Twaibu Msoke kwa kuielimisha jamii kuhusu umuhimu wa kuvaa barakoa
katika kupambana na gonjwa la corona. Koplo Taibu alijizolea umaarufu
baada ya video ikimuonyesha akiwahimiza abiria kwenye daladala kufuata
maelekezo ya serikali kama kuvaa barakoa, kutosimamisha abiria kwenye
usafiri wa umma na kukaa umbali wa mita moja siyo kwa kujilinda tu bali
kuwalinda na wengine.
Akiongea katika hafla hiyo, Mkuu
wa Mawasiliano wa NBC Nd. David Raymond Kigwile alisema “Kufikia maamuzi
ya kumpongeza Koplo Taibu ilikuwa kitu rahisi kwa benki yetu, hususan
kwa sababu vitendo vyake vya kishujaa vinaendana na msimamo wa benki
yetu katika kupambana na virusi vya Covid-19.” Itambulike kuwa Benki ya
NBC pia imechukua hatua madhubuti kupamba na kuenea kwa virusi hivyo
kama kuwa benki ya kwanza kuweka vitakasa mikono katika ATM zake zote
nchini, utekelezaji wa nafasi ya mita mbili katika matawi yake. Benki ya
NBC pia itaendelea kuwahamasisha na kuwaelimisha wafanyakazi wake na
Watanzania kwa ujumla jinsi ya kumpambana kwa ugonjwa huyo.
Aidha RPC Ilala Nd. Zuberi
Chembera alisema, “Koplo Twaibu ameonyesha mfano mzuri wa kuhamasisha
jamii juu ya uvaaji wa barakoa kwa dhumuni la wananchi kujikinga na
kuwakinga wengine dhidi ya maambukizi ya virusi vya korona. Kitendo
hicho ni mfano wa kuiga na kinahitaji pongezi ya pekee hususan kipindi
hiki ambacho dunia nzima inapambana na janga hili.
Pamoja Benki ya NBC kumtunuku
Koplo Brown Msoke fedha taslim TSHs. 1,000,000 na kumfungulia akaunti
katika benki hiyo, Jeshi la Polisi Tanzania pia limemzawadia Koplo
Twaibu kiasi cha TSHs 200,000 na cheti maalumu kutoka kwa Kamanda wa
Polizi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa.
Katika kuendeleza dhamira ya
kuelimisha jamii matumizi sahihi ya barakoa, Benki ya NBC imezindua
kampeni yake mpya ya #NBCBarakoaChallenge. Pamoja kuhimiza uvaaji wa
barakoa, kampeni ya #NBCBarakoaChallenge itakayoendeshwa kupitia
mitandao ya kijamii ya NBC inaangalia pia kuwakumbusha na kuelimisha
Watananzania juu ya umuhimu wa kuzingatia tabia kinga ili kuzuia
Covid-19.
Jinsi ya kushiriki Barakoa Challenge
- Jipige picha ukiwa umevaa barakoa.
- Post kwenye ukurasa wako wa Instagram ukiwa na hashtag #NBCMaskChallenge.
- Watag watu watatu uwaandikie ujumbe wa kuwakumbusha kuvaa barakoa.
Post yenye likes nyingi zaidi kujishindia simu janja aina ya Samsung A10s kila wiki.
Hakikisha akaunti yako haiko private ili tuweze kuona post yako.
Vigezo namsharti kuzingatiwa
Kuhusu National Bank of Commerce (NBC)
Benki ya Taifa ya Biashara, NBC ni
benki ya zamani kuliko zote nchini Tanzania ikiwa na uzoefu wa zaidi ya
miongo mitano. Tunatoa huduma mbalimbali za kibenki kwa wateja wa
rejareja, biashara, mashirika na misaada ya uwekezaji, bidhaa na huduma
za usimamizi mzuri wa fedha.
Benki hii inaanzia mwaka 1967
ambapo Serikali ya Tanzania ilibinafsisha taasisi zote za fedha,
zikiwamo benki. Mwaka 1991, sheria ya mabenki ilirekebishwa na miaka
sita baadae, yaan mwaka 1997, taasisi iliyojulikana kama Benki ya Taifa
ya biashara, iligawanywa ka;ka tanzu tatu tofau;: NBC Holding
Corpora;on, Na;onal Microfiance Bank (NMB) na NBC (1997) Limited. Mwaka
2000, Benki ya Afrika Kusini, Absa Group Limited, ilipata hisa 55%
kutoka NBC (1997) Limited. Serikali ya Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania
ilipata 30% ya hisa na Shirika la Fedha la Kimataifa (IFC) kama
mwanachama wa Benki ya dunia (World Bank Group), ilipata 15% ya hisa za
benki hii. Taasisi hiyo mpya ikaitwa NBC Limited.
Benki ya NBC ni benki pekee ya
kimataifa inayopa;kana ka;ka maeneo mbalimbali nchini. Ikiwa na matawi 5
na mashine za ATM zaidi ya 230, Benki ya NBC inatoa huduma mbalimbali
za ukusanyaji fedha za huduma nyingine za kibenki kwa wateja mbalimbali.
Benki ya NBC sasa imeajiri wafanyakazi takriban 1,200 nchi nzima.
Kwa maelezo zaidi au msaada tupigie +255 76 898 4000/4011 | +255 22 219 3000 | +255 22 551 1000 or email us NBC_Marke8ngDepartment@nbc.co.tz
No comments :
Post a Comment