Thursday, March 5, 2020

ZAIDI YA WABUNIFU 700 NCHINI WAMEPATA AJIRA ZA MOJA KWA MOJA




 Mkurugenzi Mkazi wa Mfuko wa Maendeleo ya Watu (HDIF) Joseph Manirakiza kulia akizungumza na waandishi wa habari juu ya wiki ya ubunifu itakayoanza Machi 8 hadi 13 mwaka huu jijini Dar es Salaam. Katikati ni Kaimu Kiongozi wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo wa Uingereza (DFID) Natalie Smith na kushoto ni Mkurugenzi wa Tume ya Sayansi na Teknolojia Dr. Amos Nungu.
Mtaalamu wa Mawasiliano kutoka Mfuko wa Maendeleo  ya Watu (HDIF)'Hannah  Mwandoloma akiwakaribisha wadau  wa Maendeleo katika mkutano wa waandishi wa habari kuhusu Wiki ya Ubunifu itakayoanza Machi 8 hadi 13 jijini Dar es Salaam.


 
Kaimu Kiongozi wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo wa Uingereza (DFID) Natalie Smith  katikati akifafanua jambo kwa waandishi wa habari juu ya wiki ya ubunifu itakayoanza Machi 8 hadi 13 mwaka huu jijini Dar es Salaam. Katikati ni  na kushoto ni Mkurugenzi wa Tume ya Sayansi na Teknolojia Dr. Amos Nungu na kulia niMkurugenzi Mkazi wa Mfuko wa Maendeleo ya Watu (HDIF) Joseph Manirakiza.
 Mtaalamu wa Mawasiliano kutoka Mfuko wa Maendeleo  ya Watu (HDIF)'Hannah  Mwandoloma akiwakaribisha wadau  wa Maendeleo katika mkutano wa waandishi wa habari kuhusu Wiki ya Ubunifu itakayoanza Machi 8 hadi 13 jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wanahabari katika mkutano huo

ZAIDI ya wabunifu 700  nchini wamepata ajira za moja kwa moja kutokana na bunifu mbalimbali walizozifanya kwa maendeleo huku wengine 14,000 wakipata ajira za muda.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Darves salaam leo Machi 5, 2020 Mkurugenzi wa Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Dk Amos Nungu amesema serikali kwa kushirikiana na Mfuko wa Maendeleo ya Watu (HDIF) kwa ufadhili na Serikali ya Uingereza wameandaa wiki ya ubunifu ili kuona bunifu mbalimbali zenye kuchagiza maendeleo.
Amesema maonesho hayo ambayo ni ya awamu ya sita kufanyika hapa nchini yatawakutanisha wabunifu na wadau zaidi ya 6000 ambayo yatafanyika katika Mikoa ya  Dar es Salaam, Dodoma, Iringa, Mbeya, Arusha na Zanzibar na yanaenda kwa kauli mbiu ya 'Buni kwa tija'.
Amesema maonesho hayo yataanza Machi 8 mwaka huu lakini yatafunguliwa Machi 9 na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, William Ole Nasha.
"Serikali imekuwa ikihakikisha mfumo wa ubunifu unahusisha wabunifu, wadau wa maendeleo na jamii hivyo, tunajivunia matokeo chanya yanayopatikana kupitia ubunifu kwa kipindi cha zaidi ya miaka saba tokea mwa 2011.
Amesema kwa kuanzia waliwatengeneza wabunifu 110 kwa kupitia atamizi mbalimbali ambapo zaidi ya Sh bilioni 1.9 zilitoewa na kusababisha mtazamo wa sekta nyingi ikiwemo za serikali kutumia ubunifu katika shughuli zao.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkazi wa HDIF, Joseph Manirakiza amesema walianza kuandaa wiki ya ubunifu mwaka 2015 kwa kuangalia sekta za maji, afya, elimu na usafi na kwamba kwa kuanzia hapo wabunifu mbalimbali wamekuwa wakiunganishwa na wadau wa maendeleo kwa ajili ya kuwapatia fedha za kuendeleza bunifu zao.
Ameongeza kuwa,  kutokana na kukua kwa uelewa kuhusu ubunifu watu wengi wameendelea kujitokeza kufanya bunifu kwa malengo ya kutatua changamoto mbali mbali kwenye jamii zikiwemo za kiuchuni na kuongeza ushirikiano baina ya sekta binafsi na serikali.
''Wiki ya Ubunifu ilianza kwa washindi wa masuala ya ubunifu katika sekta hizo kuonesha bunifu zao kwa wadau na baadae kupewa fedha za ujiendeleza lakini baadae tuliamua kuwakutanisha wabunifu na wadau wa maendeleo ili kujadiliana namna ya kuendeleza kazi zao hivyo, tunaendelea kupanua huduma tulianza na Dar es Salaam na sasa tunafikia mikoa sita na malengo ni kufikia mikoa yote nchini,'' alisisitiza Manirakiza.
Naye, Kaimu Kiongozi wa Mfuko wa Maendeleo wa Kimataifa wa Uingereza (DFID) Natalie Smith amesema wiki ya ubunifu ambayo inafanyika kwa mara ya sita sasa imesaidia ukuaji wa sekta hya ubunifu nchini Tanzania kuongeza ukuaji wa maendeleo na ongezeko la wafadhili.
Amesema serikali ya Tanzania pia imeongeza uwekezaji katika sekta ya ubunifu kwa kuandaa mashindano ya Kitaifa ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu (MAKISATU 2020) yatakayofanyika mkoani Dodoma.

Mwaka huu HDIF CISTECH imeandaa wiki hiyo ya ubunifu kwa kushirikina na wadau mbali mbali wakiwemo  UNDP, UNICEF,  UN,  WOMEN, UNCDF CLOUDS MEDIA, SEGAL FAMILY FOUNDATION, EXIM BANK na Ubalozi wa  Netherland.

No comments :

Post a Comment