Naibu Waziri wa Ujenzi, Mawasilino
na Uchukuzi, Elias Kwandikwa (kushoto) Afisa Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa
Mawasiliano kwa wote (UCSAF), Justina Mashiba (katikati) na Mkurugenzi
Mtendaji wa Kampuni ya Vodacom Tanzania PLC, Hisham Hendi (kulia)
wakibonyeza kitufe cha kompyuta kuashiria uzinduzi rasmi wa awamu ya
pili ya mradi wa kuunganisha shule na mtandao wa intaneti ambapo kampuni
ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania imetoa kompyuta 806, router 163
zilizounganishwa na intaneti kwa mwaka mzima.
Naibu Waziri wa Mawasilino na
Uchukuzi ,Elias Kwandikwa (kushoto)akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji
wa Kampuni ya Vodacom Tanzania ,Hisham Hendi (kulia) wakati
walipokutana kwenye ufunguzi wa mradi wa kuunganisha shule 163 kwenye
mtandao wa intaneti kwa shule hizo, Hii ni kutokana kujihami na virusi
vya homa ya corona
Naibu Waziri wa Ujenzi,
Mawasiliano na Uchukuzi, Elias Kwandikwa (kushoto) akiwakabidhi kompyuta
Walimu Festo Kagoma (kulia) na Adelaida Pangani kutoka shule ya
sekondari Maze iliyoko Mpwapwa Mkoani Dodoma ikiwa ni sehemu ya msaada
wa kompyuta 806 kutoka kampuni ya simu za Mkononi ya Vodacom Tanzania
PLC, katikati ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo Hisham Hendi.
Makabidhiano hayo yalifanyika Jijini Dodoma kwenye uzinduzi wa awamu
ya pili ya mradi wa kuunganisha shule 163 nchini kwenye mtandao wa
Intaneti
……………………………………………………………………………………………….
- Zaidi ya wanafunzi 81,500 kufaidika na matumizi ya kompyuta zilizounganishwa na mtandao wa intaneti bure
Dodoma.
Kampuni ya simu za mkononi kupitia
taasisi yake ya Vodacom Tanzania Foundation kwa kushirikiana na Mfuko
wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) wameazimia kuhakikisha wanawasaidia
wanafunzi nchini kujisomea kidijitali.
Ushirikiano huu utawafaidisha
zaidi ya wanafunzi 81,500 kutoka shule za msingi na sekondari 163
zilizoko maeneo mbalimbali nchini ambao wamekabidhiwa kompyuta 806,
vipanga njia (router 163) ambavyo vimeunganishwa na muda wa maongezi kwa
muda wa mwaka mmoja, vyote vikiwa na jumla ya TSh390, 274,905.
Wakati huo huo zaidi ya wanafunzi
2,500 katika shule za sekondari za Chikola, Membe, Intela, Mumi na Mazae
mkoani Dodoma watafaidika na matumizi ya kompyuta hizo kufuatia shule
hizo kupewa msaada wa kompyuta, routers na printer katika mradi huu.
Mwaka jana, Vodacom ilishirikiana
na UCSAF kutoa elimu ya kidijitali shuleni nchini kwa kuzingatia upana
wa miundombinu ya mtandao wake. Hadi kufikia mwisho wa mradi huu zaidi
ya wanafunzi 81,500 katika shule 163 watafaidika na msaada wa kompyuta
na kuunganishwa na huduma ya intaneti bure.
Akizungumza wakati wa hafla ya
makabidhiano Jijini Dodoma, Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na
Mawasiliano, Mheshimiwa Elias Kwandikwa, alisema mahitaji ya elimu bora
kwa kutumia teknolojia ya kisasa hayaepukiki ikiwa taifa lina dhamira ya
kuandaa vijana kwa ajili ya mfumo wa sasa wa kidijitali.
“Serikali kupitia mfuko wa
mawasiliano kwa wote, umeleta TEHAMA, na sasa kampuni ya Simu za mkononi
ya Vodacom Tanzania wanaziunganisha shule hizo na mtandao wa intaneti
ambapo Walimu na Wanafunzi watapata nafasi ya kutafuta materials za
kujifunzia” alisema Mh Kwandikwa.
Naibu Waziri aliongeza kwamba kwa
sababu Vodacom wana portal iliyo chini ya mradi wa Instant Schools
unaoitwa Instant School, aliwaomba Waalimu kuwapa nafasi wanafunzi ili
wajifunze Zaidi kupitia vifaa hivyo.
“Sisi tumetoa baadhi ya vifaa, na
tunawashukuru Vodacom Tanzania PLC kwa msaada huu utakaowawezesha walimu
na wanafunzi kufundisha, kusoma na kuongeza uwezekano wa kupata taarifa
mbalimbali.” Aliongeza Naibu Waziri.
Kwa upande wake, Mkurugenzi
Mtendaji wa Vodacom Tanzania PLC Hisham Hendi, alisema msaada huo ni
sehemu ya ajenda ya Vodacom kukuza elimu kupitia mfumo wa kidijitali
hasa kwa sehemu za vijijini nchini..
“Vodacom Tanzania PLC tunaamini
kwamba, katika wakati ujao teknolojia itakuwa kiungo muhimu katika
kuunganisha fursa kwa kila mmoja ili kufikia mahitaji muhimu, sekta ya
elimu ni mahala pa kuanzia. Tuna furaha kushirikiana na serikali ili
kuhakikisha kwamba watu wengi wanashiriki katika mfumo wa sasa wa
kidijitali. Pamoja na router hizi tulizotoa, ili kuhakikisha kwamba
hawakosi intaneti, tumeamua kuwaunganisha na kifurushi cha mwaka mzima
kwa kila shule, ili wajisomee bila tatizo lolote,” Hendi alisema
Halikadhalika kompyuta hizi
zitawawezesha walimu na wanafunzi kutumia mfumo wa Portal kupitia mradi
wa Instant School ambao pia unasimamiwa na Vodacom Tanzania Foundation
kwa ajili ya kupata zana mbalimbali za kielimu bure kwa kutumia simu ya
mkononi na kompyuta, hivyo kuchochea usomaji kidijitali.
“Hadi sasa mfumo wetu wa Instant
School umetembelewa na wageni wapatao 65,916 ambapo wote wamejionea
faida kwa kusoma kidijitali,” aliongeza Hendi.
“Ushirikiano huu unakwenda
sambamba na mkakati wa kampuni wa kutoa rasilimali ili kusaidia
upatikanaji wa maendeleo katika sekta ya elimu,” Hendi aliongezea
kusema.
Afisa Mtendaji Mkuu wa UCSAF,
Justina Mashiba alisema, “Tunashukuru kwa ushirikiano huu na Vodacom
kuhakikisha mpango wetu unafanikiwa kwa kuunganisha shule za umma na
upatikanaji intaneti ili kutumia vifaa vya ICT kikamilifu. Mchango huu
unasaidia mpango wetu wa kuhakikisha huduma za mawasiliano zinapatikana
kila mahali haswa katika maeneo ya vijijini,”
Tukio la leo ni mwanzo wa awamu ya
pili ya utoaji wa msaada wa kompyuta kwa shule za umma Tanzania Bara na
Zanzibar chini ya ushirikiano wa Vodacom Tanzania Foundation na UCSAF.
Kupitia awamu ya kwanza ya mradi
huu, Vodacom Tanzania PLC ilitoa kompyuta 48 kwa shule 24, hii
iliwafaidisha wanafunzi Zaidi ya 15,000 nchini.
Mkurugenzi Hendi ametoa wito kwa
wadau wengine kushirikiana na Vodacom Tanzania PLC ili kuhakikisha
kwamba miundombinu ya kampuni hiyo inatumika kwa faida Watanzania wote.
Kwa upande mwingine, Hendi
ameiomba serikali kuweka kidijitali mitaala iliyopitishwa na taasisi
husika ili kuweza kutumika na watu wa rika zote wakiwemo wanafunzi ambao
ndio wahitaji zaidi.
Ends
Kuhusu Vodacom Tanzania Foundation:
Vodacom Tanzania Foundation ni
sehemu ya shughuli za kijamiii ya kampuni ya Vodacom Tanzania PLC
ambayo ina simamia utoaji wa huduma kwa watu wenye uhitaji hususani kwa
wanawake na vijana. Mfuko huu umejumuisha misaada ya hisani na ina
tumia teknolojia ya simu za mkononi kutatua matatizo ya kijamii.
Katika kufanya kazi na mashirika
yasio ya kiserikali na washirika, Vodacom Tanzania Foundation imeweza
kusaidia miradi 120 mpaka sasa na imewekeza zaidi ya shilingi bilioni 15
kuboresha maisha ya watanzania.
No comments :
Post a Comment