Katibu wa Jumuia ya
Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT-Taifa) Queen Mlozi akizungumza na
waandishi wa habari jijini Dodoma kuelekea siku ya maadhimisho ya
wanawake Dunia ambayo hufanyika kitaifa Machi 8 kila mwaka na
yanatarajia kufanyika kitaifa mkoani Simiyu.
……………………………………………………………………………………………
Na.Alex Sonna,Dodoma
Katibu wa Jumuia ya
Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT-Taifa) Queen Mlozi amemuomba
Rais,Dk.John Magufuli kuendelea kuwapa
Wanawake nafasi za uongozi
kutokana na waliopo kufanya vizuri kwenye awamu yake ya tano.
Bi.Mlozi ametoa ombi
hilo leo jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari
kuelekea siku ya maadhimisho ya wanawake Dunia ambayo hufanyika kitaifa
Machi 8 kila mwaka na yanatarajia kufanyika kitaifa mkoani Simiyu.
Aidha Bi.Mlozi amesema
kuwa katika Awamu ya Tano nchi imeweka historia ya pekee kwa kumteua
Makamu wa Rais, mwanamke Samia Suluhu Hassan, Naibu Spika ,Dk.Tulia
Ackson, mawaziri, manaibu na ngazi nyingine mbalimbali.
Bi.Mlozi amesisitiza
kuwa wanawake ambao walipewa nafasi mbalimbali za uongozi
hawajamuangusja Rais kwenye kazi wamekuwa wakifanya vizuri katika
utekelezaji wa majukumu yao.
“Kiukweli kabisa
tunampongeza Rais wetu Dkt.Magufuli kwa kuandika historia ya kuwateuwa
wanawake katika uongozi mbalimbali hivyo tunamuomba endelee kuwateua
kwenye nafasi nyingi ili hatimaye tuweze kufikia katika asilimia 50% kwa
50%”amesema Mlozi
Hata hivyo amesema kuwa
wanawake wanatakiwa kujiamini,wenye ujasiri,wenyer busara na kuweza
kujiona kuwa wanathaminiwa na kuacha kuwa wanyonge kwani kinachotakiwa
hapo ni usawa kati ya mwanamke na mwanaume.
Aidha amesema kuwa kipindi hiki
nchi inaelekea kwenye uchaguzi hivyo wananchi wanatakiwa kuwa makini na
kuwachagua viongozi wenye ueledi na uwezo wa kutafsiri Ilani ya CCM.
Bi.Mlozi amewataka
wanawake kumpigia kura za kishindo rais na viongozi wengine
watakaojitojeza kuchukua fomu kwa ajili ya kugombea nafasi mbalimbali
hususani wanawake ili waweze kushinda katika nafasi hizo.
“Wanawake ni kioo Cha
Jamii na kielelezo hata katika familia au kwenye maendeleo hivyo lazima
wawe kifua mbele Kupambana na udhalimu, ukatili na unyanyasaji wa
kijinsia wa aina yeyote ile,”amesisitiza Bi.Mlozi
No comments :
Post a Comment