Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey
Mwanri akiongoza majadiliano wakati wa kongamano la vijana kujadili
fursa za kilimo mifugo na uvuvi kwa mikoa ya Tabora,Singida,Dodoma na
Kigoma katika ukumbi wa Mtemi Isike Mwanakiyungi leo mjini Tabora.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey
Mwanri akiwa na vijana wakisoma maazimio ya mkoa kuhusu upandaji miti
mara baada ya kupanda miti ya kumbukumbu akihimiza vijana kupanda miti
naili kutunza mazingira na kupata ajira
Kijana Raphael Malongo( kushoto)
toka mkoani Singida akitoa ushuhuda wa mafanikio aliyoyapata baada ya
mafunzo kwa vitendo toka nchini Benin yaliyomwezesha kuanzisha kilimo
biashara na kuajili vijana wenzie Singida.Kulia ni Mwezeshaji wa
kongamano Joseph Massimba wa SUGECO Morogoro.
Mkuu wa
Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri akiwa na vijana mara baada ya kumaliza
zoezi la upandaji miti ikiwa ni uhamasishaji kilimo cha miti na
kuzalisha ajira kwa vijana wa mikoa ya Tabora,Singida,Dodoma na Kigoma
(Habari na picha WK)
………………………………………………………………………………………………..
Tabora
Vijana wameiomba serikali ianzishe
vijiji maalum kwa ajili ya shughuli za kilimo, mifugo na uvuvi endelevu
ili kuongeza upatikanji wa malighafi za viwanda nchini.
Kauli hiyo imetolewa leo Mjini
Tabora na Mwenyekiti wa Wajasiliamali Vijana mkoa wa
Tabora Mfaume Juma
Mfaume kwenye kongamano la vijana katika kilimo na kuongeza kuwa uwepo
wa eneo maalum la kilimo kwa vijana kutasaidia vijana kuwa na uhakika
wa ardhi
“Sisi vijana wa Tabora tunaomba
tupatiwe mashamba ekari angalau kumi kwa ajili ya kuzalisha ili tuwe na
kijiji cha wajasiliamali wazalishaji mazao ya kilimo na uvuvi ili
kuondoa tatizo la ardhi “ alisema Mfaume
Aliongeza kusema kuwa vijana wengi
wanashindwa kufanya kazi za kilimo kwa kuwa halmashauri nyingi
hazitenga mashamba na maeneo ya ufugaji kibiashara na tatizo la ukosefu
wa mitaji na elimu ya ujasiliamali
Mfaume alitumia fursa ya kongamno
hilo kupongeza jitihada za Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri za
kuwafundisha vijana kuacha kukaa vijiweni na sasa wamehamasika kujiunga
katika vikundi vya upandaji miti na kilimo kama sehemu ya ajira.
“Tabora yetu imebadilika tangu
Mkuu huyu wa Mkoa afike,vijana tulianza kwa shida lakini alitutia moyo
sasa tumefanikiwa kukopeshwa trekta mbili kwa ajili ya kilimo “ alisema
Mfaume
Kwa upande wake,Imanuel Sotta wa
shirika la Compassion Tabora ameipongeza serikali kwa utashi na maono
yake ya kuwezesha vijana kupitia mikopo ya uwezeshaji vijana kiuchumi
toka mapato ya ndani ya halmshauri.
Kijana John Kipingu toka Nzega
ameeleza kuwa anaiomba serikali iwasimamie maafisa ugani kuweza
kuwafundisha vijana kutumia rasilimali maji kulima kilimo cha bustani na
mboga mboga kwani zinahitajika sana sokoni.
Nae Beatrice Bilanda toka wilaya
ya Kibondo mkoa wa Kigoma alisema vijana wanahitaji taarifa za fursa ya
kilimo mapema ili ziwasaidie kufanya mabadiliko na ushiriki katika
kilimo utaongezeka.
“ Kilimo cha mazao kwa kutumia
jembe la mkono na bei ya kubwa ya pembejeo na mbegu zinaendelea kuwa
changamoto kwa vijana walio katika kilimo na ufugaji” alisema Beatrice
na kuiomba serikali kutoa mikopo ya pembejeo kwa vijana.
Naye Raphael Malongo toka Singida
amewashauri vijana wenzake kujisomea vitabu na kutumia mitandao ya
kijamii kupata elimu na mafunzo yatakayo saidia kuongeza tija katika
uzalishaji mazao ya kilimo na mifugo na kutatua changamoto za soko na
visumbufu vya mazao
“ Naishukuru Wizara ya Kilimo na
FAO kwa kunifadhili kwenda masomoni nchini Benin kujifunza kwa vitendo
shughuli za kilimo hata sasa nimeweza kuanzisha kilimo biashara Singida
na kuajili vijana wenzagu kupitia kampuni ya Malongo Poulty Farm
kufugaji nyuki kisasa” alisema Malongo
Malongo amesema kwa sasa
amefanikiwa kutengeneza mtambo wa kuzalisha nishati ya bio gesi baada ya
kufuga ng’ombe mmoja tu anawezesha kupata samadi anayotumia kuzalisha
mazao ya bustani na chakula,hivyo vijana wajitokeze kutumia fursa za
kilimo kwa kushiriki kwenye makongamano na mafunzo
Akijibu hoja za vijana ,Mkuu wa
Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri amewataka vijana kutumia ardhi nzuri
iliyopo nchini na uwepo wa wataalam wa kilimo na mifugo kujiunga katika
vikundi vya ushirika ili wapate nguvu ya kuanzisha kazi za kilimo na
kufikiwa na fursa za mitaji na utaalam
Mwanri amewashauri vijana nchini
kujituma na kubadili fikra kuwa kilimo na ufugaji ni ajira ya uhakika
kutokana na mahitaji makubwa ya bidhaa na malighafi za viwandani
kuongezeka.
“ Leo vijana mmekutana hapa
serikali inataka kuwajengea matumaini mapya ili mbadilike na kutumia
fursa za kilimo,mifugo na uvuvi kuongeza uchumi wenu na kuzalisha ajira “
alisema Mwanri
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya
Kaliua Abel Busalama amewataka vijana kujiamanini kuwa sekta ya kilimo
ni chaguo sahihi kwa wakati huu ambapo serikali inajielekeza kuhamasisha
vijana kujiajili
Busalala aliongeza kuwa fahamisha
vijana kuwa uchumi wan chi unategemea kilimo ndio maana jitihada kubwa
kupitia halmashauri zinafanyika kwa kutenga maeneo kwa vijana
wanaojitokeza kama ilivyo kwa halmashauri ya wilaya ya Kaliua.
Kongamano la vijana katika kilimo
limefanyika katika ukumbi wa Mtemi Isike Mwanakiyungi mjini Tabora na
kuhusisha vijana zaidi ya 340 toka mikoa ya Tabora ,Singida,Dodoma na
Kogoma chini ya uenyekiti wa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri
No comments :
Post a Comment