Monday, March 9, 2020

UJUMBE KUTOKA BURUNDI WATEMBELEA TAASISI YA SARATANI YA OCEN ROAD KUJIFUNZA UENDESHAJI TAASISI YA SARATANI



Ujumbe kutoka Burundi wakiwa kwenye majadiliano wakti walipotembelea chumba cha tiba ya mionzi ya 3D kinachotumia mashine za Linac. Ugeni huo upo nchini ukijifunza katika taasisi ya Saratani ya Ocean road
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road(ORCI) Dk. Julius Mwaiselage akizungumza uwepo wa ugeni kutoka Burundi kuja kujifunza utendaji wa taaisisi juu ya kutibu magonjwa ya Saratani
Moja ya mashine ys LINAC ambayoa inatibu magonjwa ya saratani kibingwa ikiwa katika muonekano tofautitofauti
Ujumbe huo wa kutoka Burundi wakijadiliana jambo wakati wa ziara ya kutembelea vitengo ndani ya Taasisi hiyo ya Ocean Road.
Ujumbe kutoka Burundi wakiwa kwenye majadiliano wakti walipotembelea chumba cha tiba ya mionzi ya 3D kinachotumia mashine za Linac. Ugeni huo upo nchini ukijifunza katika taasisi ya Saratani ya Ocean road
Daktari Bingwa wa magonjwa ya Saratani wa ORCI, Dk. Nanzoke Mvungi akitoa maelezo kwa ugeni kutoka Burundi ambao wapo hapa nchini kujifunza
……………………………………………
UJUMBE wa wataalam wa watu watano wakiwemo Madaktari na maafisa kutoka Wizara ya Afya ya Burundi upo nchini  kwa ziara maalum ya siku tano kujifunza mambo mbalimbali ya
utendaji na uendeshaji unaofanywa na  Taasisi ya Saratani ya Ocean Road (ORCI) ikiwemo namna inavyotoa huduma zake  za matibabu kwa wagonjwa wa Saratani kwa ubora Ukanda wa Afrika Mashariki.
Ugeni  huo pia utapata nafasi ya kujifunza kwa nadharia na vitendo ambapo watazunguka katika kujionea jinsi huduma zinavyotolewa na namna wanavyoendesha matibabu ikiwemo kutumia mitambo ya kisasa inayotumia miale ya mionzi  mashine ya Linac Accelerator ambayo inapatikana Tanzania pekee kwa Ukanda huu wa Afrika Mashariki.
Awali akizungumza na waandishi wa Habari, Mkurugenzi Mtendaji wa ORCI, Dk. Julius Mwaiselage amesema wameupokea ujumbe huo kutoka Burundi  ambapo utakuwa Nchini kwa siku tano na kujifunza  ili kupata uzoefu ambapo nao wakiwa mbioni kuanzisha huduma kama hizo nchini mwao.
‘ORCI  tuna ujumbe kutoka Burundi umekuja hapa Tanzania, kuangalia na kujifunza maendeleo  katika hutoaji wa huduma za saratani hapa nchini.
Kama inavyofahamika ukanda huu wa Afrika hususani Tanzania, ORCI imepiga hatua kubwa sana katika utoaji wa huduma za saratani kwa wananchi wake hivyo Shirika la kimataifa la nguvu za atomic – IAEA  limeona ni busara sana kwa zile nchi ambazo zinataka kuanzisha huduma zake za saratani, zifike Tanzania hapa kwetu ili kujifunza mambo mbalimbali ambayo yamefanyika kwa weredi na kwa upana mkubwa sana.
‘Tumepata hii timu ya kutoka Burundi ambao tutakuwa nao hapa kwa siku tano na kujaribu kuonyesha na kuwaelezea tulivyofanya kwa kupitia  uboreshaji wa huduma  kutibu saratani kwenye vituo, uboreshaji wa tiba  ya kutibu kwenye Kanda, na uboreshaji wa Ocean road kupitia kununua mashine mpya.
Pia uboreshaji wa tiba kemia, upatikanaji wa dawa pamoja na mafunzo kwa watumishi  wa Afya katika utoaji wa huduma ya saratani.’ Alisema Dk. Mwaiselage.
Dk. Mwaiselage ameipongeza Serikali ya awamu ya tano kwa kuwezesha taasisi hiyo kiasi kwa sasa imekuwa kimbilio kwa nchi nyingi ambazo zinataka kuja kujifunza namna ya tiba ya Saratani.
‘ORCI  tunaipongeza na tunashukuru kwa msaada mkubwa kutoka Serikali, na hasa serikali hii ya awamu ya tano inayoongozwa na  Dk. John Pombe Joseph Magufuli wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa kipindi hiki cha miaka minne taasisi imekuwa mbele sana katika hutoaji wa huduma na nchi nyingi imeona Tanzania tukipiga hatua kwenye kutibu saratani ikiwemo kununua mashine hizi mionzi za kisasa za LINAC   ambazo zinapatikana katika nchi chache sana za Afrika huku zikipatikana nchi chache za Ulaya, India na Marekani.’ Alisema Dk. Mwaiselage.
Dk. Mwaiselaga amesema wamejitahidi katika upatikanaji wa dawa za saratani ambazo zinapatikana kwa kiwango kikubwa sana na wagonjwa wanatibiwa vizuri.
‘Utaratibu wa Tanzania wa kununua dawa ni mzuri sana tunatumia Bohari kuu ya Dawa ‘MSD’ ambapo Serikali inatoa fedha zinaenda huko na MSD wananunua dawa kiwandani nah ii inafanya upatikanaji wa dawa na tiba kuwa mzuri na wagonjwa wengi ikiwemo nje wanafika hapa kupata hduuma hii ambapo pia tumeboresha huduma zaidi. Lengo  ni kuona watanzania wote wanapata huduma hapahapa bila kwenda nje ya nje ya Nchi’ alieleza Dk. Mwaiselage.
Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Saratani Nchini Burundi,  ambaye alionge kwa niaba ya  ujumbe huo, Dk. Jonas Nsegiyumva alieleza kuwa,  Burundi inaendelea kuona namna ya kuzuia ugonjwa huo wa saratani ikiwemo kuwapatia tiba wananchi wake ambapo ujio wao hapa nchini utakuwa chachu ya kwa Taifa lao.
‘Tumeshukuru kuja hapa Taasisi ya Ocean Road kujifunza dhidi matibabu ya Saratani,  tumeona Madaktari ni wengi tena ambao wanauwezo ambao wanaweza kutibu watu. Pia wana wagonjwa wengi wakiwa wanatibiwa vizuri sana.
Kwa sasa hivi nchini kwetu  ndio tumeanzisha Taasisi yetu ijulikanayo kama  Taasisi ya Saratani Bujumbura  na mwaka mmoja ama miwili tunaweza kusema ni idadi ya wagonjwa wangapi wa saratani . Kwa Burundi saratani zinazosumbua kwa sasa ni saratani za kike, saratani ya utumbo na zingine  nyingi.’ Alisema  Dk. Nsegiyumva.
Aidha, ORCI imeeleza kuwa kwa sasa wanatarajia kuendelea kupokea ugeni mwingine kama huo kutoka nchi mbalimbali zikiwemo za Liberia na Lethoto  ambazo zitafika nchini kujifunza juu ya utoaji na tia ya Saratani.

No comments :

Post a Comment