Monday, March 9, 2020

HAIWEZEKANI MWANANCHI WA KIJIJINI ANUNUE MAJI UNIT 1 KWA TSH 5,000,MJINI TSH.1800-NAIBU WAZIRI AWESO



NAIBU Waziri wa Maji, Jumaa Aweso,akizungumza na washiriki  wakati akifungua mkutano wa mrejesho wa uhakiki na tathmini ya utekelezaji wa mpango wa malipo kwa matokeo awamu ya nne(PBR) inayotekelezwa kwa ufadhili wa Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza(DFID), uliofanyika jijini Dodoma.
Baadhi ya washiriki kutoka sehemu mbalimbali wakifatilia hotuba ya Naibu  Waziri wa Maji, Jumaa Aweso,wakati akifungua mkutano wa mrejesho wa uhakiki na tathmini ya utekelezaji wa mpango wa malipo kwa matokeo awamu ya nne(PBR) inayotekelezwa kwa ufadhili wa Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza(DFID), uliofanyika jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Maji Prof. Kitila Mkumbo,akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa mrejesho wa uhakiki na tathmini ya utekelezaji wa mpango wa malipo kwa matokeo awamu ya nne(PBR) inayotekelezwa kwa ufadhili wa Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza(DFID), uliofanyika jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu wa wizara ya Maji,Mhandisi Anthony Sanga,akitoa taarifa wakati wa ufunguzi  wa mkutano wa mrejesho wa uhakiki na tathmini ya utekelezaji wa mpango wa malipo kwa matokeo awamu ya nne(PBR) inayotekelezwa kwa ufadhili wa Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza(DFID), uliofanyika jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (Ruwasa), Mhandisi Clement Kivegalo,akitoa tathmini  wakati wa ufunguzi  wa mkutano wa mrejesho wa uhakiki na tathmini ya utekelezaji wa mpango wa malipo kwa matokeo awamu ya nne(PBR) inayotekelezwa kwa ufadhili wa Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza(DFID), uliofanyika jijini Dodoma.
Mwakilishi wa Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza(DFID), Getrude Kihunrwa,akizungumza wakati wa ufunguzi  wa mkutano wa mrejesho wa uhakiki na tathmini ya utekelezaji wa mpango wa malipo kwa matokeo awamu ya nne(PBR) inayotekelezwa kwa ufadhili wa Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza(DFID), uliofanyika jijini Dodoma.
NAIBU Waziri wa Maji, Jumaa Aweso,akiwa katika picha ya pamoja na washiriki kutoka sehemu mbalimbali mara baada ya kufungua mkutano wa mrejesho wa uhakiki na tathmini ya utekelezaji wa mpango wa malipo kwa matokeo awamu ya nne(PBR) inayotekelezwa kwa ufadhili wa Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza(DFID), uliofanyika jijini Dodoma.
……………………………………………………………………………………………………
Na.Alex Sonna,Dodoma
Naibu Waziri wa Maji Jumaa Aweso amezitaka mamlaka za Maji kufanya uwiano ulio
sawa wa  Ulipaji wa gharama za maji kati ya Maeneo ya mjini na vijijini .
Kauli hiyo ameitoa leo jijini Dodoma wakati akifungua mkutano wa mrejesho wa uhakiki na tathmini ya utekelezaji wa mpango wa malipo kwa matokeo awamu ya nne(PBR) inayotekelezwa kwa ufadhili wa Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza(DFID).
Ukiangalia maji yanayotumika DSM,Maji yanayotumika Mwanza na Maeneo mengine mjini kwa maana ,maeneo ya vijijini wananchi wanatumia maji kwa gharama kubwa sana ,mfano Unit 1 ya Maji DSM inanunuliwa kwa Tsh.1800 lakini ukienda vijijini  unit 1 mwananchi ananunua mpaka Tsh.5,000 ,hili jambo  si sahihi  na Unit 1 sawa nan doo hamsini ,hivyo mamlaka mnaohusika na huduma ya usambazaji wa maji mnatakiwa mliangalie sana”.amesisitiza Mhe.Aweso
“Nikuombe sana Mkurugenzi wa Ruwasa jukumu letu ni kuhakikisha mwananchi wa mijini na vijijini wanapata huduma nafuu, lazima tuangalie namna ya kumpa mwananchi unafuu, vijijini wananunua maji kwa gharama kubwa,”amesema Mhe.Aweso
Aidha amesema kuwa  maeneo yaliyo kuwa na miradi ya maji  kichefuchefu likiwemo eneo la Mwakitolyo Mkoani Shinyanga  sasa tayari serikali ilishachukua hatua ya kumfukuza mkandarasi na kinachofanyika ni kuwatumia wataalam wa ndani ili huduma ya maji ipatikane kwa wananchi.
 Katibu Mkuu wizara ya Maji,Prof.Kitila Mkumbo amesema Serikali pamoja na Wadau wameshatekeleza miradi ya Maji 1423  tangu mwaka 2015 hadi sasa ,kati ya hiyo  miradi 792 ilishakamilika mpaka kufikia  mwezi Disemba  Mwaka jana na serikali inaendelea na utekelezaji wa miradi 631.
Kwa upande wake Naye, Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Mhandisi Anthony Sanga amesema kuwa  kuna kero kubwa ya maji vijijini hivyo bila kuwa na takwimu kwenye utendaji kazi watakwama.
Awali, Mkurugenzi wa Ruwasa, Mhandisi Clement Kivegalo, amesema kuwa katika awamu hiyo ya nne ya mpango huo ambayo inatekelezwa na Ruwasa, Halmashauri 181 zilifuzu ambapo Sh.Bilioni 63.46 zimetolewa.
“Hii ni sawa na ongezeko la takribani asilimia 110 ni zaidi ya mara mbili ya kiasi kilichotolewa katika awamu ya tatu, hata hivyo bado kuna maeneo ambayo tathmini inaonesha kuwa baadhi ya halmashauri hazikufanya vizuri katika vigezo vinavyotajwa,”amesema Sanga
Naye, Mwakilishi wa Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza(DFID), Getrude Kihunrwa , amesema kwasasa hali ya utekelezaji wa miradi unakwenda vizuri kwani hapo mwanzo walitamani hata kuachana na kutekeleza mradi huo lakini kwa Sasa hali ni safi na wataendelea kushirikiana na serikali katika kutekeleza miradi hiyo.
“Hali ya utekelezaji wa Mradi huu kwa Sasa unaridhisha kwa mwanzo hali haikuwa shwari, kabisa, lakini kwa Sasa mambo yanakwenda sawa, mfano ni Wilaya ya Gairo ambayo ilikuwa ikifanya vibaya, lakini leo ni moja ya Wilaya zilizopokea zawadi kwa kufanya vizuri” amesema Bi Getrude.

No comments :

Post a Comment