Monday, March 9, 2020

TMA YAPEWA RUKSA KUTOZA WAHITAJI TAKWIMU ZA HALI YA HEWA ZA USANIFU MIRADI



Meneja wa mafunzo wa Wakala ya Mafunzo kwa Njia ya Mtandao (TaGLA) Brown Hasunga,akitoa taarifa ya awali wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya menejimenti ya TMA yaliyofanyika leo jijini Dodoma (katikati) Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi Dk Leonard Chamuriho na kushoto ni Mkurugenzi wa TMA Dk  Agnes Kijazi
Mkurugenzi wa TMA Dk  Agnes Kijazi,akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya TMA yenye lengo la  udhibiti na ukusanyaji wa mapato ya huduma zinazotolewa na mamlaka hiyo yaliyofanyika leo jijini Dodoma kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi Dk Leonard Chamuriho ambaye alikuwa mgeni rasmi.
Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi Dk Leonard Chamuriho,akizungumza na washiriki wakati akifungua  mafunzo ya TMA yenye lengo la  udhibiti na ukusanyaji wa mapato ya huduma zinazotolewa na mamlaka hiyo yaliyofanyika leo jijini Dodoma kushoto kwake ni Mkurugenzi wa TMA Dk  Agnes Kijazi.
Sehemu ya washiriki wakifatilia hotuba ya Mkuu Wizara ya Uchukuzi Dk Leonard Chamuriho,wakati wa ufunguzi  mafunzo ya TMA yenye lengo la  udhibiti na ukusanyaji wa mapato ya huduma zinazotolewa na mamlaka hiyo yaliyofanyika leo jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi Dk Leonard Chamuriho akiwa kwenye picha ya pamoja na  na washiriki mara baada ya kufungua  mafunzo ya TMA yenye lengo la  udhibiti na ukusanyaji wa mapato ya huduma zinazotolewa na mamlaka hiyo yaliyofanyika leo jijini Dodoma.
…………………………………………………………………………………………….
Na.Alex Sonna,Dodoma
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imepewa ruhusa ya kuwatoza fedha wahitaji 
takwimu za hali ya hewa za usanifu miradi mbalimbali  ikiwemo wa majengo  ili kufanya kazi ya usanifu.
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dodoma na Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi Dk Leonard Chamuriho wakati akifungua mafunzo ya menejimenti ya TMA yenye lengo la udhibiti na ukusanyaji wa mapato ya huduma zinazotolewa na mamlaka hiyo.
Dk.Chamuriho amesema TMA imelega kukusanya mapato katika huduma inazozitoa ni vyema wasanifu hao wakaweza  kutozwa fedha hizo ili kurudisha gharama zilizotumika wakati wa kuandaa takwimu hizo.
“Mkumbuke kuwa hapa mnaongea na Mhandisi wa ujenzi hivyo kwenye kazi zetu za usanifu huwa tunakuja kwenu kuhitaji takwimu kutoka hali ya hewa mfano kwa sasa tunasanifu majengo marefu tunahitaji kujua nguvu ya upepo kwa kila urefu unapokwenda hivyo sio dhambi na ninyi mkitoza hizo takwimu kwani zinakwenda kutumika kibiashara”amesema Dk.Chamuriho
Aidha Dk.Chamuriho amesema kuwa wanaosanifu muindombinu ya ujenzi kama vile  madaraja wanataka kujua mtiririko na wingi wa maji ili waweze kusanifu madaraja hayo kama yanaweza  kuhimili nguvu za asili,takwimu hizo zinapatikana kwenu.
Hata hivyo ameongeza kuwa ubora  wa huduma za hali ya hewa umezidi kuongezeka na kuonekana kwa jamii kwa kiwango kikubwa, hivyo jitihada hizo zitumike pia katika ukusanyaji wa mapato na udhibiti wa huduma za hali ya hewa nchini.
Amesema kwa sasa  serikali imeanza kufunga rada mkoa wa Mtwara na wanataraji kuanza kufunga nyingine katika mikoa ya Mbeya ya Kigoma, kwa lengo la kutimiza makubaliano ya kimataifa ambayo serikali iliridhia kubadilishana taarifa kwa njia ya mtandao wa dunia (Global Telecommunication System).
Awali Mkurugenzi wa TMA Dk  Agnes Kijazi, amesema kuwa ili kuweka msingi imara kwa TMF mafunzo hayo yatawafanya kuwa na uwezo wa kutoa huduma bora zaidi kwa kukidhi mahitaji ya wadau nchini.
Dk.Kijazi amesema kuwa katika mafunzo hayo wanafunzi watahusika  kufanya mazoezi mbalimbali na majadiliano kwa lengo la kuinjengea menejimenti ya TMA uwezo katika maeneo ya udhibiti na ukusanyaji wa mapato katika huduma wanazotoa.
Amesema kuwa  viwango vya usahihi wa utabori wa hali ya hewa umezidi kuimarika kwa  mikaa 10 hadi kufikia zaidi ya asilimia 80 huku kiwango cha chini kilichowekwa na shirika la hali ya hewa duniani cha asilimia 70.
Kwa Upande wake  Meneja wa mafunzo wa Wakala ya Mafunzo kwa Njia ya Mtandao (TaGLA) Brown Hasunga amesema kuwa wameamua kutoa mafunzo hayo ili kuongeza uelewa kwa menejimenti ya mamlaka hiyo baada ya TMA kubadilika kutoka wakala hadi kuwa mamlaka.

No comments :

Post a Comment