Monday, March 9, 2020

JESHI LA POLISI LIMEBAINI MZEE MANGULA ALIWEKEWA SUMU,



*****************************
NA EMMANUEL MBATILO
Makamu mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Bara, Mhe.Philip Mangula imegundulika amewekewa sumu baada ya uchunguzi kufanyika na kubaini hivyo ijapokuwa
bado haijajulikana aliwekewa kwa njia ipi.
Ameyasema hayo leo, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa katika mkutano na wanahabari Jijini Dar es Salaam.
Akizungumza katika mkutano huo, Kamanda Mambosasa amesema kuwa taarifa hizo walizipata Februari 28 mwaka huu baada ya mzee huyo kudondoka ghafla katika ofisi ndogo ya chama Lumumba Jijini Dar es Salaam mara baada ya kumaliza kikao cha kamati kuu ya halmashauri kuu ya Taifa.
“Katika taarifa hiyo tulielezwa kwamba, Mzee Mangula alipelekwa Muhimbili na kulazwa ICU, Jeshi la polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama limebaini kwamba ndani ya mwili wa Mzee Mangula ulipatikana na sumu, kwa yeyote atakayebainika kupanga, awe ndani ya CCM, mwanafamilia ama Serikalini hatua kali zitachukuliwa dhidi yake ” amesema Kamanda Mambosasa.
Aidha Kamanda Mambosasa amesema kuwa upelelezi kuhusu namna ambavyo sumu hiyo iliingia mwilini bado unaendelea, na Jeshi hilo halitasta kuchukua hatua kali kwa mtu yeyote atakayebainika aliyehusika na uhalifu huo.

No comments :

Post a Comment