Monday, March 9, 2020

SERIKALI IMEWATAKA WANANCHI KUWA WABUNI KUKABILIANA NA CHANGAMOTO ZA KIUCHUMI



**************************
Na Magreth Mbinga
Serikali imewataka watu hasa waishio vijijini kupitia changamoto walizonazo kuibua ubunifu ili kukabiliana na changamoto za kiuchumi.
Rai hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa elimu sayansi na teknolojia William Olenasha katika
ufunguzi wa wiki ya ubunifu iliyofanyika katika Kijiji cha makumbusho jijini Dar es salaam.
“Nimezindua wiki ya ubunifu ambayo inakutanisha wadau na wabunifu mbalimbali kwaajili ya kutambulisha bidhaa zao ambazo wanabuni”alisema Olenasha.
Pia Olenasha amesema kama Tanzania inataka kukuza uchumi kwa kutegemea viwanda lazima iwe na wabunifu ndio maana wameanzisha mashindano ya wabunifu Taifa yatakayo fanyika mjini Dodoma.
Vilevile Mkurugenzi wa NHIF Joseph Evalisti amesema wao ndio waandaaji wa wiki ya ubunifu wameandaa tamasha hilo ili kuwakutanisha wabunifu na kuwafanya watambulike na watu mbalimbali.
“Tulianza na watu sita tulijikita zaidi hapa Dar es salaam kwa sasa tuna wabunifu wengi na tunataka twende nje ya mkoa huu wiki ijayo tunazindua wiki ya ubunifu Dodoma” alisema Joseph.
Hatahivyo mkurugenzi wa sayansi na teknolojia Dk Amosi Nungu amewataka vijana wajitokeze kwa wingi ili serikali iwasaidie kukuza ubunifu wao mpaka sasa wamewasaidia vijana sitini katika kuendeleza ubunifu wao katika nyanja mbalimbali.

No comments :

Post a Comment