……………………………………………………………………………….
Itakumbukwa kuwa mapema wiki hii
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli
alikutana na kufanya mazungumzo na viongozi watatu wa vyama vya
upinzani.
Viongozi hao ni Mshauri wa Chama
cha ACT-Wazalendo, Maalimu Seif Sharif Hamad, Mwenyekiti wa Chama cha
Wananchi (CUF), Prof. Ibrahim Lipumba na Mwenyekiti wa Chama cha
NCCR-Mageuzi, Bwana James Mbatia, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kituo cha
Demokrasia Tanzania (TCD).
Tume ya Haki za Binadamu na
Utawala Bora (THBUB) inapenda kuchukua fursa hii kumpongeza kwa dhati
Mhe. Rais kwa hatua yake hiyo ya kizalendo na muhimu kwa ustawi wa nchi
yetu.
Hatua hiyo ya Mhe. Rais ya
kukutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa vyama vya upinzani ni
kielelezo cha kukua kwa utawala bora nchini.
Aidha, Tume imefurahishwa na
ahadi aliyoitoa Mhe. Rais katika mazungumzo hayo ikiwa ni kwa mara ya
pili baada ya kutoa kauli kama hiyo kwa Mabalozi wawakilishi wa nchi
zao, katika ghafla ya kuanza mwaka mpya, kuwa uchaguzi mkuu ujao utakuwa
huru na wa haki. Bila shaka kauli hiyo inaonyesha dhamira aliyonayo
Mhe. Rais na Serikali yake katika kuhakikisha kuwa demokrasia, amani na
utulivu vinaendelea kushamiri hapa nchini – tunampongeza sana!
Kwa kauli hiyo ya Mhe. Rais,
Tume inaamini kuwa taasisi zenye dhamana ya kusimamia uchaguzi mkuu ujao
na wadau wa uchaguzi watachukua hatua mahsusi za kuhakikisha kuwa azma
ya Mhe. Rais inatimia.
Ni matumaini ya Tume kuwa hatua ya Mhe. Rais ya kufungua milango kwa viongozi wa vyama vya upinzani itakuwa endelevu.
Tume inamwomba Mhe. Rais
kuendeleza utaratibu huo wa kukutana na viongozi wa vyama vya upinzani
na makundi mengine pindi nafasi ya kufanya hivyo itakaporuhusu.
No comments :
Post a Comment