Mkuu wa Mkoa wa Dodoma
Dkt.Binilith Mahenge,akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake
wakati akitoa taarifa kuhusu kongamano la wadau wa elimu litakaloanza
tarehe 21 hadi 22 mwezi huu,2020 na Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania,Mhe.Kassim Majaliwa
Sehemu ya waandishi wa habari
wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt.Binilith Mahenge,(hayupo
pichani) alipokuwa akizungumza nao ofisini kwake kuhusu kongamano la
wadau wa elimu litakaloanza tarehe 21 hadi 22 mwezi huu,2020 na Mgeni
rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Mungano wa
Tanzania,Mhe.Kassim Majaliwa
Afisa Elimu Mkoa wa Dodoma Maria
Lyimo,akijibu maswali mbalimbali kutoka kwa waandishi wa habari (hawapo
pichani) kuhusu kongamano la wadau wa elimu litakaloanza tarehe 21 hadi
22 mwezi huu,2020 na Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa
Jamhuri ya Mungano wa Tanzania,Mhe.Kassim Majaliwa
………………………………………………………………………………Na.Alex Sonna,Dodoma.
Mkoa wa Dodoma unatarajia kuandaa kongamano la Wadau wa Elimu kuanzia
tarehe 21-22 mwezi huu 2020.
Akizungumza na Waandishi wa Habari Leo jijini Dodoma,Mkuu wa
Mkoa wa
Dodoma Dkt.Binilith Mahenge amesema lengo la kongamano hilo ni
kwa ajili ya kujadili changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya
Elimu Mkoani Dodoma hali ambayo husababisha kiwango cha elimu kuwa cha
chini mkoani hapa licha ya kuwa ni makao makuu ya nchi.
Dkt.Mahenge ametaja baadhi ya viashiria vinavyosababisha kushuka
kwa kiwango cha ufaulu kwa wanafunzi katika mkoa wa Dodoma ni pamoja na
umbali mrefu wa shule ,ufuatiliaji hafifu pamoja na mwamko mdogo wa
wazazi juu ya masuala ya elimu pamoja na miundombinu isiyokuwa
toshelezi.
Hivyo kongamano hilo litakutanisha wadau ili kuchambua
mikakati za kuinua kiwango cha elimu mkoani Dodoma ambapo kutakuwa na
shughuli kuu mbalimbali.
Aidha amesema kuwa kutakuwa na
uzindua wa kampeni endelevu ya ushiriki wa jamii katika uchangiaji wa
ujenzi wa miundombinu ya shule ,kufanya tathmini ya hali ya maono ya
wananchi ushiriki maendeleo ya elimu ,kubainisha masuala ya kiupambele
katika kuboresha sekta ya elimu pamoja kuamsha hamasa kwa jamii katika
suala la elimu kwa kutoa tuzo mbalimbali kwa walioonesha juhudi katika
suala la elimu.
Naye Afisa Elimu Mkoa wa Dodoma Maria Lyimo amesema jamii inatakiwa kuelewa
dhana ya sera ya elimu ya Msingi bila malipo kwani mzazi ana jukumu la kumnunulia mtoto wake mahitaji ya Msingi ya shuleni.
dhana ya sera ya elimu ya Msingi bila malipo kwani mzazi ana jukumu la kumnunulia mtoto wake mahitaji ya Msingi ya shuleni.
Kaulimbiu katika kongamano hilo ni “kuinua Kiwango cha Elimu
katika Mkoa wa Dodoma huku Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa
Jamhuri ya Mungano wa Tanzania,Mhe.Kassim Majaliwa Majaliwa .
No comments :
Post a Comment