Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Mhandisi
James Kilaba (katikati) akiwa na viongozi wengine wa Mamlaka hiyo,
wakati akizungumza leo Machi 5 mwaka 2020 jijini Dar es Salaam wakati wa
kikao kazi na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari pamoja na
waandishi waandamizi.
Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Mhandisi James Kilaba akifafanua jambo kwa wahariri wa vyombo vya habari nchini wakati wa kikao kazi.
Baadhi ya wahariri wa vyombo
mbalimbali vya habari nchini wakiwa makini kufuatilia mada zilizokuwa
zinatolewa wakati wa kikao kazi kati yao na maofisa wa TCRA wakiongozwa
na Mkurugenzi Mkuu Mhandisi James Kilaba.
Mkurugenzi wa TEHAMA wa Mamlaka ya
Mawasiliano Tanzania(TCRA) Connie Francis akielezea kwa kina namna
ambavyo TCRA inafanya shughuli zake zikiwemo za kusimamiwa wadau wao.
******************************
NA MWANDISHI WETU
KWA mara ya kwanza hapa nchini,
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) itatoa Tuzo kwa Makampuni
mbalimbali yanayotoa Huduma Bora za Mawasiliano.
Akizungumza leo Machi 5,2020
wakati wa kikao kazi na
wahariri na waandishi wa habari waandamizi wa
vyombo vya habari nchini, kwenye makao makuu ya TCRA jijini Dar es
Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Mhandisi James M. Kilaba amesema lengo
kuu la Tuzo hii, ni kutambua na kutunza Kampuni zitakazo chaguliwa kwa
kutoa Huduma Bora. Pia kuhamashisha Ubunifu katika utoaji wa Huduma za
Mawasiliano.
Makampuni yote yaliyopewa leseni
na TCRA ya kutoa huduma ya Mawasiliano yanawajibika kuwasilisha maombi
ya kushiriki kabla ya Tarehe 15 Machi, 2020.
Alisema uteuzi utaanza tarehe 16 hadi 31 Machi, 2020 na uteuzi wa waliokidhi vigezo vya kushiriki.
Tarehe 1 hadi 30 Aprili 2020-
Wananchi watapata fursa ya kupiga kura kuchagua Kampuni ipi ina Huduma
Bora ipi yenye Ubunifu inayo Faidisha Wananchi.
Alisema Tarehe 15 Mei, 2020
Sherehe kubwa ya Kutoa Tuzo kwa Watoa Huduma Bora itafanyika Mlimani
City Jijini Dar Es Salaam na Kuhudhuriwa na Viongozi wa Juu wa Nchi,
pamoja na Wakuu wa Tasisi za Mawasiliano wa Umoja wa MaTaifa (UN) Wanao
simamia Mawasiliano Ulimwenguni, ikiwemo Tasisi ya Mawasiliano
Duniani ITU- Geneva, Umoja wa Posta Duniani ( UPU), Umoja wa Posta
Afrika (PAPU) na Tasisi nyinginezo.
Mhandisi Kilaba Alisema Tuzo 17 zitatolewa kwa Makampuni 15, ya huduma za aina mbali mbali.
Mhandisi Kilaba Alisema Tuzo 17 zitatolewa kwa Makampuni 15, ya huduma za aina mbali mbali.
Aliyataja Makampuni hayo kuwa ni
pamoja na, Watoa Huduma za Utangazaji, Radio na Televisheni, Kampuni
Bora ya Radio na Televisheni Mtandaoni, Kampuni yenye Huduma Bora ya
Simu za Mkononi, Kampuni Bora ya Huduma za Posta na Usafirishaji wa
Vifurushi na Vipeto, Kampuni Bora ya Huduma za Intanet na, Kampuni Bora
ya Wasambazaji wa Maudhui ( Multiplex Operators)
Zingine ni Blog Bora, Kampuni Bora ya Utoaji wa Huduma za Intanent na Kampuni nyingine zote zenye leseni ya TCRA.
” TCRA imedhamiria kuongeza Ustawi
wa Wananchi wa Tanzania kwa Kupitia Huduma Bora za TEHAMA zenye Ubunifu
zinazo Faidisha Jamii” amesema Mhandisi Kilaba.
Zaidi wa Wahariri 50 wa Vyombo vya
Habari mbalimbali hapa nchini wamehudhuria mafunzo hayo yaliyofanyika
makao makuu ya TCRA, Mawasiliano Towers, jijini Dar Es Salaam, Tarehe
5/03/2020.
No comments :
Post a Comment