Friday, March 6, 2020

IMF: UCHUMI WA TANZANIA WAENDELEA KUKUA KWA ASILIMIA 6.



Mkurugenzi wa Kurugenzi Utafiti na sera za Uchumi Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Dk. Suleiman Misango akizungumzia kuhusu ripoti iliyotolewa na IMF jijini Arusha mara baada ya kufunga semina  ya waandishi wa habari za uchumi na fedha iliyokuwa ikifanyika kwa siku tano jijini humo.
……………………………………………
IMF Imetoa mhutasari wa taarifa yao kuhusu mwenendo wa ukuaji wa uchumi wa Tanzania na matarajio yake  ile taarifa yao fupi imeelezea mwenendo wa
uchumi kwa mwaka 2019 wakieleza kuwa utakuwa kwa asilimia 6 na   wakaongeza kuwa umekuwa ukifanya vizuri.
Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Utafiti na sera za Uchumi Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Dk. Suleiman Misango wakati akizungumza jijini Arusha mara baada ya kufunga semina  ya waandishi wa habari za uchumi na fedha iliyokuwa ikifanyika kwa siku tano jijini humo.
“Sisi tunasema kwa hapo baadaye uchumi wetu utakuwa zaidi, Takwimu zetu za hivi karibuni Robo ya kwanza mwaka 2019 inaishia machi, ya pili inaishia Juni na ya  tatu inaishia septemba kwa wastani katika kipindi hicho uchumi wetu ulikuwa kwa asilimia 6.9 na tunatarajia kwamba ile robo ya nne ambayo ndiyo inafunga mwaka tunaamini ukuaji wa uchumi wetu utakuwa kwa asilimia 7.
Dk. Suleiman Misango amesema kwa siku za Baadaye tunakubaliana na IMF kwamba kama tutakwenda na utaratibu na nguvu kama hizi ukuaji wa uchumi wetu utakuwa zaidi asilimia 7 kwa siku za karibuni na siku za muda wa kati .
Amesema kutokana na uwekezaji mkubwa unaofanywa na serikali katika sekta za Nishati , Miundombinu, Afya, Elimu, Mawasiliano , Umeme na Shughuli zingine za uzalishaji mali uwekezaji huu ndiyo wezeshi kwa ajili ya Shughuli mbalimbali za kiuchumi,ndiyo maana hali ya ukuaji wa uchumi imekuwa ikienda vizuri.
“Ili kuweza kuharakisha maendeleo unahitaji nishati ya umeme, Ili kuharakisha maendeleo unahitaji kuboresha miundombinu ya Reli na Barabara ili kuharakisha maendeleo  unahitaji kuboresha Elimu, Afya na mambo mengine”Amesema Dk. Misango.
Amesema ripoti hiyo pia imezungumzia mfumuko wa bei ambapo IMF wamekiri kabisa na kuridhika kwamba mfumuko wa bei umekuwa mdogo na mwaka jana wastani ulikuwa 3.5,  Mwezi wa Januari kulikuwa na ukuaji wa asilimia 3.7 tunatarajia mfumuko wa bei utaendelea kuwa mdogo na IMF wenyewe wamesema kabisa kuwa mfumuko wa bei utaendelea kuwa mdogo chini ya malengo yetu ya muda wa kati ya asilimia 5.
Ameeleza kuwa ripoti hiyo pia imezungumzaia pia Sekta ya nje ya Tanzania katika biashara na nchi zingine ambapo wameridhika na mwenendo wa sekta yetu katika mauzo ya nje. Yameendelea kuwa mazuri na vilevile akiba ya fedha za kigeni imeendelea kuwa ya kutosha, tunaweza kuagiza bidaa na huduma kutoka nje kwa miezi mitano ambapo  sisi pia takwimu zetu za hivi karibuni zinaonesha tunaweza kuagiza bidhaa kutoka nje kwa miezi sita.

No comments :

Post a Comment