Katikati ni Diwani
mstaafu wa viti maalumu kata ya Moshono,Veronica Mwilange akikabithi
msaada kwa mama mwenye uhitaji anayetokea katika Kaya maskini katika
kata ya Moshono mkoani Arusha (Happy Lazaro)
Afisa maendeleo kata
ya Moshono Salome Njau akitoa taarifa fupi ya maendeleo ya vituo vya
watoto wanaoishi katika mazingira magumu kata ya Moshono (Happy Lazaro)
Baadhi ya vitu vilivyotolewa katika kituo cha
watoto yatima katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani inayofanyika
kesho.(Happy Lazaro).
*******************************
Happy Lazaro ,Arusha
Wakati kilele cha maadhimisho ya siku ya
Mwanamke duniani ikitarajiwa kufanyika Machi 8 ya kila mwaka ,wanawake
wa kata ya Moshono katika halmashaurinya jiji la Arusha,wameyatumia
maadhimisho hayo kutoa misaada Mbalimbali kwa watoto yatima katika kituo
cha Bethlehem kilichopo katika kata hiyo.
Akiongea mara baada
ya kukabidhi msaada huo uliotolewa na wanawake wa kata hiyo ikiwemo
vyakula,sabuni na Nguo ,mwenyekiti wa UWT ,CCM wilaya ya Arusha,Mary
Kisaka amewapongeza wanawake hao kwa kutumia maadhimisho hayo
kuwakumbuka watoto yatima.
Aidha amewataka
wanawake kuondoa woga na kujiamini ili waweze kushika nyadhifa
mbalimbali za uongozi nchini kuweza kufikia adhimio la Beijing la
kufikia hamsini kwa hamsini.
Baadhi ya washiriki
katika hafla hiyo,akiwemo diwani wa viti maalumu aliyejihudhulu
,Veronica Mwelange ,alisema lengo la kutoa Msaada huo katika kituo cha
watoto yatima ni kuonyesha upendo kwa watoto hao na wao kama wazazi
wameonelea umuhimu wa kuwatembea watoto hao na kula hao chakula cha
mchana kama sehemu ya maadgimisho ya siku ya mwanamke.
Wengine walioshiriki
maadhimisho hayo ni pamoja na afisa maendeleo ya jamii kata ya Moshono
,Salome Njau ambaye amesema akina mama kutoka mitaa tisa katika kata ya
Moshono waliweza kuchangishana na kufanikiwa kupata kilo 100 za
mchele,sabuni ,Unga wa ngano na vinywaji mbalimbali na kutoa msaada
katika kituo hicho cha watoto yatima.
Kilele cha aadhimisho
ya siku ya mwanamke duniani kinatarajia kuadhimishwa Siku ya jumapili
Machi 8 ya kila mwaka ambapo kauli mbiu ni kizazi cha usawa kwa
maendeleo ya Tanzania ya sasa na baadae huku ikielezwa kwamba kiwango
cha wanawake kushika nyadhifa mbalimbali hapa nchini kikipanda.
No comments :
Post a Comment