Thursday, March 5, 2020

KISHINDO CHA AWAMU YA TANO



**************************
Na Emmanuel J. Shilatu
Serikali ya awamu ya 5 inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli imefanya mambo makubwa kwenye kila sekta. Yafuatayo ni baadhi tu ya mambo makubwa ya... kishindo zaidi yaliyofanyika ndani ya miaka 4 tu.
MAPATO
Tangu tupate Uhuru mwaka 1961 hadi mwaka 2015 makusanyo ya mapato ya nchi kwa mwezi hayajawahi kuzidi Tsh. Bilioni 700 ila ndani ya miaka 4 kuanzia 2015 – 2019 makusanyo ya mapato kwa mwezi mmoja yamefika Tsh. Trillion 1.9 . Hii maana yake mianya ya upotevu imedhibitika, uwezo wa nchi kimapato umeimarika na hivyo uwezo wa Serikali kuwahudumia Wananchi wake utaongezeka pia.
AFYA
Kuanzia mwaka 1961 hadi 2019 sawa miaka 54 kulikuwa na hospitali za wilaya 70 ila ndani ya miaka 4 kuanzia 2015 – 2019 jumla ya hospitali za wilaya 69 zimejengwa na Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Magufuli na vinatoa huduma za afya.
Tangu mwaka 1961 – 2015 sawa na miaka 54 kulikuwa na vituo vya afya 150. Ndani ya miaka 4 kuanzia 2015 – 2019 jumla ya vituo vya afya 381 vimejengwa na vinafanya kazi.
Hivyo ndani ya miaka 4 tu zimejengwa Zahanati 227, hospitali za wilaya 69 na vituo vya afya 381 sawa na jumla ya vituo vya kutolea huduma za afya 677.
UMEME
Mtandao wa umeme uliosambaa kwa umbali wa kilomita zaidi ya 69,204.39 na kufikisha upatikanaji wa umeme kuwa asilimia 67.5
Leo hii Taifa linajenga umeme kwenye bwawa la umeme la Nyerere la Mto Rufiji ambao utazalisha umeme megawatts zaidi ya 2115. Huu ni umeme mkubwa kuzidi umeme uliopo tangu tupate Uhuru. 
USAFIRISHAJI NA MIUNDO MBINU
Kwa zaidi ya miaka 30 nchi haikuwa na ndege zake ila ndani ya miaka 4 kuanzia 2015 – 2019 zaidi ya ndege mpya 8 zimenunuliwa na zinaendelea kutoa huduma ya usafirishaji.
Tangu tupate Uhuru Watanzania tunatumia treni ya Dizeli lakini ndani ya miaka 4 Serikali imeanza ujenzi wa reli ya kisasa kwa kiwango cha standard gauge (SGR) kutoka Dar hadi Mwanza. Utakuwa usafiri wa haraka kwani unatumia umeme, unaobeba mizigo mingi na nafuu zaidi.
Tangu Uhuru tumekuwa tukitumia miundombinu ya Wakoloni lakini leo Taifa linajenga miundombinu ya kisasa ya flyovers ya pale Tazara, Ubungo interchange, reli ya SGR na madaraja yanayopita ama kukatiza katikati ya bahari na maziwa.
Leo hii nchi nzima Kuna ujenzi wa viwanja vya ndege, ujenzi wa barabara na upanuzi wa bandari za Dar es salaam, Mtwara, Tanga na kwenye maziwa makuu nchi nzima.
ELIMU
Kwa zaidi ya miaka 30 Elimu yetu ilikuwa ya kulipia ila leo hii ndani ya miaka 4 tunashuhudia Elimu bure ikitolewa kuanzia shule ya msingi hadi sekondari. Hakika hiki ni zaidi ya kishindo cha awamu ya 5.

No comments :

Post a Comment