BancABC Tanzania Managing Director
Iman John (second right) displays a Visa E-Commerce Issuing Growth
Award that the bank won for its innovation and dedication towards
facilitating secure online transactions in the country during an event
held in Dar es Salaam over the weekend.
BancABC Tanzania Managing Director
(second right) shows a Visa E-Commerce Issuing Growth Award after the
bank won the award for its innovation and dedication towards
facilitating secure online transactions in the country during an event
held in Dar es Salaam over the weekend. Right is the Head of Marketing
and Communications Upendo Nkini, Head of Banking Easy Sales Emmanuel
Nzutu, second left and Left Agency Banking Manager Mwita Rhobi. (Picture
courtesy of BancABC Tanzania).
**************************
BancABC Tanzania ambayo ni kampuni tanzu ya Atlas Mara, kwa mara nyingine imeshinda tuzo ya Visa maarufu kama “Visa E-commerce Issuing Growth Award” kutokana
na...
huduma zake za kipekee za malipo ya mtandaoni ambazo ni salama na
nafuu hapa nchini. Benki hiyo imejishindia tuzo hiyo ya Visa kutokana na
matumizi ya kadi zake za Visa ambazo wateja wanatumia kulipia huduma
mbali mbali kwa njia ya mtandao.
Hii inakuja ikiwa ni mara ya pili
kwa benki kushinda tuzo kama hiyo. Mwaka 2016, BancABC Tanzania
ilishinda tuzo hiyo kwa kuongoza kwenye matuzi ya kadi zake za Visa
kutumika kwenye kulipia huduma kwa njia ya mtandao. Hii inatokana na
kuwa na kadi za Visa za kipekee ambazo zina usalama wa hali ya juu kwa
wateja wake.
Akizungumza jana jijini Dar es
Salaam baada ya kupokea tuzo hiyo, Mkurugenzi Mtendaji BancABC Tanzania
Imani John alisema, ‘Tunayo Furaha kubwa kuweza kujishindia tuzo kwenye
soko letu ambalo lina ushindani mkubwa sana na hii inaonyesha ni jinsi
gani tumejidhatiti kuhakikisha tunawarahisishia wateja
wetu kufanya miamala yao mbalimbali,’ alisema John huku akitoa shukrani
za kipekee kwa wateja wa BancABC Tanzania kwa kuonyesha imani yao kwa
kutumia kadi za Visa za benki hiyo kufanya malipo kwa njia ya mtandao.
‘Bila nyinyi hatungeweza kushinda tuzo hii na tunawahakikishia wateja
wetu kuwa tutaendelea kutoa huduma za kipekee hili kuendelea kuweka
imani kwa wateja wetu,’ John aliongeza.
Akizungumza kwenye tukio la
kukabidhiwa tuzo hizo, Mkuu wa Kitengo cha Huduma za kidijitali BancABC
Tanzania Silas Matoi alisema ‘Ni Furaha sana kwetu kushinda tuzo hii
ambayo ni mara ya pili kwetu. Shukrani za kipekee kwa wateja
wetu wanaotumia kadi zetu za Visa kulipia huduma mbali mbali kwa njia ya
mtandao. Matumizi ya wateja wetu wa kadi ya Visa ndio kumetufanya
kushinda tuzo hii. Tunajisikia ufahari sana kuendelea kuwahudumia na
tunawaahidi kuendelea kuwaletea huduma zilizo bora na nzuri zaidi,’
alisema Matoi.
Matoi aliongeza, ‘Ikiwa ni
moja ya njia ya kukuza malipo yaliyo salama na rahisi kwa njia ya
mtandao, mtu yeyote anaweza kumiliki kadi ya Visa hata kama hana akaunti
na BancABC. Kadi ya Visa ni rahisi kuongeza fedha na inatoa wasi wasi
wa kutembea na fedha taslimu wakati wa kwenda kufanya manunuzi.
Matoi alisema kuwa kadi za
Visa zimeundwa kwa umakini mkubwa na mfumo salama wa chip na PIN wenye
teknolojia ya hali ya juu ambayo inatumika duniani kote na hivyo kuondoa
tatizo la kuibiwa. Pia kadi hii ina huduma ya kupokea ujumbe mfupi wa
maneno na hivyo kumfanya mmliki kupata taarifa zote za kila muamala au
malipo anayofanya kwa njia ya mtandao.
“Hakuna haja ya kuhangaika wapi
unaweza kutumia kadi za Visa kwani huduma zake zinapatikana masaa 24 kwa
siku saba za wiki kwenye ATM za Visa milioni 2.7 duniani kote na kwenye
maduka milioni 46 ya rejareja ulimwenguni kote huku kwa Tanzania
ikipatikana kwenye mashine 400 za ATM za Visa na maduka Zaidi ya
1000 yanayokubali kadi ya Visa” alisema Matoi.
Kwa upande wake, Meneja
Mkazi wa kampuni ya Visa Tanzania, Bi. Olive Njoroge alisema,
‘Tunawashukuru wenzetu wa BancABC Tanzania kwa juhudi kubwa ambazo
wameziweka, kwa jinsi walivyoweza kujitangaza na kuwafahamisha wateja
wao kuwa unaweza kutumia kadi ya Visa kwenye kulipia bidhaa au huduma na
pia kwenye kutoa fedha, lakini pia kwa kulipia huduma mbali mbali kwa
njia ya mtandao. Hii ni hatua kubwa na muhimu na ndio sababu tumekuja
pamoja kuwapongeza’. Alisema Njoroge huku akiongeza kuwa kadi za Visa ni
salama na zinaweza kutumika popote ambapo kadi ya Visa inakubalika.
No comments :
Post a Comment