Friday, March 6, 2020

KIGWANGALLA ASHUHUDIA UVISHWAJI VYEO KWA MENEJIMENTI YA NCAA



Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamis Kigwangalla akiongea na watendaji pamoja na watumishi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro baada ya hafla ya uvishwaji Menejimenti ya Mamlaka hiyo.
Sehemu ya Wajumbe wa Menejimeti ya NCAA waliovalishwa vyeo waakisikiliza hotuba wa Waziri wa Maliasili na Utalii katika sherehe hiyo.
Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro Prof. Abihudi Kaswamila (aliyevaa suti) akimvalisha cheo Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi anayesimamia utawala na Rasilimali watu Bw. Samson Ntunga.
Kamishna wa Uhifadhi wa NCAA Dkt Freddy Manongi akitoa taarifa kwa Waziri wa Maliasili na utalii Dkt Hamis Kigwangalla ( hayupo pichani) kuhusu utekelezaji wa sheria ya jeshi Usu katika utendaji kazi wa Mamlaka hiyo.
…………………………………………………………………………………………….
Na Mwandishi wetu-NCAA
Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla ameshuhudia uvishwaji vyeo kwa
menejimenti ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) ikiwa ni utekelezaji wa sheria kwa taasisi zilizoko chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii kujiendesha kijeshi katika usimamizi wa Rasilimali za wanyamapori.
Katika sherehe hiyo wajumbe 15 wa menejimenti ya Ngorongoro walivishwa vyeo ambapo idadi hiyo inajumuisha Naibu Makamishna wa uhifadhi wawili na Makamishna wasaidizi Waandamizi wa uhifadhi 13.
Katika hafla hiyo Waziri Kigwangalla ameielekeza menejimenti ya NCAA kutumia mafunzo mbalimbali ya kijeshi waliyoyapata na kuhakikisha kuwa wanazingatia nidhamu ya kazi, kasi katika utekelezaji wa majukumu na kuzingatia mtiririko mzuri wa amri hasa kwa watumishi walioko chini yao ili kuhakikisha kuwaa utendaji kazi inaimarishwa na kutatua changamoto ndogondogo kwa uharaka na kijeshi usu.
Mhe. Kigwangalla emesema  kuwa sambamba na mafunzo mbalimbali ambayo viongozi wa sekta za uhifadhi  wamekuwa wakiyapata katika vyuo vya jeshi usu vya Mlele na Mbulumbulu wizara yake itashirikiana na Jeshi la Polisi ili kuwapa kozi ya uongozi wa masuala ya kijeshi katika chuo cha Polisi Moshi ili kuongeza ufanishi wa usimamizi wa mifumo ya kijeshi katika utekelezaji wa majukumu yao.
Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro Profesa Abihudi Kaswamilla amemhakikishia Waziri Kigwangalla kuwa, bodi anayoiongoza  itaendelea kusimamia utekelezaji wa mfumo wa jeshi usu kwa watendaji wa NCAA ili kuhakikisha kuwa majukumu makuu ya uhifadhi, utalii na maendeleo ya jamii yanatekelezwa ipasavyo.
Kamishna wa Uhifadhi wa NCAA Dkt. Freddy Manongi amebainisha kuwa Mamlaka hiyo itaendelea kusimamia uteekelezaji wa mfumo wa jeshi usu kwa watumishi wa Mamlaka hiyo ili kuhakikisha kuwa sekta ya utalii inayochangia fedha za kigeni kwa asilimia 25 na pato la taifa kwa zaidi ya asilimia 17 inazidi kuimarika na kuongezeka.
Viongozi wengine waliohudhuria hafla hiyo ni pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo, wakuu wa Wilaya za Ngorongoro na Karatu, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Saimon Sirro, Kamishna wa Uhifadhi wa  TANAPA Dkt Allan Kijazi na viongozi wengine kutoka vyombo vya ulinzi na Usalama. 

No comments :

Post a Comment