Mkuu wa majeshi
nchini IGP Sirro akikata utepe ishara ya kuweka jiwe la msingi katika
uzinduzi wa nyumba za polisi zinazojengwa na mwekezaji katika hoteli za
kitalii za Grand Media katika eneo la Feed force lililopo kata ya Muriet
mjini hapa pembeni yake ni Balozi wa heshima serikali ya Dubai UNT
,Fouad Mustafa Martis
Mkuu wa majeshi
nchini IGP Sirro akisoma maelezo yaliyoandikwa katika kibao Cha jiwe la
msingi la nyumba za polisi katika kata ya Muriet zilizopo mkoani Arusha
,pembeni yake ni Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akishuhudia
uzinduzi huo.
Mratibu wa mradi huo
wa ujenzi wa nyumba za polisi katika kata ya Muriet,kutoka kampuni ya
China ya CRJE (EA)Ltd ,Tumainiel Seria akizungumza katika uzinduzi huo
kuhusiana na mradi huo.
Mkuu wa majeshi
nchini IGP Sirro akiongozana na viongozi mbalimbali wakati wa kukagua
jengo hilo katika eneo la Muriet mkoani Arusha
Mkuu wa majeshi
nchini ,IGP Simon Sirro akizungumza na wananchi waliohudhuria katika
hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi katika nyumba za polisi katika kata
ya Muriet mkoani Arusha
(Happy Lazaro)
……………………………………………………………………………………………..
Happy Lazaro,Arusha.
Mkuu wa majeshi
nchini IGP Simon Sirro amekipandisha hadhi kituo Cha polisi Cha Muriet
na kuwa kituo Cha polisi cha wilaya baada ya ombi hilo kutolewa na mkuu
wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo.
Sirro amekipandisha hadhi kituo hicho jana wakati akizungumza
katika hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi kwa ajili ya ujenzi wa
nyumba za polisi sita zinazojengwa kwa ufadhili wa mwekezaji wa hoteli
za kitalii za GrandMelia ambaye amejitolea kujenga nyumba hizo sita za
Askari polisi katika eneo la FFU Kata ya Muriet mkoani Arusha.
Aidha Sirro
alimpongeza mwekezaji huyo kwa moyo huo wa kujitolea na kufikia hatua
ya kujenga kituo hicho ambacho kitasaidia Sana kupunguza matukio ya
uhalifu katika kata hiyo kutokana na idadi kubwa ya wananchi waliopo.
“Kuanzia leo
nimekipandisha hadhi kituo hiki na kuwa Cha wilaya Kama ambavyo
nimeombwa na mkuu wa mkoa wa Arusha kutokana na kuwa ni ombi la
wananchi kwa muda mrefu na nitamleta OCD na OCCID hapa ili waweze
kushirikiana kwa pamoja na naombeni Sana wananchi want mfuate sheria
zilizopo kwani tumejipanga kutokomeza uhalifu kabisa.”alisema Sirro.
Aidha Sirro alitumia
fursa hiyo kuwataka wazazi kuhakikisha wanawalea watoto wao katika
maadili mema ili waweze kuepukana na vijana wanaokuja kuwa wahalifu
mtaani .
Aliwataka wananchi
katika kuelekea uchaguzi kuhakikisha wanafuata sheria na taratibu za
nchi huku akiwataka uchaguzi huo kutowafarakanisha badala yake Kila my
atimize wajibu wake na kwa wakati wake pia.
“Ninachotaka
kuwaeleza ni kuwa sisi Kama jeshi la polisi kazi yetu ni kulinda
wananchi na Mali zao na hatuko tayari kuona sheria zinavunjwa na
ikitokea mwanasiasa akiingia kufanya uhalifu lazima ashughulikiwe Kama
mhalifu mwingine”alisema Sirro.
Naye Mkuu wa mkoa wa
Arusha ,Mrisho Gambo alimshukuru IGP Sirro kwa kukubali ombi lake na
kukipandisha hadhi kituo hicho cha polisi ambapo itasaidia Sana
kupunguza uhalifu katika kata hiyo huku ikilinganishwa ni eneo
linalokuwa kwa Kasi kutokana na idadi kubwa ya watu kuendelea kuhamia.
Gambo alisema
kuwa,ameshukuru Sana kutimiza ahadi yake ya kujenga nyumba za polisi kwa
kushirikiana na wafadhili mbalimbali ,ambapo alisema kuwa jeshi
limekuwa likijipanga kuhakikisha kunakuwepo kwa ulinzi wa kutosha kwa
wananchi na Mali zao,hivyo ili waweze kutimiza wajibu wao vizuri ni
lazima waboreshewe mazingira yao .
“Kwanza kabisa
nakushukuru Sana IGP kwa kutupatia Kamanda wa mfano ambaye ni mahiri
mchapa kazi anayehakikisha mkoa wetu unakuwa salama muda wote na tangu
utuletee huyo Kamanda kwa kweli uhalifu umepungua kwa kiasi kikubwa Sana
akishirikiana na Askari wake pamoja na kamati ya ulinzi na usalama ya
mkoa wa Arusha”alisema Muro.
Hata hivyo alitumia
fursa hiyo kuwashukuru wawekezaji hao wa hoteli ya Grandmelia kwa
kusaidia ujenzi wa kituo hicho kwani kwa kufanya hivyo inaonyesha jinsi
ambavyo wapo karibu na jeshi Hilo na kwa kufanya hivyo wameweza kujenga
taswira nzuri.”alisema Gambo.
Aidha alitumia fursa
hiyo kuwataka wawekezaji wa mkoa wa Arusha kuiga mfano huo kwa
kuhakikisha wanaisaidia jamii katika shughuli mbalimbali za maendeleo
Kama walivyofanya wawekezaji hao.
Kamanda wa jeshi la
polisi mkoani Arusha, Jonathan Shanna ameshukuru kwa kuona Mkuu wa mkoa
wa Arusha Mrisho Gambo ametimiza ahadi yake ya kujenga nyumba sita za
polisi kila mwaka ikiwa ni ahadi yake kwa jeshi la polisi.
Shana alisema kuwa,
jeshi la polisi mwaka Jana walipata nyumba za kisasa eneo la polisi mess
pamoja na eneo la feed force Njiro nyumba sita ambapo kwa mwaka huu
tena wamepata nyumba sita pamoja na kupewa gari kwa askari wake .
Naye Balozi wa
heshima serikali ya Dubai UNT , Fouad Mustafa Martis alisema
kuwa,wamefikia hatua ya kusaidia ujenzi wa kituo hicho Cha polisi
kutokana na mahusiano mazuri waliyo nayo na jeshi hilo,huku wakiahidi
kuendelea kusaidia zaidi .
Alisema kuwa,wamekuwa
wakishirikiana shughuli mbalimbali za maendeleo kwa kurudisha faida
wanayoipata kwa wananchi na kuwa wamekuwa na mahusiano mazuri Sana na
jeshi hilo kwa kushirikiana katika maswala mbalimbali.
Naye Mratibu wa mradi
huo Tumainiel Seria kutoka kampuni ya China ya CRJE (EA) Ltd alisema
kuwa ,wanashukuru jeshi la polisi kwa kuwapa dhamana ya ujenzi wa kituo
hicho na kuwaamini ambapo waliahidi kuutekeleza kwa wakati na kukamilika
kwa muda uliopangwa ambao ni mwezi wa nne mwaka huu.
Alisema kuwa,nyumba
hizo hadi kukamilika zitagharimu kiasi Cha dola za kimarekani laki mbili
ambapo Hadi Sasa hivi limeshakamilika kwa asilimia 40 .
No comments :
Post a Comment