Baadhi ya wadau wa Bonde la mto Katuma katika jukwaa la tatu la kidakio cha mto Katuma kilichofanyika katika manispaa ya Mpanda
…………………………………………………………………………………………..
Na Mwandishi wetu, Katavi
Wadau mbalimbali kutoka katika
asasi za kijamii wameishauri Bodi ya Maji ya Bonde la Ziwa Rukwa kuweka
mipaka inayoonekana katika vyanzo vya maji ili kurahisisha uelewa wa
mipaka hiyo kwa wananchi na hivyo kuepusha migogoro isiyo ya lazima
Wametoa ushauri huo katika
jukwaa la tatu la wadau wanaotumia maji katika kidakio cha mto Katuma
unaotiririsha maji katika Ziwa Rukwa; kilicholenga kuendeleza utunzaji
wa rasilimali za maji
“Kama tutafyeka kama TANAPA
wanavyofanya ni rahisi kwa mtu kuona mbona hapa pamefyekwa na kule
kumehidhawa, kwahiyo atajua kumbe kule ni hifadhi tungefanya hivyo hata
kwa bonde la mto Mpanda” alisema mama Fulgensia Kapama kutoka asasi ya
wanawake ya KAWODEO
Aidha wadau hao wamependekeza kuwepo na sheria za ndogo kwa ajili ya kulinda vyanzo vya maji
Akitolea mfano wa hifadhi ya
jamii ya Mpimbwe mkurugenzi wa taasisi ya UDESSO bwana Eden Waimba
ameiomba serikali na wadau mbalimbali kuongeza nguvu katika kuilinda
hifadhi hiyo
“Kule kuna wanyama pori
kwahiyo ni chanzo cha mapato pia kwa taifa; ila sasa imeanza kuingilia
na shughuli mbalimbali za kibinadamu” alisema
Bwana Thadeus Ndeseiyo ni
Mjumbe wa Bodi ya Maji ya Bonde la Ziwa Rukwa; amesema kuna umuhimu
mkubwa wa kutunza vyanzo vya maji kwa manufaa ya viumbe hai
No comments :
Post a Comment