Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Christopher Kadio (kushoto) akipokea taarifa ya
makabidhiano kutoka kwa aliyekuwa Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo,
Ramadhani Kailima, katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara hiyo, jijini
Dodoma, leo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Christopher Kadio akizungumza katika kikao cha
makabidhiano kati yake na aliyekuwa Kaimu Katibu Mkuu, Ramadhani Kailima
(kulia), katika ukumbi wa mikutano wa Wizara, jijini Dodoma, leo.
Makabidhiano hayo yalihudhuriwa na viongozi wa Wizara hiyo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Christopher Kadio (katikati) akimsikiliza aliyekuwa Kaimu
Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Ramadhani Kailima, baada ya makabidhiano ya
ofisi yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara, jijini Dodoma,
leo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Christopher Kadio (katikati) akimsikiliza Mkurugenzi wa
Utawala na Rasilimaliwatu wa Wizara hiyo, Emmanuel Kayuni, baada ya
Katibu MKuu huyo, kukabidhiwa Ofisi na Kaimu Katibu Mkuu, Ramadhani
Kailima (wapili kulia) katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara, jijini
Dodoma, leo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Christopher Kadio akizungumza katika kikao cha
makabidhiano kati yake na aliyekuwa Kaimu Katibu Mkuu, Ramadhani Kailima
(kushoto kwa Katibu Mkuu), katika ukumbi wa mikutano wa Wizara, jijini
Dodoma, leo. Makabidhiano hayo yalihudhuriwa na viongozi wa Wizara hiyo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Christopher Kadio (kushoto) akisalimiana na Mkurugenzi wa
Idara ya Huduma kwa Wakimbizi, Sudi Mwakibasi, wakati Katibu Mkuu
alipokuwa anawasili Wizarani, jijini Dodoma, leo, kwa ajili makabidhiano
ya ofisi kati yake na aliyekuwa Kaimu Katibu Mkuu, Ramadhani Kailima
(kushoto). Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
……………………………………………………………………………………………………..
Na Mwandishi Wetu, MOHA, Dodoma.
KATIBU Mkuu wa Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Christopher Kadio, amewataka
Wakuu wa Idara na Vitengo wa
Wizara yake wafanye kazi kwa ushirikiano na wawe wazi ili kuondoa
changamoto mbalimbali zilizopo ndani ya Wizara hiyo.
Akizungumza baada ya makabidhiano
ya ofisi kati yake na aliyekuwa Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo,
Ramadhani Kailima, yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Wizara
hiyo jijini Dodoma, leo, Katibu Mkuu Kadio amewataka viongozi hao
kufanya kazi kwa pamoja na kuwa wazi ili kuiletea Wizara na Serikali kwa
ujumla mafanikio chanya.
“Nashukuru kwa kunikaribisha,
nimefurahi kuwa nanyi, ila tufanye kazi kwa mashauriano kwa pamoja, ili
tuweze kutatua changamoto mbalimbali ambazo kila Wizara wanazo, na pia
nasi tunazo, “ alisema Kadio.
Pia Kadio alielekeza kuonana na
kila Mkuu wa Idara na Kitengo baada ya makabidhiano hayo, ili kusikiliza
majukumu yao, pamoja na kujua changamoto mbalimbali zinazowakabili na
kutafuta njia ya kuzitafua.
“Nataka mje tuzungumza, kila mmoja
wenu aje ofisini kwangu tuzungumze, na pia muwe wazi, muwe wakweli ili
nijue majukumu yenu, changamoto zenu ili tuweze kusaidiana,” alisema
Kadio.
Katibu Mkuu Kadio pia aliwapongeza
kwa kazi nzuri ambazo Wizara imekuwa inazifanya kwa kipindi chote na
kupitia utendaji huo mzuri kuna maboresho na mafanikio ya mambo
mbalimbali ndani ya Wizara.
“Nawapongeza kwa kazi nzuri
mnazozifanya licha ya kuwepo kwa changamoto lakini tutapambana nazo,
kuna maboresho na mmefanikiwa mambo mengi na bado tuna fursa ya kufanya
mazuri zaidi,” alisema Kadio.
Pia Kadio alisema anapenda kila
kiongozi kuwa wazi, na kusema yoyote bila woga kwasababu anataka ukweli
katika utendaji wake wa kazi.
No comments :
Post a Comment