Meneja wa TMDA Kanda ya Kaskazini, Proches Patrick akizungumza kwenye mkutano huo.
*****
Na Andrew Chale - Arusha
MAMLAKA ya Dawa na vifaa tiba (TMDA)
imekagua jumla ya shehena ya mizigo 3,160 ya dawa, vifaa tiba na
vitendanishi katika vituo vya Forodha vilivyopo Kanda ya Kaskazini.
Meneja wa TMDA Kanda ya Kaskazini,
Proches Patrick akizungumza ikiwa ni utekelezaji wa kampeni ya
Tumeboresha sekta ya afya yenye lengo la kuonyesha mafanikio na mipango
ya taasisi zote zilizo chini ya Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia
Wazee na Watoto.
Patrick alieleza kuwa, TMDA inatekeleza
majukumu yake kisheria ambapo ukaguzi huo umefanyika katika mipaka ya
Namanga, Holili, Tarakea pamoja na ule wa uwanja wa ndege wa KIA.
"Kwenye vituo vyote TMDA inawakaguzi na mfumo (IMIS) ambapo taarifa za vibali vya mizigo iliyokaguliwa huingizwa.".
"Katika kipindi cha miaka minne ya
Serikali ya awamu ya tano tumeweza kukagua shehena za mizigo 3,160 ya
dawa, vifaa tiba na vitendanishi kwenye vituo vya Forodha na mizigo
ambayo haikukidhi vigezo vya ubora, usalama na ufanisi iliteketezwa na
mingine kurudishwa kwenye nchi ilikotoka.
Lakini pia katika kipindi hicho, wametoa vibali mbalimbali na kuwa na ongezeko kubwa.
"Katika kipindi hiki ongezeko la maombi ya vibali vya kuingiza bidhaa za dawa, vifaa tiba na vitendanishi.
Jumla ya vibali 1,160 vilitolewa huu ni
ushahidi tosha kuwa elimu ya udhibiti kwa wadau wetu imeeleweka na
kukidhi sheria bila shuruti." Alisema.
Patrick ameongeza kuwa, uboreshaji wa
mifumo imesaidia kwa kutoa vibali kwa wateja wake ndani ya siku moja
baadala ya siku tatu ya awali
"Ikitokea sampuli haikukidhi vigezo
hatua za haraka huchukuliwa kuondoa bidhaa husika sokoni, kwa matokeo
ambayo hayakukidhi vigezo"alisema.
pia amesema wameweza kufanya ukaguzi wa
bidhaa katika maeneo kama famasi, maduka ya dawa muhimu, maghala,
hospitali, vituo vya afya na zahanati 5,017 yalikaguliwa katika
halamashauri 21 zinazosimiwa na TMDA.
"Tumekagua na kusajili maeneo ya
biashara 514, pia kufuatilia ubora na usalama wa bidhaa sokoni, vilevile
katika miaka minne ya Dk. Magufuli tumechukua sampuli 427 na kufanyia
vipimo" alisema.
Kwa upande wake, Mkaguzi wa Dawa TMDA Kanda ya Kaskazini, Titus Malulu alisema uelewa wa wananchi umekuwa mkubwa.
Ambapo wamekuwa wakitoa taarifa kwa bidhaa zilizowaletea madhara.
Katika upimaji wa dawa alisema wamekuwa
wakifanya mara kwa mara hasa kwa kununua ambazo tayari zipo sokoni
lengo kuendelea kufuatilia ubora wake.
"Kama tutabaini inashida tutapeleka
katika maabara yetu ya ubora Dar es salaam na wakipata kuwa zinashida
tunaziondoa haraka sokoni"alisema

No comments :
Post a Comment